Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wakati Watoto Wanaonyesha Huzuni

Wakati Watoto Wanaonyesha Huzuni

Unahuzunika kwa sababu ya kifo cha mutu fulani wa familia? Kama ni hivyo, namna gani unaweza kupambana na huzuni yako? Ona namna Biblia ilisaidia vijana watatu wapambane na hali hiyo ngumu sana.

DAMI ANAELEZA HABARI YAKE

Dami

Kwanza ilionekana kuwa maumivu madogo tu ya kichwa. Lakini wakati maumivu ya baba yangu yaliendelea kuongezeka na hali kuwa mubaya zaidi, mama yangu aliita motokari ya kubeba wagonjwa. Naendelea kukumbuka namna wanganga-wasaidizi walimupeleka. Sikuwazia kama hiyo ilikuwa mara ya mwisho kumuona akiwa muzima. Kisha siku tatu, baba yangu alikufa kwa sababu kivimba kilikuwa katika ubongo wake. Nilikuwa tu na miaka sita.

Kwa miaka mingi, nilijihukumu kwa sababu ya kifo cha baba yangu. Katika akili yangu niliendelea kuona namna wanganga-wasaidizi walimupeleka, na nilijiuliza: ‘Sababu gani nilisimama pale tu? Sababu gani sikufanya jambo lolote?’ Niliona watu wenye kukomaa ambao walikuwa na magumu ya afya na kujiuliza, ‘Sababu gani wanaendelea kuishi lakini baba yangu hapana?’ Kadiri muda ulipita, mama yangu alinitia moyo nianze kusema namna ninajisikia. Na kwa sababu tuko Mashahidi wa Yehova, tulitegemezwa sana na kutaniko.

Watu fulani wanawaza kama mutu anaweza kuonyesha huzuni wakati tu musiba unatokea na kisha anasahau, lakini haikuwa hivyo kwangu. Nilianza kuonyesha huzuni yangu mwanzoni tu mwa miaka ya ujana.

Shauri lenye ninapatia vijana ambao muzazi wao amekufa ni hili: “Ambia mutu fulani mambo yenye unapambana nayo. Inaonekana kwamba kadiri unafunua haraka namna unajisikia, ndivyo afya yako inaendelea kuwa muzuri.”

Kwa kweli, ni vigumu kufanya mambo ya maana sana katika maisha yangu wakati ninajua kwamba baba yangu haiko pamoja na mimi. Lakini ninapata kitulizo kupitia ahadi ya Biblia yenye kuwa kwenye Ufunuo 21:4, yenye inasema kwamba Mungu “atafuta kila chozi kutoka katika macho [yetu], na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”

DERRICK ANAELEZA HABARI YAKE

Derrick

Kati ya mambo mazuri yenye ninakumbuka ni kuvua samaki pamoja na baba yangu na kupiga kambi katika milima. Alipenda milima.

Baba yangu alikuwa na matatizo ya moyo kwa wakati fulani; ninakumbuka nikimutembelea mara moja ao mara mbili hivi katika hospitali wakati nilikuwa mudogo sana. Lakini sikuwazia kama ugonjwa wake ulikuwa hatari. Baba yangu alikufa na ugonjwa wa moyo wakati nilikuwa na miaka kenda.

Wakati alikufa, nililia sana. Nilijisikia kama vile siweze tena kupumua, na sikupenda kuzungumuza na mutu yeyote. Ilikuwa mara yangu ya kwanza kujisikia mubaya hivyo katika maisha yangu, na sikupenda kufanya jambo lingine lolote. Nilikuwa katika kikundi cha vijana wa kanisa; mwanzoni walinihangaikia, lakini walichoka haraka. Wangeweza kusema mambo kama vile, “Ilikuwa siku yake” ao “Mungu alimuita baba yako” ao “Iko mbinguni sasa.” Sikutosheka kabisa na mawazo yao, lakini sikujua kama Biblia inafundisha nini juu ya mambo hayo.

Kisha, mama yangu alianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, na baadaye mimi na ndugu yangu tukajiunga naye. Tulijifunza juu ya hali ya wafu na pia juu ya ahadi ya Mungu yenye kufariji kuhusu ufufuo. (Yohana 5:28, 29) Lakini andiko lenye lilinisaidia zaidi ni Isaya 41:10. Katika andiko hilo Mungu anasema: “Usiogope, kwa maana mimi nipo pamoja nawe. Usitazame huku na huku, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu. Nitakusaidia kwelikweli.” Kujua kwamba Yehova alikuwa pamoja na mimi kulinituliza sana wakati wa huzuni, na hilo linaendelea kunituliza leo.

JEANNIE ANAELEZA HABARI YAKE

Jeannie

Wakati nilikuwa na miaka saba, mama yangu alikufa na kansere. Siku yote hiyo nilikuwa kama mwenye kuota ndoto. Ninakumbuka kwamba alikufia nyumbani na kwamba wazazi wa mama yangu walikuwa pale. Ninakumbuka pia kwamba watu wote walikuwa kimya. Ninakumbuka tena kwamba mangaribi hiyo tulikula mayai yenye kukaangwa. Nilijisikia kama maisha yangu yote yamevurugika.

Wakati huo, na kwa miaka mingi kisha jambo hilo kutokea, niliwaza kama nilipaswa kujionyesha kuwa mwenye nguvu kwa ajili ya dada yangu mudogo, kwa hiyo nilificha namna nilikuwa ninajisikia. Na hata mupaka leo, niko na mwelekeo wa kuficha huzuni yangu, na kufanya hivyo ni mubaya kwa afya.

Ninakumbuka namna Mashahidi wa Yehova wa kutaniko letu walituonyesha upendo na kututegemeza. Hata kama tulikuwa tu tumeanza kuhuzuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme, waamini wenzetu walituunga mukono. Ilikuwa kama vile tuko familia moja kwa miaka mingi. Siwaze kama baba yangu alipaswa kutupikia chakula mwaka muzima kwa sababu kila siku tulikuwa na chakula kingi kutoka kwa ndugu na dada wa kutaniko letu.

Andiko moja lenye linanigusa moyo zaidi ni Zaburi 25:16, 17. Katika andiko hilo, muandikaji wa zaburi alimuomba Mungu hivi: “Unielekezee uso wako, na unionyeshe kibali; kwa maana mimi niko peke yangu nami ni mwenye kuteseka. Taabu za moyo wangu zimeongezeka; uniondoe katika mikazo iliyo juu yangu.” Inafariji kujua kwamba hauko kabisa peke yako wakati uko katika huzuni. Mungu iko pale kwa ajili yako. Kupitia musaada wa Biblia, nimeweza kusonga mbele na kukaza akili juu ya mambo mazuri kama vile ahadi ya Biblia yenye kufariji kuhusu ufufuo. Niko na tumaini la kuona mama yangu tena na kumujua akiwa na afya kamilifu katika dunia paradiso.—2 Petro 3:13.

Ungependa kujifunza mengi zaidi kuhusu ujumbe wa Biblia wenye kufariji kwa ajili ya wale wenye kuhuzunika? Chukua kwenye Internete bila kulipa broshua “Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa.” Fungua www.pr418.com/sw, na angalia kwenye kichwa MACHAPISHO > VITABU & BROSHUA.