Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wakati Musiba wa Asili Unatokea

Wakati Musiba wa Asili Unatokea

“Mwanzoni, tulijisikia wenye kuvunjika moyo sana. Kila kitu chenye tulikuwa nacho kilikuwa kimeharibiwa na matope na maji mingi ya mvua.”​—Andrew, katika Sierra Leone.

“Kisha upepo mukubwa, tulirudia ku nyumba yetu. Tulipoteza kila kitu. Hatukujua tuseme nini. Mutoto wangu mwanamuke, alipiga magoti chini na kulia.”​—David, katika îles Vierges.

IKIWA umekwisha kuokoka musiba fulani wa asili, unaweza kuelewa namna watu wengine wenye waliokoka walijisikia: kuhuzunika sana, kukataa kukubali hali, kuvurugika, kuwa na mahangaiko, na kuota ndoto zenye kuogopesha. Watu wengi wenye wanaokoka wanajisikia wenye kuchoka na wenye kuvunjika moyo sana hivi kwamba hawana hata tamaa ya kuendelea na maisha.

Ikiwa umepoteza kila kitu kwa sababu ya musiba wa asili, wewe pia unaweza kujisikia kama hautaweza tena kuvumilia. Unaweza hata kuwaza kama maisha yako haina tena maana. Lakini, Biblia inafundisha kama maisha yako iko na maana na kama unaweza kuwa na sababu za muzuri za kutumaini kwamba wakati wenye kuja utakuwa muzuri zaidi.

KUJUA KWELI YA BIBLIA KUNAFANYA MAISHA IKUWE NA MAANA

Andiko la Muhubiri 7:8 linasema hivi: “Mwisho wa jambo ni muzuri zaidi kuliko mwanzo wake.” Wakati tu uko unaanza kupona musiba fulani wa asili, unaweza kuona kama maisha yako haitakuwa tena muzuri. Lakini, wakati unatumika kwa uvumilivu ili kutengeneza tena maisha yako, mambo inaweza kuwa tena muzuri zaidi.

Biblia inatabiri wakati wenye “sauti ya kulia wala kilio cha taabu havitasikika tena.” (Isaya 65:19) Jambo hilo litafanyika wakati dunia itageuzwa kuwa paradiso chini ya Ufalme wa Mungu. (Zaburi 37:11, 29) Hakutakuwa tena misiba ya asili. Kumbukumbu yoyote ya mambo yenye kuumiza na maumivu ya kimwili na ya moyoni vitaondolewa milele, kwa sababu Mungu Mweza-Yote anaahidi hivi: “Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayataingia katika moyo.”​—Isaya 65:17.

Waza kidogo: Muumbaji amepanga ‘kukupatia wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini’​—maisha yenye amani chini ya utawala mukamilifu wa Mungu. (Yeremia 29:11) Je, kujua kweli hiyo kunaweza kufanya maisha yako ikuwe na maana? Sally, mwenye tulizungumuzia katika habari ya kwanza anasema hivi: “Kujikumbusha mambo ya muzuri sana yenye Ufalme wa Mungu utatufanyia wakati wenye kuja kunaweza kukusaidia usikazie akili mambo ya zamani na kutakusaidia uvumilie hali yako ya sasa.”

Tunakutia moyo ujifunze mingi zaidi kuhusu mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanyia wanadamu hivi karibuni. Ukifanya vile, unaweza kuwa hakika kuwa hata kama ulipatwa na musiba wa asili, maisha yako iko na maana sasa kadiri unangojea kwa hamu wakati wenye hakutakuwa misiba ya asili. Lakini kwa sasa, Biblia inatoa mashauri yenye kufaa yenye inaweza kukusaidia kuvumilia matokeo ya musiba wa asili. Fikiria mifano fulani.