Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hati ya Kigeorgia ya karne ya 14 yenye vitabu Vinne vya Injili vya Mokvi

GEORGIA | 1924-1990

Biblia ya Kigeorgia

Biblia ya Kigeorgia

KIGEORGIA ni moja kati ya lugha za mapema zaidi kuwa na tafsiri ya Biblia, sambamba na Kiarmenia, Kikoptiki, Kilatini, Kisiria, pamoja na lugha nyingine. Hati za kale za vitabu vya Injili vya Kigeorgia, barua za Paulo, pamoja na Zaburi, ziliandikwa katika miaka ya 450 W.K. au hata mapema zaidi. Katika karne zilizofuata, kazi ya kutafsiri na kunakili Biblia katika Kigeorgia iliongezeka, na hivyo kukawa na tafsiri mbalimbali. *

Mawazo ya Biblia yalitumiwa katika kazi za fasihi na yalichangia sana kujenga viwango vya maadili vya watu wa Georgia. Kwa mfano, hadithi ya kusikitisha ya Malkia Shushanik, ambayo huenda iliandikwa mwishoni mwa karne ya tano, ina maneno kutoka kwenye mistari kadhaa ya Biblia. Katika shairi lake refu linaloitwa Vepkhvistqaosani (Shujaa Aliyevaa Ngozi ya Chui), lililoandikwa miaka ya 1220, Shota Rustaveli alirejelea viwango vya maadili vya Kikristo. Aliandika kuhusu urafiki, ukarimu, na upendo kwa watu tusiowajua. Viwango hivyo bado vinachukuliwa kwa uzito na watu wa Georgia.

^ fu. 3 Ili kupata habari zaidi, soma makala yenye kichwa “Maandishi ya Kale Yenye Thamani,” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1, 2013.