Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Ni ya Zamani Sana ao Ilisema Mambo Mbele ya Wakati?

Biblia Ni ya Zamani Sana ao Ilisema Mambo Mbele ya Wakati?

SAYANSI

BIBLIA HAIKO KITABU CHA SAYANSI, LAKINI INAZUNGUMUZIA MAMBO YENYE YALIKUJA KUJULIKANA KISHA MIAKA MINGI. TUCHUNGUZE MIFANO FULANI.

Ulimwengu ulikuwa na mwanzo?

Wakati fulani, wanasayansi wakubwa waliwaza kwa uhakika wote kuwa jibu ni hapana. Lakini, sasa wengi wanakubali kuwa ulimwengu ulikuwa na mwanzo. Biblia ilisema jambo hilo tangu zamani.​—Mwanzo 1:1.

Dunia iko na umbo gani?

Zamani, watu wengi walifikiri kuwa dunia ilikuwa tambarare (plat). Katika miaka ya 400 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wanasayansi Wagiriki walisema kuwa dunia ilikuwa muviringo. Lakini, zamani sana mbele ya hapo, ni kusema, katika miaka ya 700 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, muandikaji mumoja wa Biblia mwenye kuitwa Isaya alizungumuzia ‘muviringo wa dunia.’​—Isaya 40:22.

Mbingu zenye nyota zinaweza kuharibika?

Aristote, mwanasayansi Mugiriki mwenye aliishi katika miaka ya 300 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, alifundisha kuwa uharibifu unafanyika tu katika dunia, na kuwa mbingu zenye nyota hazitabadilika ao kuharibika hata kidogo. Wazo hilo lilikubaliwa kwa mamia ya miaka. Lakini katika miaka ya 1800, wanasayansi wengi walianza kuzungumuzia hali ya ulimwengu kuwa katika muvurugo. Walisema kuwa vitu vyote, ikuwe mbinguni ao duniani, vinaenda kwenye uharibifu. Lord Kelvin, mwanasayansi mumoja mwenye alisaidia kuendeleza wazo hilo, alionyesha kuwa Biblia inasema hivi juu ya mbingu na dunia: “Nazo zote zitachakaa kama vazi.” (Zaburi 102:25, 26) Kelvin aliamini, kama vile Biblia inafundisha, kwamba Mungu angeamua kuzuia hali hiyo ya kuharibika iharibu vitu vyenye Ameumba.​—Mhubiri 1:4.

Ni nini inakamata sayari kama vile dunia yenye tunaishi ndani?

Aristote alifundisha kuwa sayari zote zenye kuwa katika anga ziko moja ndani ya ingine na kuendelea. Kupitia sayari moja unaweza kuona zingine, na alionyesha kuwa dunia ilikuwa katikati. Katika miaka ya 1700 wakati wetu, wanasayansi walikuwa wanakubali wazo la kwamba inawezekana nyota na sayari havikamatwe na kitu. Lakini katika kitabu cha Ayubu, chenye kiliandikwa katika miaka ya 1400 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, tunasoma kuwa Muumbaji ‘anatundika dunia pasipo na kitu.’​—Ayubu 26:7.

MAMBO YA MATUNZO

HATA KAMA BIBLIA HAIKO KITABU CHA MAMBO YA MATUNZO, IKO NA KANUNI FULANI ZENYE KUONYESHA KAMA IMEZUNGUMUZIA MAMBO YENYE KUHUSU MATUNZO TANGU ZAMANI.

Kutenga wagonjwa.

Sheria ya Musa ilisema kuwa watu wenye kuwa na ugonjwa wa ukoma walipaswa kutenganishwa na watu wengine. Ni kisha tu magonjwa yenye yalitokea katika Enzi ya Kati (Moyen Ages) ndio wanganga walijifunza kutumikisha kanuni hiyo, yenye inaendelea kuleta matokeo ya muzuri.​—Mambo ya Walawi, sura ya 13 na 14.

Kunawa mikono kisha kugusa maiti.

Mupaka mwisho-mwisho mwa miaka ya 1800, wanganga walikuwa wanagusa maiti na kisha walitunza wagonjwa bila kunawa mikono yao. Watu wengi walikuwa wanakufa kwa sababu ya tabia hiyo. Lakini, Sheria ya Musa ilisema kuwa mutu yeyote mwenye aligusa maiti hakukuwa safi kulingana na desturi. Ilifikia hata kusema kuwa katika hali kama hizo, maji yalipaswa kutumiwa ili kujitakasa kulingana na sheria. Kwa kweli, tabia hizo za kidini zilikuwa na matokeo ya muzuri juu ya afya.​—Hesabu 19:11, 19.

Kujiepusha na uchafu.

Kila mwaka, watoto zaidi ya 500 000 wanakufa kwa sababu ya ugonjwa wa kuhara, wengi wao ni kwa sababu hawakuepushwa na mavi ya mwanadamu yenye yaliachwa ovyo-ovyo. Sheria ya Musa ilisema kuwa mavi ya mwanadamu yalipaswa kuzikwa, mbali na kwenye watu walikuwa wanaishi.​—Kumbukumbu la Torati 23:13.

Wakati wa kutahiriwa.

Sheria ya Mungu ilisema kuwa mutoto mwanaume alipaswa kutahiriwa siku ya munane kisha kuzaliwa kwake. (Mambo ya Walawi 12:3) Inasemewa kwamba damu ya watoto wenye wametoka kuzaliwa iko na uwezo wa kuganda na kufikia hali yake ya kawaida kisha juma la kwanza. Wakati wa zamani, mbele kukuwe maendeleo katika mambo ya matunzo, ilikuwa jambo la hekima kungojea zaidi ya juma moja mbele ya kutahiri mutoto.

Upatano wenye kuwa kati ya afya ya moyoni na afya ya kimwili.

Watu wenye kutafuta habari juu ya mambo ya matunzo na wanasayansi wanasema kwamba mambo kama vile kuwa na furaha, tumaini, kuonyesha shukrani, na kuwa tayari kusamehe, ni mambo yenye kuwa na faida juu ya afya ya kimwili. Biblia inasema hivi: ‘Moyo wenye shangwe [ao, furaha] ni dawa nzuri, lakini roho iliyopondeka inakausha mifupa.’​—Methali 17:22.