Ona video zinazopatikana

Mapadri Wenye Kasirani Wanatendewa Kwa Upole

Mapadri Wenye Kasirani Wanatendewa Kwa Upole

 Artur, mwangalizi wa muzunguko mu Armenia, alikuwa natembelea kutaniko fulani ya Mashahidi wa Yehova. Alivumbula kama ile kutaniko haifanyake mahubiri ya mahali pa watu wengi, yenye inaomba kutumia prezantware. Juu ya kutia moyo ndugu wa mu ile kutaniko waanze kuhubiri na prezantware, Artur na bibi yake, Anna, pamoya na Shahidi mwingine mwenye kuitwa Jirayr, walitia prezantware mu muji fulani mudogo. Walichagua fasi kwenye watu wengi wanapitaka.

 Mara moya wapita-njia walianza kupendezwa na kukamata vichapo. Lakini, kisha wakati kidogo, wapinzani pia walianza kuona prezantware. Mapadri wawili walikaribia prezantware, na bila hata kuuliza jambo fulani, mumoja kati yao, aliisukuma na miguu na ikaanguka. Kisha, akapiga Artur kofi mu sura, na akaangusha linete yake. Artur, Anna, na Jirayr walijaribu kutuliza wale mapadri, lakini hawakuweza. Wale mapadri walisukuma prezantware na miguu yao na vichapo vikasambalana. Kisha kufokea Mashahidi, kuwaambia mambo ya mubaya, na kuwaogopesha, wakaenda.

 Artur, Anna, na Jirayr walipeleka mambo ku biro ya polisi. Walifasiria mambo yenye ilitokea na kwa kifupi walizungumuza juu ya Bibla na wakubwa wa polisi na wengine wenye walikuwa natumika ku biro ya polisi. Kisha, wale Mashahid watatu walipelekwa mu biro ya polisi-musimamizi. Ku mwanzo, ule polisi-musimamizi alipenda tu kujua mambo yenye ilitokea. Lakini, wakati alifikia kujua kama Artur, mwanume mwenye nguvu, hakupigana kisha kupigwa kofi, ule polisi-musimamizi aliacha kuuliza maulizo kuhusu ile jambo na alianza kuuliza maulizo kuhusu mambo yenye Mashahidi wa Yehova wanaamini. Ile ilifanya wazungumuze naye kwa saa ine! Ule polisi-musimamizi alishangazwa sana na mambo yenye alisikia na alifikia kusema hivi: “Dini ya muzuri kabisa! Na miye nitajiunga na nyiye!”

Artur na Anna

 Siku ya kufuata, wakati Artur alianza tena kuhubiri ku prezantware, mwanaume fulani, mwenye alionaka mambo yenye ilitokeaka ile siku alimukaribia. Alimupongeza Artur juu alibakia mutulivu na juu hakupiganaka na wale mapadri. Alimuambia kama mambo yenye alionaka ilifanya asiheshimie tena mapadri.

 Ile mangaribi, ule polisi-musimamizi alimuita tena Artur ku biro ya polisi. Lakini, kuliko kuzungumuzia mambo yenye ilitokeaka, alimuuliza maulizo ya mingi juu ya Biblia. Na polisi wawili walijiunga nao ku ile mazungumuzo.

 Siku ya kufuata, Artur alitembelea tena ule polisi-musimamizi juu ya kumuonyesha video fulani zenye kutegemea Biblia. Ule polisi-musimamizi aliita polisi wengine wakuye kuangalia naye zile video.

 Kupitia matendo ya mubaya ya wale mapadri, polisi wengi walipata nafasi ya kuhubiriwa kwa mara ya kwanza. Ile ilifanya wakuwe na mawazo ya muzuri juu ya Mashahidi wa Yehova.