Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Uzinifu

Uzinifu

Watu wanafundishwa sana kuwa waaminifu katika ndoa, lakini uzinifu unaendelea kuleta magumu katika familia nyingi.

Uzinifu ni nini?

MAMBO WATU WANASEMA

Watu wa desturi fulani wanaona kuwa haiko makosa kufanya kitendo cha ndoa na mutu mwenye haiko bibi ao bwana yako, zaidi sana ikiwa ni bwana ndiye anafanya hivyo. Na wengine hawaone ndoa kuwa muungano wa maisha yote.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Katika Biblia, mara nyingi neno uzinifu linatumiwa wakati mutu mwenye kuoa ao kuolewa anafanya kitendo cha ndoa na mutu mwengine mwenye haiko bibi ao bwana yake. (Ayubu 24:15; Methali 30:20) Mungu anachukia sana uzinifu. Katika Israeli ya zamani, mutu mwenye alifanya uzinifu alipaswa kuuawa. (Mambo ya Walawi 18:20, 22, 29) Yesu alifundisha kuwa wanafunzi wake wanapaswa kuepuka uzinifu.—Mathayo 5:27, 28; Luka 18:18-20.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Wakati mutu anafanya uzinifu, anavunja kiapo kizito chenye alifanya kwa bibi ao bwana yake wakati walifunga ndoa. Pia, uzinifu ni ‘kumutendea Mungu zambi.’ (Mwanzo 39:7-9) Uzinifu unaweza kutenganisha bila huruma watoto na wazazi wao. Na zaidi ya hayo, Biblia inaonyesha kuwa “Mungu atawahukumu . . . wazinzi [wazinifu].”—Waebrania 13:4.

“Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi [uchafu].”Waebrania 13:4.

Uzinifu unavunja ndoa?

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia inaruhusu mutu mwenye kuoa ao kuolewa avunje ndoa yake ikiwa tu bibi ao bwana yake anafanya uzinifu. (Mathayo 19:9) Hilo linamaanisha kuwa bibi ao bwana asiyekuwa na kosa iko na haki ya kuamua ikiwa atabakia na bibi ao bwana yake mwenye alifanya uzinifu, ao ikiwa atavunja ndoa. Huo ni uamuzi wa mutu yeye mwenyewe.—Wagalatia 6:5.

Zaidi ya hiyo, Mungu anaona ndoa kuwa muungano mutakatifu wa maisha yote. (1 Wakorintho 7:39) Mungu anachukia wakati mutu anatafuta kuvunja ndoa yake kwa sababu ya mambo madogo-madogo, kama vile kujisikia tu kuwa hafurahie bibi ao bwana yake. Kwa hiyo, uamuzi wa kuvunja ndoa haupaswe kukamatwa kwa muchezo.—Malaki 2:16; Mathayo 19:3-6.

‘Ninawaambia ninyi kwamba kila mutu anayemutaliki muke wake, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, anamuweka katika hali ya kuweza kufanya uzinzi.’Mathayo 5:32.

Uzinifu ni zambi yenye haiwezi kusamehewa?

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia inasema hapana. Inasema kuwa Mungu anasamehe watu wenye kutubu na kuacha zambi zao, hata zambi ya uzinifu. (Matendo 3:19; Wagalatia 5:19-21) Biblia inazungumuzia wanaume na wanawake wenye waliacha kufanya uzinifu na kisha wakakuwa marafiki wa Mungu.—1 Wakorintho 6:9-11.

Mungu alimusamehe Mufalme Daudi wa Israeli ya zamani. Daudi alifanya uzinifu na bibi ya askari wake mumoja. (2 Samweli 11:2-4) Biblia inaonyesha waziwazi kuwa ‘jambo ambalo Daudi alikuwa amefanya lilikuwa mbaya’ machoni pa Yehova. (2 Samweli 11:27) Kisha kukaripiwa, Daudi alitubu na Mungu akamusamehe. Lakini, Daudi alipaswa kupata matokeo mabaya ya matendo yake. (2 Samweli 12:13, 14) Kisha muda kupita, Mufalme Sulemani mwenye hekima alisema kuwa “yeyote anayefanya uzinzi . . . amepungukiwa moyoni.”—Methali 6:32.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Ikiwa umefanya uzinifu, ni lazima umuombe Mungu akusamehe, na pia umuombe bibi ao bwana yako akusamehe. (Zaburi 51:1-5) Ujifunze kuchukia uzinifu kama Mungu. (Zaburi 97:10) Uepuke pornografia, kuwazia-wazia unafanya kitendo cha ndoa na mutu asiyekuwa bibi ao bwana yako, kuchezea wengine kimapenzi. Uepuke pia kila kitu chenye kinaweza kufanya utamani mutu mwenye haiko bibi ao bwana yako.—Mathayo 5:27, 28; Yakobo 1:14, 15.

Ikiwa bibi ao bwana yako amefanya uzinifu, ukuwe hakika kama Mungu anaelewa namna unajisikia. (Malaki 2:13, 14) Umuombe akutulize na kukuongoza, “naye mwenyewe atakutegemeza.” (Zaburi 55:22) Ukiamua kusamehe bibi ao bwana yako na kuendelea na ndoa yenu, ni lazima ninyi wawili mufanye nguvu sana ili kuwa tena na muungano katika ndoa yenu.—Waefeso 4:32.

Kisha Daudi kutubu zambi yake ya uzinifu, nabii Nathani alimuambia hivi: ‘Yehova ameacha zambi yako ipite.’2 Samweli 12:13.