Hamia kwenye habari

Je, Biblia Inazungumza Kuhusu Toharani?

Je, Biblia Inazungumza Kuhusu Toharani?

Jibu la Biblia

 Hapana. Biblia haina neno “toharani,” wala haifundishi kwamba nafsi za watu waliokufa zinasafishwa toharani. a Fikiria kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu dhambi na kifo na jinsi hilo linavyopingana na fundisho la toharani.

  •   Imani katika damu ya Yesu ndiyo husafisha dhambi za mtu, si kuishi toharani kwa muda. Biblia inasema kwamba “damu yake Yesu, Mwana wake [Mungu], yatusafisha dhambi yote” na kwamba “Yesu Kristo . . . kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu.” (1 Yohana 1:7, Union Version; Ufunuo 1:5, Biblia Habari Njema) Yesu Kristo alitoa “maisha yake kuwa fidia ya watu wengi” ili kulipia dhambi zao.​—Mathayo 20:28, BHN.

  •   Watu waliokufa hawajui lolote. “Walio hai hujua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui chochote.” (Mhubiri 9:5, BHN) Mtu ambaye amekufa hawezi kuhisi chochote na hivyo hawezi kusafishwa kwa moto wowote ulio toharani.

  •   Hakuna adhabu ya dhambi baada ya mtu kufa. Biblia inasema kwamba “mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo” na kwamba mtu “ambaye amekufa ameondolewa hatia ya dhambi yake.” (Waroma 6:7, 23) Kifo ndiyo adhabu kamili ya dhambi.

a Kuhusu toharani, kitabu Orpheus: A General History of Religions kinasema kwamba “hakuna jambo lolote kulihusu katika Injili.” Vivyo hivyo, kitabu New Catholic Encyclopedia kinasema: “Kwa ujumla, msingi wa fundisho la Katoliki kuhusu toharani ni mapokeo, si Maandiko Matakatifu.”​—Toleo la Pili, Buku la 11, ukurasa wa 825.

b Ona kitabu New Catholic Encyclopedia, Toleo la Pili, Buku la 11, ukurasa wa 824.