Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Juu ya Magonjwa Yenye Kuenea Sana?

Biblia Inasema Nini Juu ya Magonjwa Yenye Kuenea Sana?

Jibu la Biblia

 Biblia ilitabiri kama mu siku za mwisho kutakuwa magonjwa ya kuambukiza (magonjwa yenye kuenea sana). (Luka 21:11) Ile magonjwa yenye kuenea sana haiko malipizi yenye Mungu anapatia watu. Kwa kweli, hivi karibuni Mungu atatumia Ufalme wake ili kumaliza magonjwa yote, bila kusahau magonjwa yenye kuenea sana.

 Biblia ilisemaka kama kutakuwa magonjwa yenye kuenea sana?

 Biblia haikusema majina ya magonjwa yenye kuenea sana kama vile Coronavirus, UKIMWI, ao homa ya Hispania. Lakini, ilitabiri kama kutakuwa “magonjwa ya kuambukiza” na “pigo lenye kuua.” (Luka 21:11; Ufunuo 6:8) Ile mambo ni sehemu ya alama ya “siku za mwisho,” zenye zinaitwa pia “umalizio wa mupangilio wa mambo.”​—2 Timoteo 3:1; Matayo 24:3.

 Mungu alishakatumia magonjwa ili kupatia watu malipizi?

 Biblia inazungumuzia mifano kidogo tu yenye kuonyesha wakati wenye Mungu alitumia magonjwa ili kupatia watu malipizi. Kwa mufano, alifanya watu fulani wakuwe na ukoma. (Hesabu 12:1-16; 2 Wafalme 5:20- 27; 2 Nyakati 26:16-21) Ile magonjwa haikupata watu wengi sana na haikupata watu wenye hawana kosa. Lakini, ile mambo ilikuwa hukumu juu ya watu wenye walikuwa wamemuasi Mungu waziwazi.

 Magonjwa yenye kuenea sana leo ni malipizi kutoka kwa Mungu?

 Hapana. Watu fulani wanasema kama leo Mungu iko anatumia magonjwa yenye kuenea sana na magonjwa ingine ili kupatia watu malipizi. Lakini, Biblia haiunge mukono ile mawazo. Juu ya nini?

 Sababu moja ni kuwa, waabudu fulani wa Mungu, ikuwe wa zamani ao wa leo, wamepatwa na magonjwa. Kwa mufano, mwanaume muaminifu Timoteo, alikuwa na ‘ugonjwa wa mara kwa mara.’ (1 Timoteo 5:23) Lakini Biblia haiseme kama alikuwa na ule ugonjwa juu Mungu hakumukubali. Leo pia, kuko watumishi waaminifu wa Mungu wenye wanagonjwa ao kuambukizwa na magonjwa. Mara mingi wale watu wanapatwa na magonjwa juu walikuwa pa nafasi ya mubaya na kwa wakati wa mubaya.—Muhubiri 9:11.

 Tena, Biblia inafundisha kama wakati wenye Mungu atapatia watu malipizi haujafika. Lakini, tunaishi “siku ya wokovu,” ni kusema, wakati wenye Mungu iko anatolea watu wote mualiko wa kumukaribia ili wafikie kuokolewa. (2 Wakorinto 6:2) Mungu iko anatumia kazi ya kuhubiri yenye kufanywa mu dunia yote ili kutolea watu ule mualiko. Ile kazi iko na ujumbe wa muzuri, ni kusema, “habari njema ya Ufalme.”​—Matayo 24:14.

 Magonjwa yenye kuenea sana itaishaka?

 Ndiyo. Biblia ilitabiri kama hivi karibuni hakuna mutu mwenye atakuwa tena mugonjwa. Wakati Ufalme wake utatawala, Mungu atamaliza magonjwa yote. (Isaya 33:24; 35:5, 6) Atamaliza mateso, maumivu, na kifo. (Ufunuo 21:4) Na atafufua wale wenye wamekufa ili waishi ku dunia, mu hali zenye kukamilika. Pia, watakuwa na afya ya muzuri.​—Zaburi 37:29; Matendo 24:15.

 Maandiko ya Biblia yenye kuzungumuzia magonjwa

 Matayo 4:23: “[Yesu] akazunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya Ufalme na kuponyesha kila namna ya ugonjwa na kila namna ya uzaifu katikati ya watu.”

 Inamaanisha: Miujiza ya Yesu ni mifano tu kidogo yenye kuonyesha mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanyia wanadamu wote hivi karibuni.

 Luka 21:11: “Kutakuwa . . . magonjwa ya kuambukiza.”

 Inamaanisha: Magonjwa yenye kuenea sana ni sehemu ya alama ya siku za mwisho.

 Ufunuo 6:8: “Angalia! farasi wa rangi ya majivu, na ule mwenye kukaa juu yake alikuwa na jina Kifo. Na Kaburi lilikuwa linamufuata karibu-karibu. Na wakapewa mamlaka . . . ili kuua . . . kwa pigo lenye kuua.”

 Inamaanisha: Unabii kuhusu wapanda-farasi ine wenye kuzungumuziwa mu Ufunuo unaonyesha kama mu siku zetu kungekuwa magonjwa yenye kuenea sana.