Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Ni kweli kwamba zamani mutu fulani angepanda kabisa magugu katika shamba la mutu mwengine?

Kopi hii ya 1468 ya Digest ya Mutawala Justinien ni moja kati ya maandishi yenye habari nyingi juu ya mambo ya sheria ya wakati wa zamani

KULINGANA na Mathayo 13:24-26, Yesu alisema hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekuwa kama mutu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake. Watu wakiwa wamelala usingizi, adui yake alikuja na kupanda magugu katikati ya ngano, naye akaondoka. Wakati jani lilipoota na kuzaa matunda, magugu yalionekana pia.’ Waandikaji fulani wako na mashaka kama mambo yenye kuzungumuziwa katika mufano huo yalikuwa yanafanyika kabisa, lakini kulingana na maandishi ya zamani ya sheria ya Roma, jambo hilo lingefanyika.

Kamusi moja ya Biblia inasema kama kulingana na sheria ya Roma, kupanda magugu katika shamba la mutu mwengine ili kulipiza kisasi ilikuwa kuvunja sheria. Jambo hilo lilifanyika kabisa kwa sababu kulikuwa sheria yenye kulizungumuzia. Alastair Kerr, mutu mwenye elimu ya mambo ya sheria, alisema kama katika mwaka wa 533 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Mutawala wa Roma Justinien alitoa maandishi yake yenye kuitwa Digest. Maandishi hayo yalikuwa kifupi cha sheria ya Roma na yalikuwa na maelezo mbalimbali ambayo watu wenye elimu walitoa juu ya sheria hiyo kuanzia mwaka wa 100-250 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu. Kulingana na Digest, Ulpian, mumoja kati ya watu hao wenye elimu, alizungumizia jambo moja lenye lilifanyika kati ya mwaka wa 101 na 200. Magugu yalikuwa yamepandwa katika shamba la mutu fulani na hilo liliharibu mimea. Digest inazungumuzia haki za mwenye shamba zenye zingemuruhusu apate malipo kutoka kwa mutu mwenye alipanda magugu, ni kusema, feza kwa ajili ya mimea yenye iliharibika.

Mambo hayo yalifanyika katika Utawala wa zamani wa Roma, hilo linaonyesha kama mambo yenye kuzungumuziwa katika mufano wa Yesu yalifanyika kabisa.

Wakati wa mitume, Roma ilipatia viongozi Wayahudi wa Yudea uhuru kwa kadiri gani?

WAKATI huo, Yudea ilitawaliwa na Waroma; waliwakilishwa na gavana mwenye kuongoza kikundi cha askari. Kazi yake kubwa ilikuwa kukusanya kodi kwa ajili ya Roma na kufanya kukuwe amani na utaratibu. Waroma walikuwa wanakataza mambo yenye hayakupatana na sheria na kupatia malipizi mutu yeyote mwenye kuleta muvurugo. Lakini, mara nyingi Waroma waliachia watu wenye mamlaka wa jimbo wasimamie mambo ya kawaida ya eneo hilo.

Mukutano wa Sanhedrini ya Wayahudi

Sanhedrini ilikuwa tribinali kubwa ya Wayahudi na baraza lenye kusimamia mambo yenye kuhusu sheria ya Wayahudi. Kulikuwa pia tribinali ndogo-ndogo katika Yudea yote. Inawezakana watawala Waroma waliruhusu tribinali hizo kuhukumu raia na watu wenye kufanya makosa makubwa. Lakini, tribinali za Wayahudi hazikupewa ruhusa ya kuua watu wenye kufanya makosa makubwa. Kwa kawaida watawala Waroma tu ndiyo walikuwa na haki ya kufanya hivyo. Hali ya pekee yenye kujulikana sana ilitokea wakati Stefano alisambishwa na watu wa Sanhedrini na kuruhusu apigwe majiwe mupaka kifo.​—Mdo. 6:8-15; 7:54-60.

Kwa hiyo, Sanhedrini ya Wayahudi ilikuwa na mamlaka makubwa. Lakini, Emil Schürer, mutu mwenye elimu, anasema kama “mipaka yake ya juu kabisa ilikuwa kwamba watawala Waroma wangeingilia mambo wakati wowote na kuyashugulikia wao wenyewe bila kuomba Sanhedrini ruhusa, kama vile walifanya wakati waliona jambo fulani lenye halipatane na sheria ya Waroma.” Kwa mufano, jambo kama hilo lilitokea wakati Klaudio Lisia, kiongozi wa jeshi, alilinda mutume Paulo, raia Muroma.​—Mdo. 23:26-30.