Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanamuke Wanahubiriaka?

Mashahidi wa Yehova Wanamuke Wanahubiriaka?

 Ndiyo. Mashahidi wa Yehova wote ni wahubiri, na hata mamilioni ya wanamuke wanahubiriaka pia. Kama vile tu Biblia inasema: “Wanamuke wenye kutangaza habari njema ni jeshi kubwa.”​—Zaburi 68:11.

 Mashahidi wa Yehova wanamuke wanafuata mufano wa wanamuke wa zamani wenye wanazungumuziwa mu Biblia. (Mezali 31:10-​31) Hata kama hawako viongozi mu kutaniko, wanahubiriaka sana habari njema. Tena, wanafundishaka watoto wao kanuni za Biblia. (Mezali 1:8) Maneno na matendo yao ya muzuri inafanyaka wengine wajikaze kuwaiga.​—Tito 2:3-5.