Kwa Wagalatia 2:1-21

  • Paulo akutana na mitume huko Yerusalemu (1-10)

  • Paulo amrekebisha Petro (Kefa) (11-14)

  • Kutangazwa kuwa waadilifu kupitia imani tu (15-21)

2  Baada ya miaka 14 nilipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba,+ na Tito pia.+  Lakini nilienda kutokana na ufunuo, nami nikawajulisha habari njema ambayo ninahubiri kati ya mataifa. Hata hivyo, nilifanya hivyo faraghani, mbele ya wanaume walioheshimiwa sana, ili kuhakikisha kwamba sikuwa ninakimbia bure au sikuwa nimekimbia bure.  Hata hivyo, hata Tito,+ aliyekuwa pamoja nami, hakulazimishwa kutahiriwa,+ ingawa alikuwa Mgiriki.  Lakini jambo hilo lilitokea kwa sababu ya akina ndugu wa uwongo walioingizwa kimyakimya,+ walioingia kisirisiri ili kupeleleza uhuru+ tunaofurahia katika muungano na Kristo Yesu, ili watufanye kuwa watumwa kabisa;+  hatukukubaliana nao wala kujitiisha kwao,+ hapana, hata kwa muda mfupi,* ili kweli ya habari njema iendelee kuwa pamoja nanyi.  Lakini kuhusu wale walioonekana kuwa muhimu+—vyovyote walivyokuwa hapo awali sioni tofauti, kwa maana Mungu haangalii sura ya nje—watu hao walioheshimiwa sana hawakuniongezea kitu chochote kipya.  Badala yake, walipoona kwamba nilikuwa nimekabidhiwa habari njema kwa ajili ya wale wasiotahiriwa,+ kama vile Petro alivyokabidhiwa kwa ajili ya wale waliotahiriwa⁠—  kwa maana yule aliyemtia Petro nguvu kwa ajili ya utume kwa wale waliotahiriwa, alinitia nguvu mimi pia kwa ajili ya watu wa mataifa+  nao walipotambua fadhili zisizostahiliwa nilizopewa,+ Yakobo+ na Kefa* na Yohana, ambao walionekana kuwa nguzo, walinipa mimi na Barnaba+ mkono wa kulia wa kushirikiana,* ili sisi twende kwa mataifa, nao waende kwa watu waliotahiriwa. 10  Walituomba tuwakumbuke maskini, nami nimejitahidi sana kufanya jambo hilo.+ 11  Hata hivyo, Kefa*+ alipokuja Antiokia,+ nilimpinga* uso kwa uso, kwa sababu kwa hakika alikuwa amekosea.* 12  Kwa maana kabla ya watu fulani kutoka kwa Yakobo+ kufika, alikuwa akila chakula pamoja na watu wa mataifa;+ lakini walipofika, akaacha kufanya hivyo, akajitenga kwa kuwaogopa wale waliotahiriwa.+ 13  Wayahudi wengine pia wakajiunga naye katika unafiki huo, hivi kwamba hata wakamshawishi Barnaba katika unafiki wao. 14  Lakini nilipoona kwamba hawakuwa wakitembea kwa unyoofu kulingana na kweli ya habari njema,+ nilimwambia Kefa* mbele yao wote: “Ikiwa wewe, ingawa ni Myahudi unaishi kama mataifa wanavyoishi, na si kama Wayahudi wanavyoishi, unawezaje kuwalazimisha watu wa mataifa waishi kulingana na mazoea ya Kiyahudi?”+ 15  Sisi tulio Wayahudi kwa kuzaliwa, na si watenda dhambi kutoka kwa mataifa, 16  tunatambua kwamba mtu hutangazwa kuwa mwadilifu, si kupitia matendo ya sheria, bali kupitia tu imani+ katika Yesu Kristo.+ Basi sisi tumeweka imani yetu katika Kristo Yesu, ili tutangazwe kuwa waadilifu kupitia imani katika Kristo bali si kupitia matendo ya sheria, kwa maana hakuna mtu yeyote atakayetangazwa* kuwa mwadilifu kupitia matendo ya sheria.+ 17  Sasa ikiwa sisi pia tumepatikana kuwa watenda dhambi tulipokuwa tukitafuta kutangazwa kuwa waadilifu kupitia Kristo, basi je, Kristo ni mhudumu wa dhambi? La hasha! 18  Ikiwa ninayajenga tena mambo ambayo wakati mmoja niliyabomoa, ninaonyesha kwamba mimi ni mkosaji. 19  Kwa maana kupitia sheria nilikufa kuielekea sheria,+ ili niwe hai kumwelekea Mungu. 20  Mimi nimetundikwa mtini pamoja na Kristo.+ Si mimi tena niliye hai,+ bali ni Kristo anayeishi katika muungano na mimi. Kwa kweli, uhai ninaoishi sasa katika mwili ninaishi kwa imani katika Mwana wa Mungu,+ aliyenipenda na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.+ 21  Mimi sizikatai* fadhili zisizostahiliwa za Mungu,+ kwa maana ikiwa uadilifu ni kupitia sheria, kwa kweli Kristo alikufa bure.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kwa saa moja.”
Pia anaitwa Petro.
Au “ushirikiano.”
Au “alikuwa na hatia.”
Au “nilimkabili.”
Pia anaitwa Petro.
Pia anaitwa Petro.
Tnn., “mwili utakaotangazwa.”
Au “sizitupi.”