Ona video zinazopatikana

Walijitoa kwa Kujipendea​—Mu Bulgaria

Walijitoa kwa Kujipendea​—Mu Bulgaria

 Mashahidi wa Yehova wa mu Bulgaria wako wanafundisha sana watu juu ya Mungu na Neno yake Biblia. Tangu mwaka wa 2000, Mashahidi wa Yehova wengi wa mu mainchi ingine wamehamia mu Bulgaria ili kuwasaidia ndugu zao mu ile kazi. Kunakuwaka magumu gani ya kuhamia mu inchi ya kigeni ili kuhubiri? Juu ya nini ni muzuri kufanya vile? Tuzungumuzie mambo fulani yenye wale wenye walihamia mu Bulgaria walisema.

Kujiwekea Muradi

 Darren mwenye anaishi mu inchi ya Uingereza anasema hivi: “Sikuzote, tulikuwa na muradi wa kutumikia mu inchi ingine kwenye kuwa lazima kubwa. Kisha kumuoa Dawn, tulihamia Londres ili kufundisha Biblia mu luga ya Kirusi.” Wakati fulani, tulikuwa na mipango ya kuhama lakini juu ya sababu mingi hatukuweza kuenda. Tuliwaza kama hatungeweza kuenda, kisha rafiki moya alitusaidia kuona kama hali yetu imebadilika na kama tungeweza kuhamia fasi ingine.” Darren na Dawn walianza kutafuta inchi kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri na kwenye wangeweza kabisa kuhamia. Mu 2011, walihamia Bulgaria.

Darren na Dawn

 Mifano ya muzuri ya wale wenye walihamia mu inchi ingine ilitia moyo watu fulani wenye ku mwanzo hawakukuwa na muradi wa kutumikia mu inchi ingine. Giada mwenye anaishi mu Italia pamoya na bwana yake Luca, anasema hivi: “Nilikutana na Mashahidi wenye bidii, wenye walitumika kwa furaha mu Amerika ya Kusini na mu Afrika. Furaha yao na mambo yenye waliniambia ilinigusa sana. Ile ilinisaidia nirekebishe miradi yangu ya kiroho.”

Luca na Giada

 Tomasz na Veronika walitoka mu Jamuhuri ya Cheki ili kuenda Bulgaria mu 2015 pamoya na watoto wao wawili, Klara na Mathias. Nini njo iliwachochea kuhama? Tomasz anasema hivi: “Tulichunguza kwa ukaribu mifano ya wengine wenye walihamia mu inchi ingine, kutia ndani watu wa familia yetu na tulifikiri sana juu ya mambo fulani ya muzuri yenye walijionea. Furaha yao ilitugusa sana na tuliizungumuzia ku nyumba.” Sasa watu wa hii familia yenye furaha wako wanahubiri mu eneo ya mupya katika muji wa Montana mu Bulgaria.

Klara, Tomasz, Veronika, na Mathias

 Linda ni Shahidi mwingine mwenye alihamia Bulgaria. Anasema hivi: “Kumepita miaka mingi nilitembeleaka Équateur na nikakutana na watu fulani wenye walihamiaka kule juu ya kuhubiri. Ile ilifanya niwaze kama kuko siku moya tu nitatumikiaka fasi kwenye kuko lazima kubwa.” Petteri na Nadja, bibi na bwana wa Finlandi, nao pia walifikiri sana juu ya mufano wa wengine. Walisema hivi: “Mu kutaniko yetu, tulikuwa na wahubiri fulani wenye uzoefu wenye walihamiaka fasi fulani ili kuhubiria watu. Sikuzote walikuwa wanazungumuzia kwa uchangamufu miaka yote yenye walipitisha mu ile utumishi. Walisema kama ile njo ilikuwaka miaka ya muzuri zaidi mu maishi yao.”

Linda

Nadja na Petteri

Kupanga Mambo Mbele ya Wakati

 Ni jambo ya maana sana kwa wale wenye wanapenda kutumikia mu inchi ingine kupanga mambo mbele ya wakati. (Luka 14:28-30) Nele wa Belgique anakumbuka hivi: Wakati nilianza kufikiri kwa uzito juu ya kutumikia mu inchi ingine, nilisali na kutafuta habari mu vichapo vyetu, habari zenye kuzungumuzia mambo ya kufanya ili kutumikia mu inchi ya kigeni. Nilijifunza zile habari na nilijikaza kujua nini iliomba kufanya juu niweze kuwa tayari kuhama.”

Nele (mwenye iko ku mukono wa kuume)

 Kristian na Irmina wa Polandi, wameishi mu Bulgaria kwa zaidi ya miaka kenda. Walielewa kama walifanya muzuri zaidi kuhuzuria mu kikundi ya Kibulgaria mu inchi ya Polandi mbele wahame. Ile kikundi iliwatia moyo na iliwasaidia wajifunze luga. Kristian na Irmina walisema hivi: “Tulifikia kuelewa kama ni muzuri sana kuwa tayari kujitolea na kuona namna Yehova Mungu anahangaikia mahitaji yetu. Wakati uko tayari kumuambia Yehova, ‘Mimi huyu! Unitume mimi!’ unaweza kufanya mambo yenye hauyawazaka kama unaweza kufanya.”​—Isaya 6:8.

Kristian na Irmina

 Juu ya kujitayarisha na kutia makuta kidogo pembeni, Reto na Cornelia, bibi na bwana wa Uswisi, waliamua kuishi maisha ya mwepesi. Wanasema hivi: “Mwaka moya mbele tuhame, tulienda Bulgaria kwa juma moya juu tujue maisha ilikuwa namna gani kule. Kule, tulizungumuza na wamisionere wenye kuwa na uzoefu wenye walitupatia mashauri yenye kufaa.” Reto na Cornelia walitumia muzuri mashauri yenye walipata na kwa sasa wamefanya miaka zaidi ya 20 mu Bulgaria.

Cornelia na Reto, pamoya na watoto wao wanaume Luca na Yannik

Namna ya Kupambana na Magumu

 Wale wenye wamehamia mu inchi ya kigeni wanapaswa kujipatanisha na hali za mupya na pengine zingine zenye kuwa nguvu sana. (Matendo 16:9, 10; 1 Wakorinto 9:19-23) Shida kubwa ya watu wengi ni kujifunza luga ya mupya. Luca mwenye tulishataya anasema hivi: “Sikuzote tulikuwa tunafurahia kutoa maelezo mu maneno yetu ku mikutano. Lakini wakati fulani ilikuwa nguvu sana kwangu na kwa bibi yangu kutayarisha hata jibu moya ya mwepesi mu Kibulgaria! Ilikuwa sawa vile tunakuwa watoto tena. Kusema kweli, watoto wenye Kibulgaria njo ilikuwa luga yao ya kizalikio walikuwa natoa maelezo ya muzuri sana hata kuliko yetu.”

 Ravil wa Alemanye alisema hivi: “Kujifunza luga ya mupya kulikuwa nachokesha sana. Lakini niliendelea kuwaza hivi, ‘Usijione kuwa wa maana sana, cheka kidogo wakati unafanya makosa.’ Niliona magumu sawa vile haiko magumu lakini sawa sehemu ya utumishi wangu mutakatifu kwa Yehova.”

Ravil na Lilly

 Linda, mwenye tulishataya anasema hivi: “Mu mambo ya kujifunza luga nakuwaka bure kabisa. Haikuwake mwepesi kujifunza Kibulgaria. Na mara mingi nilifikiria tu kuacha. Unaweza kujisikia weye peke wakati hauwezi kuzungumuza na watu na hauelewe mambo yenye wako wanasema. Juu ya kutia nguvu hali yangu ya kiroho, nilijifunza mambo yote mu Kisuede. Ku mwisho, kwa musaada wa ndugu na dada nilifikia kujua ile luga.”

 Kukumbuka kwenye ulitokaka inaweza kuwa jaribu ingine. Wale wenye wanahama wanaacha watu wa familia yao na marafiki wao. Eva mwenye alihamia Bulgaria na bwana yake Yannis alisema hivi: “Ku mwanzo nilijisikia miye peke. Juu ya kupiganisha ile hali, tulikuwa tunazungumuza kikawaida na familia yetu na marafiki wetu wenye tuliachaka na tulijikaza kuwa na marafiki wapya hapa.”

Yannis na Eva

 Kuko magumu ingine. Robert na Liana, wenye walihama kutoka Uswisi walisema hivi: “Luga na desturi ilikuwa shida sana kwetu na hatukujitayarisha juu ya baridi yenye tulikuta hapa.” Kuwa na mawazo ya muzuri na kuwa watu wenye kuchekesha wengine kidogo kumesaidia ule ndugu na bibi yake kutumika mu Bulgaria kwa uaminifu muda wa miaka 14 yenye imepita.

Robert na Liana

Baraka

 Lilly anatia moyo wengine kuenda kuhubiria fasi kwenye kuko lazima kubwa. Alisema hivi: “Nilifikia kumujua Yehova mu njia yenye pengine kama ningebakiaka mu inchi yetu singemujuaka. Niko na mambo mingi sana ya kufanya ili kusaidia wengine na ile imenisaidia nikomale kiroho na inanipatia furaha na niko mwenye kutosheka.” Ravil, bwana yake anakubaliana naye. Alisema hivi: “Hii njo maisha, nafasi ya pekee sana ya kufikia kujua Wakristo wenye bidii wa mu inchi mbalimbali wenye kuwa na uzoefu mingi ya kufundisha kweli za Biblia. Nimejifunza mambo mingi sana kutoka kwao.”

 Utayari na roho ya kujitolea ya wengi imesaidia kuhubiri “habari njema ya Ufalme . . . katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” (Matayo 24:14) Juu wako na roho ya kujitolea, wale wenye wamekuja Bulgaria wameona namna Yehova ametimiza tamaa za moyo wao na kufanya mipango yao yote iendeke muzuri.​—Zaburi 20:1-4.