Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA

Unafanya Mambo Mengi?

Unafanya Mambo Mengi?

Unajisikia kama uko na mambo mengi ya kufanya? Kama ni hivyo, hauko peke yako. Gazeti The Economist linasema hivi: “Kila mahali, watu wote wanaonekana kuwa na mambo mengi ya kufanya.”

KATIKA uchunguzi moja wa mwaka wa 2015 kuhusu wafanyakazi wa wakati wote katika inchi munane, wengi wenye waliulizwa walisema kwamba wanaona kuwa ni vigumu kutimiza mambo yenye wanaombwa katika kazi na yenye wanaombwa katika familia zao. Kati ya sababu hizo kuna kuongezeka kwa madaraka katika kazi, kuongezeka kwa garama (dépenses), kufanya saa nyingi katika kazi. Kwa mufano, katika inchi ya États-Unis, wafanyakazi wa wakati wote wanasema kwamba wanatumika karibu saa 47 kila juma. Karibu mutu 1 juu ya watu 5 alisema kwamba anatumika saa 60 ao zaidi!

Katika uchunguzi mwingine wenye ulifanywa katika inchi 36, zaidi ya mutu 1 juu ya watu 4 walisema kwamba wanafanya mambo haraka-haraka hata katika wakati wao wa kupumuzika! Hali hiyo inaweza pia kufikia watoto kama wako na kazi nyingi sana ya kufanya moja kisha ingine.

Wakati tunaendelea kujikaza kufanya mambo mengi zaidi kuliko namna wakati unaruhusu, tunaweza kuwa na mikazo​—kupatwa na hali yenye imeitwa “musongo wa wakati.” Lakini inawezekana kuwa na maisha yenye usawaziko zaidi? Mipango yetu, mambo yenye tunaamini, na mambo yenye tunachagua yanaweza kuchangia namna gani? Kwanza, tuchunguze sababu ine zenye kufanya watu fulani wajikaze kufanya mambo mengi.

1 TAMAA YA KUTAKA KUTIMIZA MUZURI MAHITAJI YA FAMILIA

Baba mumoja mwenye kuitwa Gary anasemahivi: “Nilitumika siku saba katika juma. Nilifanya hivyo kwa sababu sikuzote kulikuwa jambo la muzuri lenye nilipenda kupatia watoto wangu. Nilipenda wapate vitu vyenye sikupataka.” Hata kama wako na nia nzuri, wazazi wanapaswa kuchunguza mambo yao ya kutia pa nafasi ya kwanza. Uchunguzi mbalimbali unaonyesha kwamba watu wazima na watoto wenye wanatia feza na vitu vya kimwili pa nafasi ya kwanza wako na mwelekeo wa kukosa furaha, hawatosheke katika maisha, na hawana afya nzuri ya kimwili kama vile wale wenye hawatie vitu vya kimwili pa nafasi ya kwanza.

Watoto wenye wanafundishwa na wazazi wao kukazia akili vitu vya kimwili hawana furaha kabisa

Ili kutafuta watoto wao wakuwe na furaha katika siku zenye kuja, wazazi fulani wanapanga kufanya mambo mengi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya watoto wao. Kitabu Putting Family First (Kutia Familia pa Nafasi ya Kwanza) kinasema kwamba wazazi kama hao hata kama wako na nia nzuri, “matokeo ni kwamba watoto na wazazi wanateseka.”

2 KUWAZA KWAMBA NI ‘MUZURI ZAIDI KUWA NA MALI NYINGI’

Watu wenye kufanya matangazo ya biashara wanajikaza kutufanya tuamini kwamba tunajiima mambo mengi kama hatuuze vitu vyao vya sasa. Kulingana na gazeti The Economist: “Kutokea kwa vitu vingi vya kuuza kunafanya watu wajisikie kama hawana wakati wa kutosha,” kadiri watu wenye kuuza “wanajaribu kuchagua nini watauza ao wataangalia ao watakula” katika wakati kidogo ambao wako nao.

Katika mwaka wa 1930, mutu mumoja mwenye elimu ya mambo ya feza alisema kwamba maendeleo katika mambo ya teknolojia yangefanya wafanyakazi wapumuzike zaidi. Alidanganyika kabisa! Elizabeth Kolbert, mumoja wa waandikaji wa gazeti New Yorker, alisema hivi: “Kuliko kuondoka mbele ya wakati katika [kazi],” watu “wanapata vitu vipya vyenye wako navyo lazima”​—na vitu hivyo vinaomba feza na wakati mwingi.

3 KUJIKAZA KUTIMIZA MAMBO YENYE WENGINE WANATAZAMIA

Wafanyakazi fulani wanatumika saa nyingi zenye kuchokesha ili kuepuka kukosa kufurahisha wakubwa wao wa kazi. Wafanyakazi wengine wanaweza kuchochea watu wenye wanafanya nao kazi wajisikie kuwa na hatia kama hawakawie katika kazi. Na watu hawajue kama hali ya maisha itakuwa namna gani, hilo linafanya watumike sana kwa muda wa saa nyingi ao kuwa tayari kuenda kutumika wakati wowote.

Vilevile, wazazi wanaweza kujisikia kuwa wenye kukazwa wakati wanajaribu kujipatanisha na familia zingine. Kama hawajipatanishe, wanaweza kujisikia wenye makosa kuhusu “kuima” watoto wao mambo yenye wako nayo lazima.

4 KUTAFUTA KUJULIKANA NA KUTAKA KUTIMIZA MIPANGO FULANI

Tim, mwenye anaishi États-Unis, anasema hivi: “Nilipenda sana kazi yangu, na nilijikaza kutumika sana wakati wote. Niliwaza kwamba nilipaswa kuonyesha uwezo wangu.”

Kama vile Tim, wengi wanaona kama kuna upatano mukubwa kati ya namna mutu anajiona na maisha yake. Matokeo? Elizabeth Kolbert mwenye tumekwisha kutaja anasema: “Watu wengi wameona kwamba kuwa na mambo mengi ya kufanya ni jambo la maana sana.” Anaongeza hivi: “Unaonekana kuwa mutu wa maana zaidi kadiri unakuwa na mengi ya kufanya.”

UJIFUNZE KUWA NA USAWAZIKO

Biblia inatia moyo kufanya kazi kwa bidii. (Methali 13:4) Lakini inatutia moyo pia kuwa na usawaziko. Mhubiri 4:6 inasema hivi: ‘Konzi moja ya pumuziko ni afazali kuliko konzi mbili za kazi ngumu na kufuatilia upepo.’

Kuwa na maisha yenye usawaziko ni muzuri kwa ajili ya afya yetu ya kimwili na ya kiakili. Lakini inawezekana kabisa kupunguza hali hiyo? Ndiyo. Tuzungumuzie mashauri ine:

1 UJUE MUZURI MAMBO YENYE UNAPENDA NA MIPANGO YAKO

Ni jambo la kawaida kuwa na kiasi fulani cha feza chenye kinaweza kufanya ujisikie salama. Lakini inaomba kuwa na kiasi gani cha feza? Ni nini inaonyesha kwamba mutu iko na maisha ya muzuri? Ni kupitia tu feza ao vitu vya kimwili? Lakini, kupumuzika sana na kujifurahisha sana kunaweza kuongeza musongo wa wakati.

Tim, mwenye tumekwisha kutaja, anasema hivi: “Mimi na bibi yangu tulichunguza muzuri maisha yetu na tuliamua kuyafanya kuwa mepesi. Tulifanya liste yenye kuonyesha hali yetu ya sasa na mipango yetu mipya. Tulizungumuzia matokeo ya maamuzi yetu ya zamani na mambo yenye tulikuwa nayo lazima ili kutimiza mipango yetu.”

2 USICHOCHEWE NA WATU WENYE KUWAZA KWAMBA MAISHA MAZURI NI KUWA NA VITU VINGI VYA KIMWILI

Biblia inatushauri kuzuia “tamaa ya macho.” (1 Yohana 2:15-17) Matangazo ya biashara yanaweza kuchochea tamaa hizo, kwa kufanya mutu atumike saa nyingi ao ajiingize katika mambo ya kujifurahisha yenye kuchukua feza nyingi na yenye kupita mipaka. Ni kweli kwamba hauwezi kuepuka matangazo yote ya biashara. Lakini unaweza kupunguza uwezekano wako wa kuyafuata. Unaweza pia kuchunguza kwa uangalifu ni nini uko nayo lazima kabisa.

Kumbuka pia kwamba marafiki wako wanaweza kukuchochea kufanya jambo fulani. Kama wanapenda kufuatilia mambo ya kimwili ao wanawaza kwamba maisha mazuri ni kuwa na vitu vya kimwili, ni jambo la hekima utafute marafiki wenye wanajua mambo ya maana ya kutia pa nafasi ya kwanza. Biblia inasema hivi: “Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima.”​—Methali 13:20.

3 WEKEA KAZI YAKO MIPAKA

Uambie mukubwa wako wa kazi kuhusu kazi yako na mambo yenye unatia pa nafasi ya kwanza. Na usijisikie mubaya kuwa na maisha yenye kuwa mbali na kazi yako. Kitabu Work to Live (Kutumika Ili Kuishi) kinasema: “Wale wenye wanatia mipaka kati ya kazi na mambo ya nyumbani ao wenye wanakamata mapumuziko wametambua jambo nzuri sana: Hakuna hatari fulani yenye inatokea wakati unaenda.”

Gary, mwenye tumekwisha kutaja, alikuwa na feza nyingi, kwa hiyo aliamua kupunguza saa zake za kazi. Anasema hivi: “Nilizungumuza na watu wa familia yangu ili kuona kama tungefanya maisha yetu yakuwe mepesi. Kisha, tulifanya hivyo hatua kwa hatua. Nilizungumuza pia na mukubwa wangu wa kazi ili apunguze siku zangu za kutumika katika juma, na aliitika.”

4 UONE WAKATI WENYE UNAPITISHA KATIKA FAMILIA KUWA WA MAANA SANA

Bibi na bwana wanapaswa kupitisha wakati pamoja, na watoto wako na lazima ya kupitisha wakati pamoja na wazazi wao. Kwa hiyo, epuka kujipatanisha na familia nyingine zenye kufanya mambo mengi sikuzote. Gary anashauri hivi: “Ujiwekee wakati wa kupumuzika na kujifurahisha na uache kufanya mambo yenye hayako ya lazima.”

Wakati muko pamoja katika familia, musiruhusu televizyo, telefone, ao chombo kingine kiwazuie kuzungumuza. Mukule pamoja hata mara moja kwa siku, na mutumie wakati wa kula ili kuzungumuza katika familia. Wakati wazazi wanafuata shauri hilo, watoto wao wanakuwa wenye furaha na wanapata matokeo mazuri kwenye masomo.

Mutumie wakati wa kula ili kuzungumuza katika familia

Kwa kumalizia, ujiulize hivi: ‘Napenda nini katika maisha? Napenda nini kwa ajili ya familia yangu?’ Kama unapenda kuwa na maisha mazuri na yenye kusudi, utie pa nafasi ya kwanza mambo yenye kupatana na hekima yenye kuwa katika Biblia.