Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

CreativeDesignArt/DigitalVision Vectors via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Je, Usawa wa Kijamii Ni Ndoto Tu?​—Biblia Inasema Nini?

Je, Usawa wa Kijamii Ni Ndoto Tu?​—Biblia Inasema Nini?

 Watu wengi wanatamani kuwe na usawa wa kijamii lakini ndoto hiyo haijatimia.

  •   “Ubaguzi wa rangi unaendelea kuwa kama sumu inayoathiri taasisi, jamii, na maisha ya kila siku katika maeneo yote. Ubaguzi wa rangi unaendelea kuwafanya watu watendeane kwa ukosefu wa haki.”​—António Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

 Je, kutawahi kuwa na usawa wa kijamii? Biblia inasema nini?

Maoni ya Mungu kuhusu usawa wa kijamii

 Biblia inafundisha maoni ya Mungu kuelekea watu wa rangi mbalimbali.

  •   “[Mungu] alifanyiza kila taifa la watu kutoka kwa mtu mmoja ili wakae juu ya uso wa dunia nzima.”​—Matendo 17:26.

  •   “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mtu anayemwogopa na kutenda uadilifu anakubaliwa naye.”​—Matendo 10:34, 35.

 Biblia inaonyesha kwamba wanadamu wote ni wa familia moja na kwamba Mungu anawakubali watu wa kila jamii.

Usawa wa kijamii utapatikanaje?

 Usawa wa kijamii utaletwa na Ufalme wa Mungu, serikali iliyo mbinguni. Serikali hiyo itawafundisha watu jinsi ya kutendeana kwa njia inayofaa. Watu watajifunza jinsi ya kushinda hisia zozote za ubaguzi ambazo huenda wakawa nazo.

  •   “Wakaaji wa nchi [watajifunza] kuhusu uadilifu.”​—Isaya 26:9.

  •   “Matokeo ya uadilifu wa kweli yatakuwa amani, na mazao ya uadilifu wa kweli yatakuwa utulivu wa kudumu na usalama wa kudumu.”​—Isaya 32:17.

 Leo, mamilioni ya watu wanajifunza kutoka katika Biblia jinsi ya kuwatendea wengine kwa heshima.