Ona video zinazopatikana

Tuliamua Kufanya Maisha Yetu Ikuwe Mwepesi

Tuliamua Kufanya Maisha Yetu Ikuwe Mwepesi

 Madián na Marcela walikuwa na maisha ya muzuri katika Medellín, Kolombia. Madián alikuwa na nalipwa muzuri ku kazi yake, na juu ya ile waliishi mu nyumba ya muzuri. Lakini, jambo fulani iliwafanya wachunguze tena mambo yenye wanapaswa kutia pa nafasi ya kwanza, juu walikuwa watumishi wa Yehova Mungu. Wanasema hivi: “Mu 2006, tulihuzuria Mukusanyiko wa Pekee wenye kichwa ‘Uwe na Jicho Rahisi.’ Hotuba za mingi zilitutia moyo kufanya maisha yetu ikuwe mwepesi juu tuweze kumutumikia Yehova zaidi. Wakati tulitoka ku mukusanyiko, tulitambua kama hatukukuwa nafanya vile. Tulikuwa napenda kuuza vitu mingi na ile ilifanya tujiingize mu madeni.”

 Kisha kufuata zile hotuba, Madián na Marcela walianza kufanya maisha yao ikuwe mwepesi. Wanasema hivi: “Tulianza kupunguza garama. Tulihamia mu nyumba ya kidogo, tuliuzisha gari yetu, na kuuza pikipiki.” Zaidi ya ile, waliacha kuenda mu maduka ya kabambi-kabambi juu wasishawishiwe kuuza-uza vitu. Walianza kupitisha wakati zaidi pamoya na majirani wao na wako nazungumuza nao kuhusu Biblia. Na walifanya urafiki na mapainia wa pekee, wenye walikuwa namutumikia Yehova Mungu kwa bidii. *

 Bila kukawia, Madián na Marcela waliamua kupanua utumishi wao kwa kuhamia mu kutaniko ya kidogo ya mu maeneo ya mashamba yenye ilikuwa na lazima kubwa ya musaada. Juu waweze kuhama, Madián aliacha kazi yake. Mukubwa wake wa kazi hakuelewa juu ya nini aliacha kazi ya muzuri vile. Kwa hiyo, Madián alizungumuza naye, na kumuuliza hivi: “Unapataka makuta ya mingi, lakini uko na furaha?” Mukubwa wake wa kazi alisema kama hana furaha, juu iko na magumu ya mingi yenye hawezi kumaliza. Kisha, Madián alimuambia hivi: “Ya maana mu maisha haiko uwingi wa makuta yenye unapataka. Lakini ya maana ni mambo yenye inafanya ukuwe na furaha kabisa. Kufundisha watu juu ya Mungu kunafanya miye na bibi yangu tukuwe na furaha, na tunapenda tukuwe na furaha zaidi kwa kutumia wakati zaidi mu hii kazi.”

 Madián na Marcela wametosheka kabisa na kupata furaha kwa kufuatia miradi ya kiroho. Kwa miaka 13 yenye imepita, wametumikia fasi kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri mu kutaniko fulani kaskazini-mangaribi mwa Kolombia. Na kwa sasa wako na pendeleo ya kutumika kama mapainia wa pekee.

^ Painia wa pekee anawekwa na biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya inchi yake juu ya kuhubiri habari njema wakati yote mu eneo fulani. Biro ya tawi inamutimiziaka mahitaji yake ya musingi kwa kumupatiaka makuta kidogo.