Ona video zinazopatikana

Biblia Inafundisha Kama Dunia Iko Tambarare?

Biblia Inafundisha Kama Dunia Iko Tambarare?

Jibu ya Biblia

 Hapana, Biblia haifundishe kama dunia iko tambarare. * Biblia haiko kitabu ya sayansi. Lakini, haipinge mambo yenye sayansi imehakikisha kama ni ya kweli. Mambo yenye Biblia inasema “yanategemeka sikuzote, sasa na milele.”​—Zaburi 111:8.

 Biblia inamaanisha nini wakati inasema “pembe ine (4) za dunia”?

 Biblia inatumia maneno “pembe ine (4) za dunia” na “miisho ya dunia.” Ile maneno haiko ya kukamata vile unaisikia, haimaanishe kama dunia iko na pembe ine zenye kuwa sawasawa ao iko na miisho. (Isaya 11:12; Yobu 37:3) Lakini, ile maneno ya mufano inaonyesha tu eneo yote ya dunia. Ni mu ileile njia njo Biblia inatumia maneno “kutoka mashariki na mangaribi, na kutoka kaskazini na kusini.”​—Luka 13:29.

 Inaonekana neno ya Kiebrania yenye inatafsiriwa “pembe” ao “miisho” ni neno ya mufano yenye inatokana na neno “mabawa.” Kulingana na kitabu The International Standard Bible Encyclopedia, “juu ndege anatumiaka mabawa ili kufunika vitoto vyake, [ile neno ya Kiebrania] inatumiwa juu ya kumaanisha mwisho wa kitu fulani kisha ile kitu kunyooshwa.” Ile kitabu inasema kama mu Yobu 37:3 na mu Isaya 11:12, “ile neno inamaanisha maeneo ya pembeni ya bahari, mipaka, ao miisho ya sehemu fulani ya dunia.” *

 Tuseme nini kuhusu namna Shetani alimujaribu Yesu?

 Ili kumujaribu Yesu, “Ibilisi akamupeleka kwenye mulima wenye kuwa na urefu wenye hauko wa kawaida na kumuonyesha falme zote za ulimwengu na utukufu wa falme hizo.” (Matayo 4:8) Watu fulani wanasema kama hii habari ya Biblia inafundisha kama kuko fasi kwenye mutu anaweza kusimama ku dunia na kuona fasi yote. Lakini, inaonekana kama “mulima wenye kuwa na urefu wenye hauko wa kawaida” wenye kuzungumuziwa mu hii habari ni maneno ya mufano tu na haiko fasi halisi. Ona juu ya nini tunasema vile.

  •   Hakuna mulima fulani ku dunia kwenye mutu anaweza kusimama na kuona falme zote za ulimwengu.

  •   Ibilisi hakumuonyesha tu Yesu falme zote za ulimwengu, lakini pia “utukufu wa falme hizo.” Ile mambo yote haingeweza kuonekana kwa mbali. Kwa hiyo, inaonekana Ibilisi alitumia aina fulani ya maono juu ya kumuonyesha Yesu ile mambo. Tunaweza kufananisha ile na wakati mutu fulani anatumia projecteur na écran ili kuonyesha mutu fulani picha za maeneo mbalimbali ya dunia.

  •   Habari yenye kufanana na ile yenye kupatikana mu Luka 4:5 inasema kama Shetani alionyesha Yesu “falme zote za dunia yenye kuikaliwa na watu,” jambo yenye macho ya wanadamu haingeweza kuona. Ile inaonyesha kama Shetani alimujaribu Yesu kwa kutumia njia ingine yenye haingeweza kuonekana na macho ya mwanadamu.

^ Biblia inasema kama Mungu ‘anakaa juu ya muviringo wa dunia.’ (Isaya 40:22) Vitabu fulani vinaonyesha kama neno yenye kutafsiriwa hapa kuwa “muviringo” inaweza kumaanisha duara ao muviringo, lakini watu wengi wenye elimu hawakubaliane na ile. Hata vile, Biblia haionyeshe kama dunia iko tambarare.

^ Toleo Yenye Kurekebishwa, Buku ya 2, ukurasa wa 4.