Ona video zinazopatikana

Mikaeli, Malaika Mukubwa, Ni Nani?

Mikaeli, Malaika Mukubwa, Ni Nani?

Jibu ya Biblia

 Bila shaka, Mikaeli mwenye dini fulani zinaitaka “Mutakatifu Mikaeli,” ni jina yenye Yesu alipewa mbele akuye ku dunia na kisha kurudia mbinguni. * Mikaeli alibishana na Shetani juu ya kifo ya Musa, na alisaidia malaika fulani juu afikishie Danieli ujumbe wa Mungu. (Danieli 10:13, 21; Yuda 9) Mikaeli maana yake “Ni Nani Mwenye Kuwa Kama Mungu? Na ile jina inamufaa sana juu anateteaka utawala wa Mungu na kupigana na maadui wake.​—Danieli 12:1; Ufunuo 12:7.

 Ona juu ya nini tunasema kama Yesu njo Mikaeli, malaika mukubwa.

  •   Mikaeli ni “malaika mukubwa.” (Yuda 9) Maneno “malaika mukubwa” inapatikana mu maandiko tu mbili ya Biblia. Na mu ile maandiko mbili ile maneno inatumiwa kwa umoja, ni kusema ni malaika mumoya tu njo anaitwa kwa ile jina ya cheo. Andiko moya kati ya ile maandiko inasema kama Bwana Yesu, mwenye kufufuliwa, “atashuka kutoka mbinguni na mwito wenye amri, pamoja na sauti ya malaika mukubwa.” (1 Watesalonike 4:16) Yesu iko na “sauti ya malaika mukubwa” juu yeye njo Mikaeli, malaika mukubwa.

  •   Mikaeli anaongoza jeshi ya malaika. “Mikaeli na malaika wake wakapigana na ule nyoka mukubwa,” Shetani. (Ufunuo 12:7) Mikaeli iko na mamlaka makubwa kule mbinguni. Njo maana anaitwa “mumoja kati ya wakubwa wa mbele” na “ule mukubwa.” (Danieli 10:13, 21; 12:1) David E. Aune, mwenye elimu ya Agano Jipya, anasema kama ile majina ya cheo inaonyesha kuwa Mikaeli njo “kiongozi wa malaika wote.”

     Biblia inaonyesha jina ingine ya malaika mwenye kuwa na mamlaka juu ya malaika wengine wote. Inasema kama “Bwana Yesu atafunuliwa kutoka mbinguni pamoja na malaika wake wenye nguvu, katika moto wenye kuwaka, wakati ataleta kisasi.” (2 Watesalonike 1:7, 8; Matayo 16:27) Yesu “alienda mbinguni, na malaika na mamlaka na nguvu vilitiishwa kwake.” (1 Petro 3:21, 22) Haiwezekane kukuwe Yesu na kukuwe Mikaeli kisha Mungu awafanye wote wawili kuwa viongozi wa malaika. Ile inaweza kutokeza ushindani mbinguni. Njo maana inatapatana na akili kusema kama majina Yesu na Mikaeli ni majina mutu mumoya tu.

  •   Mikaeli “atasimama” wakati wa “taabu” yenye haiyatokeaka. (Danieli 12:1) Mara mingi mu kitabu ya Danieli, neno “kusimama” inatumiwa juu ya kuzungumuzia mufalme mwenye anachukua hatua ili kufanya jambo fulani ya pekee. (Danieli 11:2-4, 21) Yesu Kristo, mwenye anaitwa “Neno la Mungu” na “Mufalme wa wafalme” atafanya jambo ya pekee wakati ataua maadui wa Mungu na kulinda watu wa Mungu. (Ufunuo 19:11-​16) Atafanya vile wakati wa “taabu kubwa yenye haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu.”​—Matayo 24:21, 42.

^ Mu Biblia muko watu wengine wenye wako na majina zaidi ya moya. Kwa mufano, Yakobo (anaitwa pia Israeli), Petro (anaitwa pia Simoni), na Tadayo (anaitwa pia Yuda).​—Mwanzo 49:1, 2; Matayo 10:2, 3; Marko 3:18; Matendo 1:13.