Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Nufaika Kutokana na Dhabihu ya Yesu

Nufaika Kutokana na Dhabihu ya Yesu

 Mara moja kila mwaka, Mashahidi wa Yehova hukusanyika ulimwenguni pote pamoja na mamilioni ya watu walioalikwa ili kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu, kama alivyoamuru. (Luka 22:19) Tukio hilo hutusaidia kuthamini umuhimu wa kile ambacho Yesu alifanya alipotoa uhai wake kwa ajili ya wanadamu. Pia, linatuonyesha jinsi dhabihu yake inavyoweza kutunufaisha—sasa na wakati ujao.​—Yohana 3:16.

 Iwe utahudhuria Ukumbusho mwaka huu au la, unaweza kunufaikaje kutokana na kifo cha Yesu cha kidhabihu? Yesu alitufundisha kwamba tunapaswa kufanya mambo mawili muhimu:

  1.  1. Jifunze kumhusu Mungu na Yesu. Yesu alisema hivi aliposali kwa Baba yake wa mbinguni: “Uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”​—Yohana 17:3.

  2.  2. Tenda kupatana na mambo unayojifunza. Yesu alikazia kwamba tunahitaji kutumia mafundisho yake maishani mwetu. Kwa mfano, alimalizia Mahubiri yake ya Mlimani ambayo ni maarufu sana kwa kumpongeza mtu yeyote ‘anayesikia maneno yake na kisha kuyatenda.’ (Luka 6:46-48) Vivyo hivyo, pindi nyingine alisema hivi: “Ikiwa mnajua mambo haya, mtakuwa wenye furaha mkiyatenda.”​—Yohana 13:17.

 Je, ungependa kujifunza mengi zaidi kumhusu Mungu na Yesu? Je, ungependa kupokea ushauri unaofaa wa jinsi ya kutenda kupatana na mambo unayojifunza? Zifuatazo ni baadhi ya njia unazoweza kupata habari itakayokusaidia.

Mtaala wa Biblia

 Mtaala wetu wa kujifunza Biblia bila malipo umewasaidia watu wengi kuichunguza Biblia na kuitumia maishani mwao.

  •   Tembelea ukurasa wa Jifunze Biblia Ukiongozwa na Mwalimu ili ujifunze mengi zaidi kuhusu programu hiyo.

  •   Tazama video yenye kichwa Karibu Kwenye Funzo Lako la Biblia ili uone jinsi kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kunavyofanywa.

Mikutano ya Mashahidi wa Yehova

 Mashahidi wa Yehova hukutana mara mbili kwa juma katika jengo lao la ibada linaloitwa Jumba la Ufalme. Katika mikutano hiyo, sisi huzungumza kuihusu Biblia na jinsi tunavyoweza kutumia mafundisho yake maishani mwetu.

 Watu wote wanaweza kuhudhuria mikutano hiyo; si lazima uwe Shahidi ili uhudhurie. Kwa kutegemea hali za kwenu, unaweza kuhudhuria uso kwa uso au kupitia video iliyounganishwa kwenye mtandao.

  •   Tazama video yenye kichwa Ni Nini Hutendeka Katika Jumba la Ufalme? ili ujionee kile ambacho unaweza kutazamia katika mikutano hiyo.

Makala na video mtandaoni

 Makala nyingi na video katika tovuti hii zinaweza kukusaidia kujifunza mengi zaidi kuhusu mafundisho ya Yesu na thamani ya dhabihu yake ya fidia.

 Kwa mfano, ili ujifunze jinsi inavyowezekana kwa kifo cha mtu mmoja kuwanufaisha mamilioni ya watu, soma makala zenye kichwa “Yesu Huokoa—Jinsi Gani?” na “Kwa Nini Yesu Aliteseka na Kufa?” au utazame video yenye kichwa Kwa Nini Yesu Alikufa?