Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Upendo unatuchochea kutafuta kwanza faida za wengine

Tunapaswa Kupenda Wanadamu Wenzetu juu Tupate Baraka

Tunapaswa Kupenda Wanadamu Wenzetu juu Tupate Baraka

Juu tuko wazao wa mwanaume wa kwanza, Adamu, sisi wote tuko familia moja. Hata kama inatazamiwa kwamba watu wa familia moja wapendane na kuheshimiana, leo ni nguvu kuona ile. Ile haiko njo yenye Mungu wetu mwenye upendo anataka.

MAMBO YENYE MAANDIKO MATAKATIFU INASEMA KUHUSU UPENDO

“Unapaswa kumupenda mwenzako kama wewe mwenyewe.”​—MAMBO YA WALAWI 19:18.

“Muendelee kupenda maadui wenu.”​—MATAYO 5:44.

INAMAANISHA NINI KUPENDA WANADAMU WENZETU?

Ona namna Mungu anafasiria upendo mu Neno lake kwenye 1 Wakorinto 13:4-7:

“Upendo ni wenye uvumilivu na wenye fazili.”

Fikiri kidogo: Unajisikiaka namna gani wakati wengine wanakuvumilia na kukutendea kwa fazili na wakati hawakukasirikie juu ya makosa yako?

“Upendo hauna wivu.”

Fikiri kidogo: Unajisikiaka namna gani wakati wengine hawakuamini ao wanakusikilia wivu?

Upendo “hautafute faida zake wenyewe.”

Fikiri kidogo: Unajisikiaka namna gani wakati wengine wako tayari kuheshimia mawazo yako na hawakukaze ufuate tu mawazo yao?

Upendo “hauweke hesabu ya ubaya.”

Fikiri kidogo: Mungu iko tayari kusamehe watu wenye walimukosea kama wanatubu. “Hatatafuta makosa sikuzote, wala hataendelea kuwa na kinyongo.” (Zaburi 103:9) Tunafurahi wakati mutu mwenye tulikosea anatusamehe. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa tayari kusamehe wengine wakati wanatukosea.​—Zaburi 86:5.

Upendo “haufurahie ukosefu wa haki.”

Fikiri kidogo: Wakati tunapatwa na jambo la mubaya, hatupendake wengine wafurahi juu ya ile. Kwa hiyo, hatupaswe kufurahi wakati wengine wanapata mateso, hata ikiwa wametutendea mubaya.

Juu tupate baraka za Mungu, tunapaswa kupenda wengine bila kuangalia miaka, inchi ao dini yao. Njia moja ya kufanya vile ni kusaidia wenye wako na lazima ya musaada.