Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Wakati Muzazi Anakufa

Wakati Muzazi Anakufa

MAGUMU

Dami alikuwa na miaka sita wakati baba yake alikufa kwa sababu kivimba kilikuwa katika ubongo wake. Derrick alikuwa na miaka kenda wakati baba yake alikufa kwa sababu ya ugonjwa wa moyo. Jeannie alikuwa na miaka saba wakati mama yake alikufa kisha kugonjwa kansere ya ovari mwaka muzima. *

Vijana hao watatu walipambana na magumu ya kufiwa na mupendwa wakati walikuwa wangali wadogo sana. Jambo kama hilo limekwisha kukufikia? Kama ni hivyo, habari hii inaweza kukusaidia kupambana na magumu ya kufiwa na mupendwa. * Lakini, kwanza tuchunguze mambo fulani kuhusu kuonyesha huzuni.

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Tunaonyesha huzuni kwa njia tofauti. Hilo linamaanisha kwamba namna unaonyesha huzuni inaweza kuwa tofauti na namna wengine wanaonyesha huzuni. Kitabu Helping Teens Cope With Death kinasema hivi: “Kupambana na huzuni ya kufiwa hakufuate utaratibu fulani ao sheria fulani.” Jambo la maana ni kwamba haupaswe kuzuia huzuni kupita kiasi. Sababu gani? Kwa sababu . . .

Kuzuia huzuni kunaweza kuwa hatari. Jeannie, mwenye kutajwa kwenye mwanzo wa habari hii anasema hivi: “Niliwaza kama nilipaswa kumuonyesha dada yangu mudogo kwamba niko na nguvu ya kuvumilia kuliko yeye, kwa hiyo, sikuonyesha namna ninajisikia. Hata leo, niko na mwelekeo wa kuzuia huzuni yangu, lakini haiko muzuri kwa ajili ya afya.”

Wanasayansi wanakubaliana na jambo hilo. Kitabu The Grieving Teen kinasema hivi: “Hauwezi kuepuka ao kukataa kuonyesha hisia milele. Hisia hizo zitarudi wakati hauwazie kupitia mulipuko wa hasira ao matatizo ya afya.” Huzuni yenye mutu anazuia inaweza kumufanya atumie mubaya pombe ao dawa za kulewesha ili kupunguza maumivu.

Huzuni inaweza kufanya mutu avurugike katika namna anajisikia. Kwa mufano, watu fulani wanakasirikia mutu mwenye alikufa kwa sababu wanawaza kama mutu huyo “aliwaacha.” Wengine wanamulaumu Mungu kwa sababu wanawaza kwamba alipaswa kuzuia kifo kisitokee. Watu wengi wenye wanaonyesha huzuni wanajilaumu kuhusu mambo yenye walisema ao kutendea mutu mwenye alikufa kwa sababu hakuna tena namna ya kutengeneza mambo.

Ni wazi kwamba huzuni inatia ndani mambo mengi sana. Namna gani unaweza kupata kitulizo na musaada ili usonge mbele?

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Ambia mutu fulani namna unajisikia. Pengine unaweza kuwa na mwelekeo wa kujitenga na wengine katika wakati huu mubaya. Lakini kumufungulia moyo wako mutu wa familia ao rafiki kutakusaidia kupambana na hisia zako na kutakusaidia ili magumu ya kufiwa yasikulemee.—Kanuni ya Biblia: Methali 18:24.

Andika mambo fulani kuhusu mutu huyo. Andika mambo fulani kuhusu muzazi mwenye alikufa. Kwa mufano, unakumbuka mambo gani mazuri juu ya mutu huyo? Andika kuhusu sifa zake za muzuri. Ni sifa gani unapenda kuiga katika maisha yako?

Kama unasumbuliwa na mawazo yenye hayafae—kwa mufano, kama unaendelea kuwaza juu ya jambo la mubaya lenye uliambia muzazi wako mbele akufe—andika namna unajisikia na sababu gani. Kwa mufano, “Ninajilaumu kwa sababu nilibishana na baba yangu siku yenye ilitangulia kifo chake.”

Kisha, jaribu kuona kama uko na sababu ya kujilaumu. Kitabu The Grieving Teen kinasema hivi: “Haupaswe kujilaumu kwa sababu ya kukosa kujua kwamba hauna nafasi ya kuomba musamaha. Kuwaza kwamba mutu hapaswe kusema ao kufanya jambo lenye linaweza kumufanya aombe musamaha kisha, hakupatane na akili.”—Kanuni ya Biblia: Ayubu 10:1.

Hangaikia afya yako. Pumuzika vya kutosha, fanya mazoezi ya kutosha, na kula chakula chenye kufaa. Kama hauna hamu ya kula, ukuwe na vyakula vyepesi vyenye kujenga mwili ambavyo utatumia katika siku yote nzima kuliko kula chakula kizito. Ufanye hivyo mupaka wakati utakuwa tena na hamu ya kula. Usitulize huzuni yako kwa kutumia chakula chenye hakifae ao kwa kutumia pombe; kufanya hivyo kunaharibisha mambo zaidi.

Zungumuza na Mungu katika sala. Biblia inasema hivi: ‘Mutupie Yehova muzigo wako, naye mwenyewe atakutegemeza.’ (Zaburi 55:22) Mutu hatoe sala ili ajisikie muzuri tu. Sala ni mazungumuzo ya kweli pamoja na Mungu mwenye ‘anatufariji katika ziki yetu yote.’—2 Wakorintho 1:3, 4.

Njia moja yenye Mungu anatumia ili kufariji wale wenye kuomboleza ni Neno lake, Biblia. Sababu gani usichunguze mambo Biblia inafundisha kuhusu hali ya wale wenye wamekufa na tumaini la ufufuo? *Kanuni ya Biblia: Zaburi 94:19.

^ fu. 4 Unaweza pia kusoma habari kuhusu mambo yenye yalipata Dami, Derrick, na Jeannie katika habari yenye kufuata.

^ fu. 5 Hata kama habari hii inahusu kifo cha muzazi, kanuni zenye kuzungumuziwa zinaweza pia kutumiwa wakati ndugu ao dada wa kimwili ao rafiki anakufa.

^ fu. 19 Ona sura ya 16 ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1. Unaweza kukichukua bila kulipa kwenye www.pr418.com/sw. Fungua kichwa MACHAPISHO.