Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Ninataka Talaka!”

“Ninataka Talaka!”

Nyumba imechakaa kwa sababu ya kutotunzwa. Kwa miaka mingi imepigwa na dhoruba nyingi, na nyingine ziliidhoofisha. Sasa nyumba hiyo ni dhaifu, na inaonekana itaporomoka wakati wowote.

MFANO huo unaonyesha hali ya ndoa nyingi leo. Je, umewahi kuhisi kwamba ndoa yako inaelekea kuporomoka? Ikiwa ndivyo, uwe na hakika kwamba hakuna ndoa isiyokuwa na matatizo. Kwa kweli, Biblia inaeleza waziwazi kwamba wale wanaofunga ndoa yaelekea watapata “uchungu na huzuni.”—1 Wakorintho 7:28, The New English Bible.

Wakikazia ukweli wa maneno hayo, kikundi kimoja cha watafiti kinasema kwamba ndoa ndio “mradi hatari zaidi ambao watu wengi katika jamii yetu hujiingiza kwa ukawaida.” Kinaongezea hivi: “Uhusiano ambao huanza kwa shangwe na matumaini mengi unaweza kugeuka na kusababisha mfadhaiko na maumivu mengi maishani.”

Namna gani ndoa yako? Je, ina mojawapo ya matatizo haya?

  • Ugomvi wa kila mara
  • Maneno yenye kuumiza
  • Ukosefu wa uaminifu
  • Chuki

Ikiwa ndoa yako ni dhaifu na inaonekana kwamba itaporomoka wakati wowote, unapaswa kufanya nini? Je, talaka ndiyo suluhisho?