Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawafanyake Sikukuu za Kuzaliwa?

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawafanyake Sikukuu za Kuzaliwa?

 Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu ya kuzaliwa juu wanaamini kama ile sikukuu haimufurahisheMungu. Biblia haionyeshe waziwazi kama hatupaswe kufanya sikukuu ya kuzaliwa lakini inatusaidia kuelewa mawazo ya Mungu kuhusu zile sikukuu. Tuone mambo ine yenye inatusaidia kujua mawazo ya Mungu kuhusu sikukuu za kuzaliwa.

  1.   Sikukuu za kuzaliwa zilianzishwa na wapagani. Kitabu Funk & Wagnalls Standard Dictionary of Folklore, Mythology, and Legend inaonyesha kama watu wenye kufanya sikukuu za kuzaliwa waliamini kuwa wakati tarehe yenye mutu alizaliwa inafika kunakuwaka roho wabaya na mikoshi yenye inaweza kumutendea mubaya. Lakini, wakati marafiki wanakuwa pale na kumutakia mambo ya muzuri, ile inasaidia kumulinda juu mambo ya mubaya isimupate. Kitabu Lore of Birthdays inasema kama zamani tarehe ya kuzaliwa ilikuwa ya lazima juu ya kujua mambo yenye itatokea mu maisha ya mutu. Na ile ilikuwa nafanywa kwa kutegemea elimu ya nyota, sayansi yenye haijulikane. Ile kitabu inaongezea kama watu waliamini kuwa kuwasha mishumaa wakati wa sikukuu ya kuzaliwa kuko na nguvu fulani ya pekee ya kusaidia kutimizia mutu tamaa zake.

     Lakini Biblia inakataza uchawi, uaguzi, kupashana habari na pepo wachafu, ao “mambo kama hayo.” (Kumbukumbu la Torati 18:14; Wagalatia 5:19-​21) Watu wa Babiloni walikuwa wanasoma alama za nyota; ile ilikuwa pia uaguzi, na ni kati ya sababu zenye zilifanya Mungu aharibu muji wa Babiloni. (Isaya 47:11-​15) Mashahidi wa Yehova hawakatalake sikukuu zote kwa sababu juu tu ya namna zilianza. Lakini wakati Biblia inaonyesha muongozo wenye kuwa wazi, hawawezi kuufungia macho.

  2.   Wakristo wa kwanza-kwanza hawakukuwa nafanya sikukuu za kuzaliwa. Kitabu The World Book Encyclopedia inasema kama Wakristo waliona kufanya sikukuu ya kuzaliwa ya mutu yeyote kuwa desturi ya wapagani. Biblia inaonyesha kama mitume na wengine wenye walifundishwa moja kwa moja na Yesu waliacha mufano wenye Wakristo wote wanapaswa kufuata.​—2 Watesalonike 3:6.

  3.   Tukio yenye Wakristo wanapaswa kukumbuka ni kifo ya Yesu tu. (Luka 22:17-​20) Ile haitushangaze juu Biblia inasema kama “siku ya kufa inashindia siku ya kuzaliwa.” (Muhubiri 7:1) Wakati Yesu alikufa, alikuwa alishajifanyia jina ya muzuri mbele ya Mungu. Na ile ilifanya siku yake ya kufa ikuwe ya maana zaidi kuliko siku yake ya kuzaliwa.​—Waebrania 1:4.

  4.   Hakuna kwenye Biblia inasema kama mutumishi fulani ya Mungu alifanyaka sikukuu ya kuzaliwa. Haiko kusema kama waandikaji wa Biblia walisahau kuizungumuzia, juu Biblia inazungumuzia sikukuu mbili za kuzaliwa zenye zilifanywa na watu wenye hawakukuwa namutumikia Mungu. Lakini wakati wa zile sikukuu mbili kulifanyikaka mambo ya mubaya.​—Mwanzo 40:20-​22; Marko 6:21-​29.

Watoto wa Mashihidi wa Yehova wanaonaka kuwa wanakosa kitu fulani juu hawafanyake sikukuu za kuzaliwa?

 Sawa tu wazazi wote wazuri, wazazi Mashahidi wa Yehova wanaonyeshaka watoto wao upendo mwaka muzima. Wanawapatiaka zawadi na wakati fulani wanafanyaka karamu. Wanajikaza kufuata mufano mukamilifu wa Mungu mwenye anapatiaka watoto wake vitu vya muzuri siku zote, hapana tu tarehe fulani. Maneno yenye kufuata inaonyesha kama watoto wa Mashahidi wa Yehova hawajisikiake kama wanakosa kitu fulani juu tu hawafanyake sikukuu za kuzaliwa. (Matayo 7:11)

  •   “Inafurahisha sana kupokea zawadi wakati yenye haukukuwa nawazia.”​—Tammy, miaka 12.

  •   “Hata kama sipewake zawadi wakati wa tarehe yangu ya kuzaliwa, wazazi wangu wananipatiaka zawadi siku zingine. Ninafurahiaka ile juu wananipatiaka siku yenye sikuwazia.”​—Gregory, miaka 11.

  •   “Unawaza kujifurahisha dakika kumi, kula, keki fulani, na kuimba nyimbo njo fete? Kuya kwetu, utaona vile fete ya kweli inakuwaka.”​—Eric, miaka 6.