Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mungu, “Musikiaji wa sala,” anafurahiaka kutusikiliza.​—ZABURI 65:2

Endelea Kusali juu Ukubaliwe na Mungu

Endelea Kusali juu Ukubaliwe na Mungu

Mungu alipatia wanadamu zawadi ya pekee, ni kusema, uwezo wa kuongea naye na wa kumuelezea namna wanajisikia kupitia sala. Nabii Daudi alisali: “Ee Musikiaji wa sala, watu wa namna zote watakuendea.” (Zaburi 65:2) Lakini tunaweza kusali namna gani ili Mungu atusikie na kutubariki?

USALI KWA UNYENYEKEVU, NA USEME MAMBO YENYE IKO MU MOYO

Sala zako za kipekee zinakusaidia umwange moyo wako mbele ya Mungu, ni kusema, kumuelezea namna unajisikia kabisa. (Zaburi 62:8) Mweza-Yote anapenda sala zenye zinatoka mu moyo.

ZUNGUMUZA NA MUNGU KWA KUTUMIA JINA LAKE LA KIPEKEE

Hata kama Mungu iko na majina mingi ya cheo, iko na jina moja tu la kipekee. “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu.” (Isaya 42:8) Jina Yehova linapatikana karibu mara 7000 mu Maandiko Matakatifu. Manabii wengi walizungumuza na Mungu kwa kutumia jina lake la kipekee. Abrahamu alisema: “Tafazali Yehova, . . . acha niendelee kusema [na wewe].” (Mwanzo 18:30) Sisi pia tunapaswa kutumia jina la Mungu, Yehova, wakati tunasali.

SALI MU LUGA YAKO

Mungu anaelewa mawazo na hisia zetu hata kama tunazungumuzaka luga gani. Neno lake linatuhakikishia hivi: “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.”​—Matendo 10:34, 35.

Lakini, zaidi ya kusali, kuko mambo ingine yenye tunapaswa kufanya juu Mungu atubariki. Mu habari zenye kufuata, tutaona ile mambo.