Barua ya Pili kwa Wakorintho 6:1-18

  • Fadhili za Mungu hazipaswi kutumiwa vibaya (1, 2)

  • Huduma ya Paulo yafafanuliwa (3-13)

  • Msifungwe nira isivyo sawa (14-18)

6  Huku tukifanya kazi pamoja naye,+ tunawahimiza pia msipokee fadhili zisizostahiliwa za Mungu na kukosa kusudi lake.+  Kwa maana anasema: “Katika wakati unaokubalika nilikusikia, na katika siku ya wokovu nilikusaidia.”+ Tazama! Sasa ndio wakati unaokubalika hasa. Tazama! Sasa ndiyo siku ya wokovu.  Hatutoi sababu yoyote ya kukwaza, ili kosa lolote lisipatikane katika huduma yetu;+  bali katika kila njia tunajipendekeza kuwa wahudumu wa Mungu,+ kwa kuvumilia mengi, kwa dhiki, kwa nyakati za uhitaji, kwa shida,+  kwa kupigwa, kwa kufungwa gerezani,+ kwa machafuko, kwa kazi ngumu, kwa kukosa usingizi usiku, kwa nyakati za kukosa chakula;+  kwa utakaso, kwa ujuzi, kwa subira,+ kwa fadhili,+ kwa roho takatifu, kwa upendo usio na unafiki,+  kwa kusema maneno ya kweli, kwa nguvu za Mungu;+ kupitia silaha za uadilifu+ katika mkono wa kulia* na wa kushoto,*  kupitia utukufu na aibu, kupitia habari mbaya na habari nzuri. Tunaonwa kuwa wadanganyifu na bado tunasema ukweli,  kama wasiojulikana na bado tunatambuliwa, kama wanaokufa* na bado, tazama! tunaishi,+ kama walioadhibiwa* na bado hatujakabidhiwa kwenye kifo,+ 10  kama walio na huzuni lakini wanaoshangilia sikuzote, kama maskini lakini wanaowatajirisha wengi, kama wasio na kitu chochote na bado walio na vitu vyote.+ 11  Tumefungua kinywa chetu ili kuzungumza* nanyi, enyi Wakorintho, nasi tumefungua wazi moyo wetu. 12  Hatujajizuia* kuwaonyesha upendo,+ bali ninyi mmejizuia kutuonyesha upendo wenu mwororo. 13  Kwa hiyo, kwa kujibu—ninazungumza kama na watoto wangu—ninyi pia fungueni kabisa mioyo yenu.*+ 14  Msifungwe nira* isivyo sawa pamoja na wasio waamini.+ Kwa maana kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi sheria?+ Au nuru ina ushirika gani na giza?+ 15  Isitoshe, kuna upatano gani kati ya Kristo na Beliali?*+ Au mwamini* ana ushirika gani* na mtu asiye mwamini?+ 16  Na hekalu la Mungu lina makubaliano gani na sanamu?+ Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu aliye hai;+ kama Mungu alivyosema: “Mimi nitakaa miongoni mwao+ na kutembea miongoni mwao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+ 17  “‘Kwa hiyo, tokeni miongoni mwao na mjitenge,’ asema Yehova,* ‘na mwache kugusa kitu kichafu’”;+ “‘nami nitawakaribisha ndani.’”+ 18  “‘Nami nitakuwa baba kwenu,+ nanyi mtakuwa wana na mabinti kwangu,’+ asema Yehova,* Mweza Yote.”

Maelezo ya Chini

Labda kwa ajili ya kujilinda.
Labda kwa ajili ya kushambulia.
Au “tunaonwa kama wanaostahili kifo.”
Au “waliotiwa nidhamu.”
Au “Tumezungumza waziwazi.”
Au “Hatujakosa nafasi ya.”
Au “ninyi pia panukeni.”
Au “Msiunganishwe.”
Au “mwamini ana fungu gani.”
Au “mtu mwaminifu.”
Kutokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “Asiyefaa Kitu.” Linamrejelea Shetani.