Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Watu Wanakufa?

Sababu Gani Watu Wanakufa?

Jibu la Biblia

 Ni kawaida kujiuliza sababu gani watu wanakufa, zaidi sana wakati tunapoteza ndugu ao rafiki yetu wa karibu. Biblia inasema hivi: ‘Muchomo unaotokeza kifo ni zambi.’​—1 Wakorintho 15:56.

Sababu gani watu wote wanafanya zambi na kufa?

 Mwanaume na mwanamuke wa kwanza, Adamu na Eva, walipoteza uzima wao kwa sababu walimukosea Mungu. (Mwanzo 3:17-19) Walipaswa kufa kwa sababu walimuasi Mungu, ambaye ni “chemchemi ya uzima.”​—Zaburi 36:9; Mwanzo 2:17.

 Adamu aliwapitishia wazao wake wote matokeo ya zambi. Bibilia inasema hivi: ‘kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.’ (Waroma 5:12) Watu wote wanakufa kwa sababu wote wanafanya zambi.​—Waroma 3:23.

Kifo kitaondolewa namna gani?

 Mungu ameahidi wakati ambapo “atameza kifo milele.” (Isaya 25:8) Ili aondoe kifo, anapaswa kuangamiza mizizi inayoleta kifo, ni kusema, zambi. Mungu atafanya hivyo kupitia Yesu Kristo ambaye ‘anaondoa mbali zambi ya ulimwengu.’​—Yohana 1:29; 1 Yohana 1:7.