Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

INDONESIA

Hatutakana Imani Yetu

Daniel Lokollo

Hatutakana Imani Yetu
  • ALIZALIWA 1965

  • ALIBATIZWA 1986

  • HISTORIA FUPI Painia wa pekee aliyesimama imara wakati wa mnyanyaso.

MNAMO Aprili 14, 1989, Nilikuwa naongoza mkutano katika mji wa Maumere, katika Kisiwa cha Flores, maofisa wa serikali walipoingia kwa nguvu na kunikamata pamoja na ndugu wengine watatu.

Walinzi wa gereza walitulazimisha kusalimu bendera. Tulipokataa, walituchapa, kutupiga mateke na kutuweka kwenye jua kali kwa siku tano. Usiku tulitetemeka kwa sababu ya kulala kwenye sakafu baridi na chafu ya seli ndogo, tukiwa tumechoka na kuhisi maumivu makali ya majeraha. Mara kwa mara mlinzi wa gereza alisisitiza kwamba tukane imani yetu, lakini tulijibu, “Hata ikiwa tutakufa, hatutasalimu bendera.” Kama Wakristo wengine waliotutangulia, tuliona ni pendeleo “kuteseka kwa ajili ya uadilifu.”—1 Pet. 3:14