Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA FAMILIA

Namna ya Kusaidia Watoto Wakati Wanashindwa Kufanya Jambo Fulani

Namna ya Kusaidia Watoto Wakati Wanashindwa Kufanya Jambo Fulani

Siku moja, mutoto wako atashindwaka kufanya jambo fulani. Namna gani unaweza kumusaidia ajisikie muzuri ikiwa ile hali inatokea?

 Mambo yenye unapaswa kujua

Kushindwa ni jambo la kawaida mu maisha. Biblia inasema kama “sisi wote tunajikwaa.” (Yakobo 3:2) Watoto pia wanajikwaa. Lakini, kushindwa kufanya jambo fulani kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri, kunaweza kusaidia mutoto akuwe na uwezo wa kupambana na hali ya nguvu. Watoto hawazaliwe na ule uwezo, lakini wanaweza kujifunza kuukomalisha. Mama mumoja mwenye kuitwa Laura anasema hivi: “Mimi na bwana yangu tumeona kama ni muzuri watoto wajue mambo ya kufanya wakati wanashindwa kufanya jambo fulani, kuliko kufanya kama vile hakukukuwa kitu. Wanaweza kujifunza namna ya kuvumilia wakati mambo haiendeke muzuri.”

Watoto wengi hawajue jambo la kufanya wakati wanashindwa kufanya jambo fulani. Watoto fulani hawakujifunza namna ya kupambana na hali ya kushindwa kwa sababu wazazi wao wanawafanya waone kama hawana kosa. Kwa mufano, kama mutoto hakutumika muzuri ku masomo, wazazi fulani wanasema mara moja kama ni kosa ya mwalimu. Kama mutoto hasikilizane na rafiki yake, mara moja wazazi wake wanasema kama rafiki yake njo iko na kosa.

Sasa, kama wazazi wanalinda watoto wao ili wasipate matokeo ya makosa yao, namna gani watoto wanaweza kujifunza kukubali makosa yao na kufanya jambo fulani ili kutengeneza mambo?

 Mambo yenye unaweza kufanya

  • Saidia watoto wako wajue kama matendo yao iko na matokeo.

    Biblia inasema hivi: “Kitu chochote chenye mutu anapanda, ni kile atavuna pia.”​—Wagalatia 6:7.

    Mambo yenye tunafanyaka inakuwaka na matokeo. Wakati tunaharibisha kitu fulani ni lazima tukitengeneze. Makosa yetu inaletaka matokeo ya mubaya. Watoto wanapaswa kujua kama kila jambo lenye mutu anafanya linakuwaka tu na matokeo; na wakati wanashindwa kufanya jambo fulani, ni muzuri wajue kama kwa njia fulani wao pia wako na kosa. Kwa hiyo, epuka kutetea mutoto wako ao kupatia wengine kosa wakati mutoto wako anashindwa kufanya jambo fulani. Lakini, kulingana na miaka yake, umuache ajionee matokeo ya mambo yenye alifanya. Kwa kweli, mutoto anapaswa kuwa na uwezo wa kuona kama ile yenye inamupata ni kwa sababu ya matendo yake.

  • Saidia watoto wako wajue jambo la kufanya wakati wanashindwa kufanya jambo fulani.

    Kanuni ya Biblia: “Mwenye haki anaweza kuanguka mara saba (7), na atasimama tena.”​—Mezali 24:16.

    Kushindwa kunaweza kutuletea huzuni, lakini haiko mwisho wa maisha. Saidia mutoto ajue jambo lenye anaweza kufanya ili siku ingine asishindwe; ni muzuri kufanya vile kuliko tu kunungunika kama alionewa. Kwa mufano, kama mutoto wako alishindwa mashindano ao examen ku masomo, umusadie aone namna anaweza kupambana na ile tatizo kwa kujifunza sana na kujikaza kutumika muzuri wakati wenye kuja. (Mezali 20:4) Kama mutoto wako mwanamuke alikosana na rafiki yake, umusaidie ajue namna ya kufanya amani na kutengeneza mambo, hata kama haikukuwa kabisa kosa lake.​—Waroma 12:18; 2 Timoteo 2:24.

  • Saidia watoto wako wajuwe kama wako na mipaka.

    Kanuni ya Biblia: “Ninaambia kila mutu pale kati yenu asijifikirie yeye mwenyewe sana kuliko vile inaomba kufikiri.”​—Waroma 12:3.

    Kuambia mutoto wako kama yeye njo anajua kufanya jambo fulani “muzuri zaidi” kupita wengine ni kumudanganya na ile haiwezi hata kumusaidia. Kusema kweli, hata mutoto mwenye anatumikaka muzuri ku masomo, haiko kila mara njo atakuwa anatoka wa kwanza. Na watoto wenye wanajua kucheza muchezo fulani muzuri zaidi, haiko kila siku njo watakuwa wanapata ushindi. Watoto wenye wanajua kama wako na mipaka, mara mingi wanajuaka mambo ya kufanya wakati wanashindwa na jambo fulani.

    Biblia inasema kama magumu inaweza kutusaidia tukomalishe sifa ya uvumilivu. (Yakobo 1:2-4) Kwa hiyo, hata kama kushindwa ni jambo lenye kuhuzunisha, unaweza kusaidia watoto wako wasivunjike moyo wakati ile hali inatokea.

    Kusaidia mutoto wako ajue namna ya kupambana na magumu ni jambo lenye linaomba wakati na bidii mingi; ni vile pia juu ya kumusaidia akomalishe uwezo mwingine. Lakini kama unajikaza kufanya vile, ile itamusaidia wakati ataingia mu kipindi cha ujana. Kitabu kimoja (Letting Go With Love and Confidence) kinasema hivi: “Ni nguvu vijana wenye kuwa na uwezo wa kupambana na magumu wafanye jambo fulani la upumbavu hata wakati wanalemewa na magumu. Inawezekana watapata matokeo ya muzuri wakati hali fulani ya mupya na yenye hawakutazamia inatokea.” Kwa kweli, kukuwa na uwezo wa kupambana na hali ngumu ni jambo lenye litawasaidia mupaka wakati watakuwa watu wazima.

Shauri: Uwekee watoto wako mufano. Kumbuka kama, namna wewe unapambana na magumu ya maisha itasaidia watoto wako wajue namna ya kupambana na magumu yao pia.