Hamia kwenye habari

Maandishi Chini ya Mashine ya Kufua Nguo

Maandishi Chini ya Mashine ya Kufua Nguo

Baada ya kubatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova, Zarina alirudi kwenye nchi ya nyumbani kwao Asia ya Kati kutoka Urusi, na alikuwa ameazimia kuwalea watoto wake wawili katika imani. Kwa kuwa hakuwa na pesa nyingi, aliishi katika nyumba yenye chumba kimoja pamoja na wazazi wake na ndugu yake na mke wake. Wazazi wake walimwamuru asiwafundishe watoto wake kweli za Biblia. Pia waliwaambia binti zake wasizungumze na mama yao kuhusu Biblia.

Zarina alifikiria kwa uzito jinsi ya kuwasaidia binti zake kujifunza kumhusu Yehova. (Methali 1:8) Pia alisali kwake kwa bidii, akimwomba mwongozo na hekima. Kisha Zarina alitenda kupatana na sala zake kwa kwenda matembezi pamoja na binti zake huku akizungumza nao kuhusu maajabu ya uumbaji. Matembezi hayo mafupi yaliwasaidia binti zake kusitawisha upendezi katika Muumba.

Kisha, Zarina akabuni mbinu nyingine ya kuwafundisha binti zake kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? a Aliandika kwenye karatasi mafungu na maswali ya kitabu hicho. Pia alitia ndani sentensi chache za ziada za kuwasaidia binti zake kuelewa zaidi habari hiyo. Kisha alificha karatasi pamoja na penseli, chini ya mashine ya kuosha nguo iliyokuwa bafuni. Binti zake walipoingia humo walisoma mafungu na kuandika majibu yao.

Zarina alifaulu kujifunza sura mbili za kitabu Biblia Inafundisha pamoja na binti zake kwa kutumia mbinu hiyo kabla ya kupata mahali ambapo wangeishi wakiwa watatu. Akiwa katika nyumba mpya alikuwa huru kuwalea binti zake bila usumbufu. Mnamo Oktoba 2016, binti wote wawili walibatizwa, na walifurahi sana kwamba mama yao alitumia hekima na busara ili kuwalisha kiroho.

a Watu wengi sasa wanatumia kitabu Biblia Inatufundisha Nini?