Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA WALE WENYE WAMEFIWA NA MUPENDWA WAO

Namna ya Kupambana na Huzuni—Mambo Yenye Unaweza Kufanya Leo

Namna ya Kupambana na Huzuni—Mambo Yenye Unaweza Kufanya Leo

Kama unatafuta mashauri juu ya namna ya kupambana na huzuni, bila shaka utapata mawazo mengi sana​—mawazo fulani yanasaidia zaidi kuliko mengine. Pengine ni kwa sababu, kama vile tumeona, kila mutu iko na namna yake ya kuonyesha huzuni. Pengine mashauri yenye yanasaidia mutu mumoja hayawezi kusaidia mwengine.

Lakini, kuko mashauri ya musingi yenye watu wengi wameona kuwa ni yenye kufaa. Mashauri hayo yanatajwa mara nyingi na watu wenye kushauria wale wenye wamefiwa, na yanapatana na kanuni zenye kutumainika na zenye kupatikana mu Biblia, kitabu cha zamani chenye hekima.

1: KUBALI MUSAADA WENYE WATU WA FAMILIA NA MARAFIKI WANAKUTOLEA

  • Watu fulani wenye elimu wameona hilo kuwa jambo la maana lenye linasaidia kupambana na huzuni ya kufiwa. Hata hivyo, wakati fulani unaweza kupenda kuwa peke yako. Unaweza hata kukasirikia wale wenye wanajaribu kukusaidia. Hilo ni jambo la kawaida.

  • Usiwaze kama sikuzote unapaswa kuwa pembeni ya watu wengine, lakini pia usijitenge kabisa nao. Kwa kweli, unaweza kuwa na lazima ya musaada wao wakati wenye kuja. Kwa upole, uwaambie kile unapenda wakati huo na kile haupendi.

  • Kulingana na hali yako, uonyeshe usawaziko kati ya wakati wa kuwa pamoja na watu wengine na wakati wa kuwa peke yako.

KANUNI: “Wawili ni muzuri zaidi kuliko mumoja . . . Kwa maana kama mumoja wao anaanguka, ule mwingine anaweza kusimamisha mwenzake.”​—Muhubiri 4:9, 10.

2: UKUWE MUANGALIFU KUHUSU CHAKULA CHENYE UNATUMIA, NA UPANGE KUFANYA MAZOEZI

  • Chakula ya muzuri inaweza kusaidia kupambana na mahangaiko yenye kuletwa na huzuni. Ujaribu kula matunda mbalimbali, mboga za majani, na chakula chenye kuwa na proteine, lakini chenye hakina mafuta mengi.

  • Kunywa maji mengi na vinywaji vingine vyenye kuwa muzuri kwa afya.

  • Kama uko na hamu kidogo ya kula, kula sehemu kidogo-kidogo kila mara. Unaweza pia kuuliza munganga wako juu ya chakula kingine chenye kujenga mwili chenye unaweza kutumia. *

  • Kufanya mazoezi ya kutembea haraka na aina zingine za mazoezi ya mwili kunaweza kupunguza hisia zenye hazifae. Kufanya mazoezi kunaweza kupatia mutu nafasi ya kufikiri juu ya kifo cha mupendwa wake ao nafasi ya kusahau kwanza jambo hilo.

KANUNI: “Hakuna mutu mwenye anachukia mwili wake; lakini anaukulisha na kuutunza kwa upendo.”​—Waefeso 5:29.

3: ULALE SAA ZA KUENEA

  • Usingizi ni wa maana sikuzote, lakini zaidi sana kwa wale wenye kuwa na huzuni ya kufiwa, juu huzuni inaweza kufanya mutu achoke zaidi.

  • Ukuwe mwangalifu kuhusu kiasi cha kafeini na pombe yenye unatumia, juu vinaweza kuvuruga usingizi wako.

KANUNI: “Mukono mumoja wa pumuziko ni muzuri zaidi kuliko mikono mbili ya kazi ya nguvu na kufuatilia upepo.”​—Muhubiri 4:6.

4: UKUWE TAYARI KUBADILIKA

  • Ujue kama kila mutu iko na namna yake ya kuonyesha huzuni. Mwishowe, itakuomba kuamua ni njia gani ya muzuri zaidi yenye unaweza kutumia ili kupambana na huzuni.

  • Watu wengi wanaona kama kuambia wengine huzuni yao kunawasaidia kupambana nayo, lakini wengine wanaamua kuficha huzuni yao. Kuonyesha hisia kunaweza kusaidia mutu aweze kupambana na huzuni yake, lakini watu wenye elimu wako na mawazo tofauti juu ya jambo hilo. Ikiwa unapenda kuambia mutu mwengine namna unajisikia, lakini uko unasita kufanya vile, pengine inaweza kuwa mwepesi zaidi kwako ikiwa unaelezea rafiki yako wa karibu hisia zako fulani.

  • Watu fulani wanaona kama kulia kunawasaidia kupambana na huzuni yao, lakini inaonekana kuwa wengine wanapambana na huzuni yao hata kama wanalia kidogo tu.

KANUNI: “Moyo unajua uchungu wake mwenyewe.”​—Mezali 14:10.

5: EPUKA MAZOEA YENYE KUHARIBU AFYA

  • Watu fulani wenye wamefiwa wanajaribu kupunguza maumivu yao ya moyoni kwa kutumia mubaya pombe na dawa za kulewesha. Kujaribu kupunguza huzuni kwa njia hiyo kunaharibu afya. Kujituliza kwa njia hiyo ni kwa muda mufupi, na kunaweza kuleta tu matokeo makubwa ya mubaya. Jaribu kutumia njia zenye hazina hatari ili kupunguza mahangaiko yako.

KANUNI: “Tujisafishe kila uchafu.”​—2 Wakorinto 7:1.

6: TUMIA WAKATI WAKO KWA USAWAZIKO

  • Watu wengi wanaona kuwa ni jambo lenye kufaa kubadilisha vipindi vya kuonyesha huzuni (wakati wa kuonyesha na kupambana na hisia zao) na vipindi vya kubakia bila huzuni (wakati wa kufanya mambo yenye kuwasaidia wasahau kwanza maumivu yao).

  • Unaweza kupata kitulizo kwa muda fulani kwa kuanzisha urafiki ao kwa kukomalisha uhusiano na marafiki wako, kwa kujifunza ufundi mupya, ao kwa kutafuta wakati wa kujifurahisha.

  • Kadiri wakati unapita, bila shaka namna unatumia wakati itabadilika. Unaweza kutambua kuwa mara mingi zaidi unaanza kuwa na wakati murefu wa kubakia bila huzuni​—jambo lenye kwa kawaida ni hatua ya kupona kutokana na huzuni yako.

KANUNI: “Kila kitu kiko na wakati wake wenye uliwekwa, . . . wakati wa kulia na wakati wa kucheka; wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza.”​—Muhubiri 3:1, 4.

7: RUDILIA PROGRAMU YAKO YA KAWAIDA NA UIHESHIMIE

  • Kadiri inawezekana, rudilia bila kukawia maisha yako ya kawaida.

  • Kama unaheshimia programu yako ya kulala, ya kazi, na programu ya kufanya mambo mengine, bila shaka utafikia kufanya mambo kama zamani.

  • Kuendelea kuwa na mambo mengi ya muzuri ya kufanya kunaweza kukusaidia kupunguza maumivu ya moyoni.

KANUNI: “Itakuwa vigumu kwake kutambua kwamba siku za maisha yake zinapita haraka, kwa sababu Mungu wa kweli anamufanya aendelee kufurahi sana katika moyo wake.”​—Muhubiri 5:20.

8: EPUKA KUFANYA MAAMUZI MAKUBWA HARAKA-HARAKA

  • Watu wengi wenye wanafanya maamuzi makubwa kisha tu kufiwa na mupendwa wao wanafikia kuhuzunika juu ya maamuzi yao.

  • Kama inawezekana, chunga kipindi fulani cha wakati kipite mbele uhame, ubadilishe kazi, ao upatie watu wengine vitu vya mupendwa wako mwenye amekufa.

KANUNI: “Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio, lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.”​—Mezali 21:5.

9: KUMBUKA MUPENDWA WAKO MWENYE ALIKUFA

  • Watu wengi wenye wamefiwa wanaona kama ni muzuri kufanya mambo yenye yanaweza kuwasaidia wakumbuke mutu mwenye amekufa.

  • Pengine unaweza kupata kitulizo kwa kukusanya picha ao vitu vingine vyenye kusaidia kukumbuka, ao kuandika matukio ao mambo fulani yenye ungependa kukumbuka.

  • Uchunge vitu vyenye vinaweza kukukumbusha mambo ya muzuri, na kisha muda fulani wenye unapenda, uviangalie.

KANUNI: “Kumbuka siku za zamani.”​—Kumbukumbu la Torati 32:7.

10: UTOKE KIDOGO

  • Unaweza kupanga kuenda mapumuziko.

  • Ikiwa unaona kama haitawezekana kuenda mapumuziko kwa muda murefu, pengine unaweza kufanya jambo fulani lenye kufurahisha kwa siku moja ao mbili, kama vile kutembea kwa muda murefu, kutembelea nyumba ya makumbusho (ao, musée), ao kutembea na motokari.

  • Hata kufanya jambo fulani tofauti na mambo yenye unazoea kufanya, kunaweza kukusaidia upambane na huzuni yako.

KANUNI: “Mukuje ninyi wenyewe mahali kwenye hakuna watu ili mupumuzike kidogo.”​—Marko 6:31.

11: USAIDIE WENGINE

  • Kumbuka kama wakati wowote wenye unaweza kutumia ili kusaidia wengine, unaweza kukusaidia ujisikie muzuri zaidi.

  • Unaweza kuanza kwa kusaidia watu wenye wako pia na huzuni juu ya kifo cha mupendwa wako, kama vile marafiki ao watu wa jamaa yako wenye wanaweza kuwa na lazima ya mutu mwenye kuwa pia na huzuni ao mwenye kuelewa namna wanajisikia.

  • Kutegemeza na kutuliza watu wengine kunaweza kukufanya ukuwe tena na furaha na kufanya uone kama unaweza kutimiza tena jambo fulani la maana na kuwa ungali na kusudi katika maisha.

KANUNI: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

12: CHUNGUZA UPYA MAMBO YENYE UNATANGULIZA

  • Huzuni ya kufiwa inaweza kufanya mutu aelewe muzuri zaidi ni mambo gani yenye kuwa ya maana kabisa.

  • Tumia nafasi hiyo ili kuchunguza namna unatumia maisha yako.

  • Kama ni lazima, fanya mabadiliko kuhusu mambo yenye unatanguliza mu maisha yako.

KANUNI: “Ni muzuri zaidi kuenda katika nyumba ya maombolezo kuliko kuenda katika nyumba ya karamu, kwa sababu huo ndio mwisho wa kila mwanadamu, na wenye kuwa wazima wanapaswa kuweka jambo hilo katika moyo.”​—Muhubiri 7:2.

Ni kweli kwamba, hakuna kitu chenye kinaweza kumaliza kabisa maumivu yenye unasikia. Lakini, watu wengi wenye wamefiwa na mupendwa wao, wanaweza kushuhudia kuwa, kufuata hatua zenye kufaa, kama zile zenye tumezungumuzia katika habari hii, kuliwasaidia kupata kitulizo. Kwa kweli, liste hii haizungumuzie mambo yote yenye mutu anaweza kufanya ili kupunguza huzuni. Lakini, kama unajaribu kutumia mapendekezo fulani kati ya mapendekezo hayo, utaona kuwa yatakusaidia utulie kwa kiasi kikubwa.

^ fu. 13 Amuka! haipendekeze aina yoyote ya matunzo.