Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | KUKOMALISHA WATOTO

Watoto na Telefone​—Sehemu ya 1: Mutoto Yangu Anastahili Kuwa na Telefone?

Watoto na Telefone​—Sehemu ya 1: Mutoto Yangu Anastahili Kuwa na Telefone?

 Watoto wengi wanakomala na wako na telefone, a na wengi kati yao wanatumia telefone yao juu ya kuingia ku Enternete wakati wako wao peke ku chumba yao. Kuko hatari ya kuacha mutoto wako akuwe na telefone? Kuko faida gani? Unaachaka mutoto wako atumie telefone muda ngapi kwa siku?

 Mambo yenye unapaswa kujua

 Faida

  •   Ulinzi kwa watoto, amani ya akili kwa wazazi. Bethany, mama wa vijana wawili, anasema hivi: “Tunaishi mu dunia yenye kuwa hatari. Ni jambo ya maana kwa watoto kuzungumuza na wazazi wao kupitia telefone.”

     Mama mwenye kuitwa Catherine anaongezea hivi: “Kupitia applications fulani za telefone, unaweza kuunganisha telefone yako na ya mutoto wako juu ya kujua fasi kwenye iko. Ikiwa iko anatembeza gari unaweza kujua kama iko anaenda mbio ao hapana.”

  •   Inasaidia kufanya kazi ya ku masomo. Mama moya mwenye kuitwa Marie anasema hivi: “Walimu wanatumiaka watoto kazi fulani ya masomo kupitia e-maiI ao ujumbe fulani. Na ni mu ileile njia njo watoto wanazungumuzaka nao.”

 Hatari

  •   Kupitisha wakati mingi ku telefone. Kwa kawaida, vijana wengi wanapitishaka wakati mingi ku telefone kwa siku. Lakini, wazazi nao pia wanapitishaka wakati mingi na vyombo vyao vya kielektroniki kuliko kuzungumuza na watoto wao. Mushauri moya anasema kama, familia za mingi zinaweza kulinganishwa na “kikundi fulani ya watu wenye hawajuane wenye wako pamoya, na wenye kila mutu iko anakazia uangalifu telefone yake.” b

  •   Pornografia. Kulingana na kadirio fulani, vijana wengi wanaangaliaka kila mwezi pornografia na ile haishangaze juu Enternete inafanya ikuwe mwepesi kuangalia pornografia ku telefone. William, baba ya vijana wawili, anasema hivi: “Kwa kuruhusu watoto wao wakuwe na telefone, bila wao kujua, wazazi wanapatia watoto wao njia ya kupata pornografia ya kila aina na fasi yote.”

  •   Utumwa wa telefone. Watu wengi wanategemeaka sana telefone zao. Kama hawaone tena telefone zao, wengi wanasema kama wanasikiaka wasiwasi, hawajue mambo ya kufanya, na hata wanasikiaka sawa vile wanagonjwa. Wazazi fulani wanasema kama, wakati watoto wao wanatumia telefone zao, wanakosaka heshima. Carmen anasema hivi: “Wakati fulani saa yenye napendaka kuzungumuza na mutoto wangu mwanaume, anazungurushaka macho yake na kuniona mubaya ili kunionyesha kama niko namusumbua.”

  •   Hatari zingine. Kutumia telefone kunaletaka hatari ya kusumbuliwa ku Enternete na ya kutumiana ujumbe wenye unahusu ngono, na ile inaweza kuleta matatizo mbalimbali ya afya yenye inatokana na kuikala mubaya na kukosa kulala. Vijana fulani wanatumia application yenye inaitwa “ghost.” Ile application inaweza kuonekana sawa vile haiko ya mubaya. Iko sawa calculatrice, na inasaidia kufichika mambo fulani yenye watoto hawapendi wazazi wao waone.

     Daniel, baba ya kijana fulani mwanamuke, anamalizia kwa kusema hivi: “Telefone ni njia yenye inafungula mulango wa kupata mambo yote yenye kuwa ku Enternete, ikuwe ya muzuri ao ya mubaya.”

 Mambo yenye unapaswa kujiuliza

  •   ‘Mutoto Wangu Anastahili Kuwa na Telefone?’

     Biblia inasema hivi: “Mwerevu anafikiria sana kila hatua.” (Mezali 14:15) Ukiwa na ile mu akili, ujiulize hivi:

     ‘Ni jambo ya hekima kwa mutoto wangu kuwa na telefone juu ya ulinzi fulani ao juu ya sababu zingine? Nilifikiria kwa uangalifu faida na hatari? Kuko kitu ingine naweza kupatia mutoto wangu kuliko telefone?’

     Baba moya mwenye kuitwa Todd anasema hivi: “Inawezekana kuuzia mutoto telefone yenye haina Enternete ndani na ile inaweza kukupatia nafasi ya kuita mutoto na hata kumuandikia ujumbe fulani. Zile telefone zenye hazina Enternete zinakuwaka bei chini.”

  •   ‘Mutoto Wangu Amekomala Kabisa?’

     Biblia inasema hivi: “Moyo wa mwenye hekima unamuongoza katika njia yenye inafaa.” (Muhubiri 10:2) Ukiwa na ile mu akili, ujiulize hivi:

     ‘Nini njo inanihakikishia kama mutoto wangu ni mwenye kutumainika? Anaongeaka na miye waziwazi? Wakati fulani, anakuwaka na muelekeo wa kutosema kweli, kwa mufano kwa kunificha marafiki wake? Je, tayari alishaonyesha kama anajua namna ya kujizuia wakati wa kutumikisha vyombo vingine vya kielektroniki, kutia ndani televizyo, tablette, ao ordinatere?’ Mama moya mwenye kuitwa Serena anasema hivi: “Telefone ni ya lazima sana, lakini inaweza pia kuwa hatari sana. Sasa fikiria muzigo wenye unaweza kupatia mutoto wako na hayakuwa hata na uzoefu!”

  •   Niko Tayari Kutimiza Daraka Yangu?’

     Biblia inasema hivi: “Zoeza mutoto katika njia yenye anapaswa kufuata.” (Mezali 22:6, maelezo ya chini) Ukiwa na ile mu akili, ujiulize hivi:

     ‘Najua muzuri telefone ili kusaidia mutoto wangu aelewe hatari fulani na namna anaweza kuiepuka? Je, najua namna ya kuwekea mutoto wangu vizuizi mu telefone yake? Namna gani naweza kusaidia mutoto wangu ajue namna ya muzuri ya kutumia telefone?’ Daniel, mwenye tulishataya, anasema hivi: “Wazazi wengi wanapatiaka watoto wao telefone bila kujua hata kama wako wanaitumikisha namna gani.”

 Wazo kubwa: Watoto wako na lazima ya kuzoezwa ili kujua namna ya kutumikisha muzuri telefone. Kitabu moya inasema hivi: “Ni nguvu sana kwa watoto wengi kuepuka jaribu ya kupitisha wakati mingi ku telefone zao, zaidi sana kama wazazi hawajue mambo yenye wanafanyaka ao hawana muongozo wowote kutoka kwa wazazi wao. ” (Indistractable)

a Mu hii habari neno “telefone” ni telefone yenye iko na Enternete.

b Inapatikana mu kitabu Disconnected, ya Thomas Kersting.