Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanakuwaka na Biblia Yao?

Mashahidi wa Yehova Wanakuwaka na Biblia Yao?

 Wakati Mashahidi wa Yehova wako najifunza Biblia, wanatumikishaka tafsiri mbalimbali za Biblia. Lakini kama Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya iko mu luga yao, njo yenye wanatumikishaka sana juu inatumia jina ya Mungu, haina makosa, na iko wazi.

  •   Inatumia Jina ya Mungu. Wachapishaji fulani wa Biblia wameshindwa kupatia sifa mwenye Biblia. Kwa mufano, tafsiri fulani ya Biblia inataya majina ya watu zaidi ya 70 wenye walisaidia juu ile tafsiri itolewe. Lakini, hakuna hata fasi kwenye ile tafsiri inatumia jina ya mwenye Biblia, Yehova Mungu!

     Tafsiri ya Ulimwengu Mupya haiko vile. Inatumia jina ya Mungu fasi mingi kwenye ile jina ilikuwaka mu maandishi ya kwanza-kwanza, na haionyeshe majina ya watu wenye walisaidia kuitafsiri.

  •   Haina makosa. Mu tafsiri za mingi muko makosa. Kwa mufano, mu Matayo 7:13, tafsiri moya inasema hivi: “Muingie kupitia mulango mwembamba, juu mulango wenye unapeleka ku moto wa mateso ni pana, na barabara yenye inapeleka kule ni mwepesi kupata.” Lakini, mu maandishi ya kwanza kwanza muko neno “uharibifu,” hapana “moto wa mateso.” Pengine watafsiri walitumia maneno “moto wa mateso” juu waliamini kama watu wabaya watateswa milele mu moto. Lakini Biblia haifundishe vile. Njo maana, mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, ile andiko inasema hivi: “Muingie kupitia mulango mwembamba, kwa sababu mulango ni mukubwa, na barabara yenye kuongoza kwenye uharibifu ni kubwa.”

  •   Iko wazi. Tafsiri ya muzuri haipaswe kuwa tu bila makosa, inapaswa kuwa pia wazi na mwepesi kuelewa. Tuone mufano moya. Mu Waroma 12:11, mutume Paulo alitumikisha maneno yenye neno kwa neno inamaanisha “roho kutokota.” Juu ile maneno haiko wazi mu Kiswahili, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya inatafsiri ile andiko mu njia yenye iko mwepesi kuelewa. Inasema kama Wakristo wanapaswa ‘kuwaka roho.’

 Tumeona kama Tafsiri ya Ulimwengu Mupya inatumia jina ya Mungu, haina makosa, na iko wazi. Lakini kuko jambo ingine yenye inafanya ikuwe tofauti na tafsiri zingine: Mutu anaweza kuipata bila kulipa. Ile inafanya watu wengi sana waweze kusoma Biblia mu luga yao, hata wale wenye hawana makuta ya kuuza Biblia.