Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | KUKOMALISHA WATOTO

Watoto na Telefone​—Sehemu ya 2: Fundisha Watoto Namna Wanaweza Kutumia Telefone kwa Hekima

Watoto na Telefone​—Sehemu ya 2: Fundisha Watoto Namna Wanaweza Kutumia Telefone kwa Hekima

 Telefone iko sawa vile chombo yenye uwezo. Inaweza kusaidia ao kuwa na hatari fulani, inategemea namna inatumiwa. Namna gani unaweza kufundisha watoto wako wajue namna ya kutumia muzuri telefone? Kwa mufano, kwa siku unawaza unaweza kuruhusu watoto wako watumie telefone kwa saa ngapi? a

 Mambo yenye unapaswa kujua

  •   Telefone inaweza kufanya mwenye kuitumia akuwe mu hatari. Habari yenye ilitangulia ilikuwa na kichwa “Watoto na Telefone​—Sehemu ya 1: Mutoto Wangu Anastahili Kuwa na Telefone?” Ile habari ilionyesha kama, telefone inaweza kutufungulia mulango ku kila kitu yenye kuwa ku Enternete, ikuwe ya muzuri ao ya mubaya.

     “Ni mwepesi kwetu kusahau kama telefone inaweza kufanya watoto wetu waangukie mu mikono ya watu wabaya na mu hatari ya mawazo ya mubaya.”​—Brenda.

  •   Watoto wako na lazima ya muongozo. Vijana wamezaliwa mu dunia yenye inayala teknolojia, na wanajua namna ya kuitumia. Lakini watu wazima wengi hawajue tu sana namna ya kutumia teknolojia. Lakini ile haionyeshe kama wazazi hawajue kitu juu ya teknolojia, na kama watoto njo wanastahili kabisa kujua namna na wakati wa kutumia telefone.

     Kusema kweli, watoto wanaweza kujua namna ya kutumia telefone. Lakini, ujue kama kuko tofauti kati ya uwezo na ukomavu. Hata kama watoto wanajua mambo mingi sana juu ya teknolojia, wako tu na lazima ya wazazi wao ili wawafundishe namna ya kutumia telefone kwa hekima.

     “Kupatia mutoto wako telefone bila kumuonyesha namna ya kuitumia, iko sawa vile kumupatia funguo za motokari, kumuambia aikale ndani ya motokari, awakishe motere ya ile motokari na kisha unamuambia: ‘Ukuwe muangalifu!’ Bila hata kumufundisha namna wanatembezaka motokari.”—Seth.

 Mambo yenye unaweza kufanya

  •   Ujifunze namna telefone ya mutoto wako inatumikaka. Ujikaze kujua muzuri mambo yenye kuwa mu telefone ya mutoto wako yenye inaweza kumusaidia aitumie kwa hekima. Kwa mufano:

     Ni paramètres gani za telefone ya mutoto zenye zinaweza kusaidia wazazi kutilia watoto wao mipaka juu ya wakati wa kutumia telefone, na pia aina ya site za Enternete zenye wanaweza kufungula?

     Unajuaka paramètres za telefone ya mutoto wako zenye zinasaidia kuzuia asione mambo yenye haiko ya muzuri?

     Kama unajua muzuri telefone ya mutoto wako, utajua namna ya muzuri ya kumusaidia ili aitumie kwa hekima.

     Kanuni ya Biblia: “Kwa ujuzi mutu anaongeza nguvu zake.”​—Mezali 24:5.

  •   Utie mipaka. Uamue mambo yenye utamuruhusu mutoto wako afanye na mambo yenye hautamuruhusu afanye. Kwa mufano:

     Utaruhusu mutoto wako atumie telefone wakati wa kula, ao aitumie wakati munaenda kutembelea watu wa familia ao marafiki?

     Mutoto wako anapaswa kuwa na telefone yake usiku mu chumba ya kulalia?

     Ni application gani zenye utaruhusu atumie?

     Utamuruhusu mutoto wako akuwe natumia telefone kwa muda wa saa ngapi?

     Utamuwekea wakati wa kutumia telefone kila siku?

     Inaomba mutoto wako ajue waziwazi sheria zenye umemuwekea. Na kama hazifuate, umupatie nizamu yenye kufaa.

     Kanuni ya Biblia: “Usiime kijana nizamu.”​—Mezali 23:13, maelezo ya chini.

  •   Chunguza telefone ya mutoto wako. Ujue neno ya siri (ao mot de passe) ya mutoto wako, na uchunguze mambo yenye kuwa mu telefone yake. Kutia ndani, ujumbe, application, picha na site za Enternete zenye alifungula.

     “Tuliambia mutoto wetu mwanamuke kama tutakuwa tunachunguza telefone yake, bila hata kumuambia mbele ya wakati kama tutafanya vile. Kama tunaona kuwa hakutumia muzuri telefone yake, tutamuwekea mipaka kuhusu namna ya kuitumia.”—Lorraine.

     Juu uko muzazi, uko na haki ya kujua namna mutoto wako anatumia telefone yake.

     Kanuni ya Biblia: “Mutoto anajulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na yenye kufaa.”​—Mezali 20:11.

  •   Fundisha kanuni. Umusaidie mutoto wako apende kufanya mambo yenye kufaa. Juu kama kweli mutoto anapenda kufichika wazazi wake jambo fulani, atapata tu njia ya kuifanya hata wazazi wake wafanye nini. b

     Kwa hiyo, umufundishe mutoto wako akuwe na sifa za muzuri sawa vile, unyoofu, kujizuia, na akuwe mwenye kuchukua mambo kwa uzito. Mutoto mwenye iko na sifa za muzuri anaweza kutumia telefone kwa hekima.

     Kanuni ya Biblia: ‘Watu wakomavu . . . wamezoeza nguvu zao za utambuzi ili kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.’​—Waebrania 5:14.

a Mu hii habari neno “telefone” ni telefone yenye iko na Enternete. Ile telefone inakuwaka sawa ordinatere ya kidogo.

b Kwa mufano, vijana fulani wanatumia application yenye inaitwa “ghost.” Ile application inaweza kuonekana sawa vile haiko ya mubaya. Iko sawa calculatrice, na inasaidia kufichika mambo fulani yenye watoto hawapendi wazazi wao waone.