Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Afya ya Kimwili

Afya ya Kimwili

Biblia haiko kitabu cha mambo ya matunzo. Lakini, iko na kanuni zenye zinaweza kutusaidia tukuwe na afya ya muzuri. Ona kanuni fulani za Biblia zenye zinaweza kufanya afya yako ya kimwili ikuwe ya muzuri zaidi.

HANGAIKIA MWILI WAKO

KANUNI YA BIBLIA: “Hakuna mutu mwenye anachukia mwili wake; lakini anaukulisha na kuutunza kwa upendo.”​—Waefeso 5:29.

ILE INAMAANISHA NINI? Hii kanuni ya Biblia inatutia moyo kufanya yote yenye tunaweza ili kutunza afya yetu ya kimwili. Uchunguzi moja unaonyesha kama matatizo mingi ya afya inatokana na namna yenye watu wanachagua kuishi. Kwa hiyo, kufanya maamuzi ya muzuri kunaweza kufanya mutu akuwe na afya ya muzuri zaidi.

KILE UNAWEZA KUFANYA:

  • Chakula. Uhangaikie afya yako kwa kutumia chakula cha muzuri kwa afya na kwa kunywa maji ya mingi.

  • Fanya mazoezi kwa ukawaida. Kufanya mazoezi kunaweza kufanya afya yako ikuwe ya muzuri zaidi hata kama umezeeka, ao uko na ulemavu fulani ao ugonjwa wenye kukawia. Watu wa familia, marafiki ao wanganga wanaweza kukusaidia kufanya ile mazoezi, lakini unapaswa kufanya jambo fulani juu ile mazoezi ikuletee faida!

  • Lala saa za kuenea. Kuwa na tabia ya kulala saa za kidogo kunaweza kuleta magonjwa yenye kuwa hatari sana. Kwa sababu watu mingi wanachagua kufanya mambo ingine wakati wenye wangelala, ile inawafanya wasilale saa za kuenea. Lakini, wakati unachagua kulala saa za kuenea, ile inakusaidia ukuwe na maisha ya muzuri zaidi.

ACHANA NA TABIA ZA MUBAYA

KANUNI YA BIBLIA: “Tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho.”​—2 Wakorinto 7:1.

ILE INAMAANISHA NINI? Tunapata faida wakati hatuchafue mwili wetu na vitu vyenye kuwa hatari kwa afya kama vile tumbaku, yenye inajulikana kuwa inaleta magonjwa mingi na kifo.

KILE UNAWEZA KUFANYA: Chagua siku yenye utaacha ile tabia na uitie alama kwenye kalendari yako. Mbele ya ile siku, uachane na tumbaku, na kitu chochote chenye unatumia ili kuvuta, kama vile kiberiti (ao, allumette) ao kitu kingine. Epuka nafasi kwenye kuko watu wenye kuwa na tabia kama hizo. Ambia marafiki wako juu ya uamuzi wenye umekamata ili wakusaidie.

KANUNI ZINGINE ZA BIBLIA

Unaweza kupata Biblia yenye kuchapishwa kwa kumuona Shahidi wa Yehova wa mu eneo lenu

UHANGAIKIE USALAMA.

“Kama unajenga nyumba mupya, unapaswa pia kujenga ukuta mufupi kwa ajili ya sehemu ya juu ya nyumba yako, ili usilete hatia ya damu juu ya nyumba yako kwa sababu ya mutu kuanguka kutoka kwenye nyumba yako.”​—KUMBUKUMBU LA TORATI 22:8.

ZUIA KASIRANI YAKO.

“Mutu mwenye hakasirike haraka iko na utambuzi mwingi, lakini mwenye hana uvumilivu anaonyesha upumbavu wake.”​—MEZALI 14:29.

EPUKA KULA KUPITA KIASI.

“Usikuwe . . . kati ya wale wenye kula nyama nyingi sana.”​—MEZALI 23:20.