Sababu Gani Watu Wanakufa?
Jibu la Biblia
Ni kawaida kujiuliza sababu gani watu wanakufa, zaidi sana wakati tunapoteza ndugu ao rafiki yetu wa karibu. Biblia inasema hivi: ‘Muchomo unaotokeza kifo ni zambi.’—1 Wakorintho 15:56.
Sababu gani watu wote wanafanya zambi na kufa?
Mwanaume na mwanamuke wa kwanza, Adamu na Eva, walipoteza uzima wao kwa sababu walimukosea Mungu. (Mwanzo 3:17-19) Walipaswa kufa kwa sababu walimuasi Mungu, ambaye ni “chemchemi ya uzima.”—Zaburi 36:9; Mwanzo 2:17.
Adamu aliwapitishia wazao wake wote matokeo ya zambi. Bibilia inasema hivi: ‘kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.’ (Waroma 5:12) Watu wote wanakufa kwa sababu wote wanafanya zambi.—Waroma 3:23.
Kifo kitaondolewa namna gani?
Mungu ameahidi wakati ambapo “atameza kifo milele.” (Isaya 25:8) Ili aondoe kifo, anapaswa kuangamiza mizizi inayoleta kifo, ni kusema, zambi. Mungu atafanya hivyo kupitia Yesu Kristo ambaye ‘anaondoa mbali zambi ya ulimwengu.’—Yohana 1:29; 1 Yohana 1:7.