Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | KUKOMALISHA WATOTO

Wakati Kijana Wako Anafanya Jambo Fulani Yenye Inafanya Usimutumainie Tena

Wakati Kijana Wako Anafanya Jambo Fulani Yenye Inafanya Usimutumainie Tena

 Vijana fulani hawaheshimie saa ya kurudia ku nyumba. Wengine wanadanganya wazazi wao pengine kwa kuwaambia uongo, ao kwa kutoka ku nyumba kwa uficho ili kuenda kuangalia marafiki wao. Unaweza kufanya nini kama kijana wako anafanya jambo fulani yenye inafanya usimutumainie tena?

 Kijana wangu ni muasi?

 Haiko vile kabisa. Biblia inasema hivi: “Upumbavu umefungwa katika moyo wa kijana,” na mara mingi vijana wanaonyeshaka kama ile maneno ni ya kweli. (Mezali 22:15, maelezo ya chini). Laurence Steinberg, profesere wa saikolojia, anasema hivi: “Vijana wanakamataka maamuzi fulani ya haraka-haraka na ya upumbavu. Utazamie kama watafanya tu makosa.”

 Nifanye nini kama kijana wangu amenidanganya?

 Usiseme mara moya kama kijana wako hapendi tu kukutii. Utafiti unaonyesha kama vijana wanahangaikiaka kabisa mambo yenye wazazi wao wanawaza kuwahusu, hata kama inaweza kuonekana kuwa hawahangaike. Pengine kijana wako haonyeshe vile, lakini inawezekana anahuzunikia mambo yenye alifanya, na anahangaika kuona vile amekuvunja moyo. a

Mufupa wenye kuvunjika, wakati unapona, unaweza kuwa na nguvu. Vilevile, inawezekana kuanza tena kutumainia mutu mwenye alituvunja moyo

 Kosa ni ya nani?

  •    Ni marafiki wake? Biblia inasema hivi: “Mashirika ya mubaya yanaharibu tabia za muzuri.” (1 Wakorinto 15:33) Kwa Kweli, marafiki wanaweza kubadilisha tabia za vijana. Ni vile pia kuhusu site za Enternete za kupashana habari na za kufanya matangazo ya biashara. Zaidi ya ile, vijana hawana uzoefu wa maisha, na unaweza kuona juu ya nini vijana wanakamataka maamuzi ya mubaya. Kwa kweli, vijana wanapaswa kujifunza kukubali matokeo ya maamuzi yao, na ile itawasaidia wafikie kuwa watu wazima wenye kutumainika.

  •    Nimefanya nini? Unaweza kuwazia kama kijana wako alijiendesha mubaya juu pengine ulikuwa mukali sana. Ao wakati fulani unaweza kuwaza kama ni juu uliachilia mambo na kupatia kijana wako uhuru mwingi sana. Kuliko kufikiria mambo yenye pengine haukufanya muzuri, fikiria mambo yenye unaweza kufanya juu ya kumusaidia.

 Ninaweza kusaidia kijana wangu namna gani juu nianze tena kumutumainia?

  •   Zuia matendo yako. Pengine kijana wako anatazamia kama utakasirika. Juu ya nini usitende mu njia ingine? Uulize kijana wake kwa utulivu juu ya nini alifanya mambo ya vile. Alifanya vile juu ya kupenda kujua? Ilikuwa juu alikuwa amechoka? Ilikuwa juu alijisikia kuwa yeye peke? Ao juu marafiki walimuvunja moyo? Ile mambo yote haiko sababu ya yeye kufanya vile, lakini inaweza kukusaidia, wenye na kijana wako, kuelewa nini njo ilimusukuma kutenda vile.

     Kanuni ya Biblia: ‘Ukuwe mwepesi wa kusikiliza, hapana mwepesi wa kusema, hapana mwepesi wa kukasirika.’​—Yakobo 1:19.

  •   Saidia kijana wako afikirie mambo yenye ilitokea. Umuulize maulizo sawa vile, umejifunza nini mu hii mambo yenye ilitokea? Siku ingine utafanya nini kama hii hali inatokea tena? Maulizo ya vile inaweza kusaidia kijana wako afikiri ili ajue namna ya kukamata maamuzi ya muzuri zaidi.

     Kanuni ya Biblia: “Karipia, kemea, chochea, kwa uvumilivu wote na ufundi wa kufundisha.”​—2 Timoteo 4:2.

  •   Usaidie kijana wako aelewe kama matendo yake iko na matokeo. Malipizi yeye itamusaidia sana kijana wako ni ile yenye inahusiana na kosa yenye alifanya. Kwa mufano, kama kijana wako alifanya usimutumainie kwa kutumia gari bila ruhusa yako, unaweza kumukataza kutembeza gari kwa wakati fulani.

     Kanuni ya Biblia: “Kitu chochote chenye mutu anapanda, ni kile atavuna pia.”​—Wagalatia 6:7.

  •   Ukaze akili ju ya mambo yenye unaweza kufanya juu uanze tena kumutumainia. Kusema kweli, itaomba wakati. Lakini, kijana wako anapaswa kujua kama kisha wakati fulani, unaweza kuanza kumutumainia tena. Umusaidie aelewe kama unaweza kuanza kumutumainia tena. Kama anaona kuwa hauwezi tena kumutumainia, anaweza kuvunjika moyo.

     Kanuni ya Biblia: “Musikuwe munakasirisha watoto wenu, ili wasivunjike moyo.”​—Wakolosai 3:21.

a Inatoka mu kitabu You and Your Adolescent.