Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Mashahidi wa Yehova Wanatembelea Watu Walio na Dini Zao?

Sababu Gani Mashahidi wa Yehova Wanatembelea Watu Walio na Dini Zao?

 Tumetambua kwamba watu wengi ambao tayari wana dini zao, wanafurahia mazungumuzo ya Biblia. Bila shaka, tunajua kama kila mutu iko huru kuchagua dini yake, na hatuwalazimishe watu wasikilize mahubiri yetu.

 Tunapozungumuza na watu wa dini zingine, tunajaribu kutumia shauri la Biblia linalotuomba tufanye hivyo kwa “tabia-pole” na tuonyeshe wengine “heshima kubwa.” (1 Petro 3:15) Tunajua kwamba watu fulani watakataa ujumbe wetu. (Mathayo 10:14) Hata hivyo, ni lazima tuzungumuze na watu kwanza ili tujue ikiwa watakubali ao kukataa ujumbe wetu. Tunajua pia kwamba hali za watu zinabadilika kila siku.

 Kwa mufano, mutu anaweza kukataa kutusikiliza kwa sababu ana kazi nyingi, lakini siku ingine anaweza kuzungumuza nasi kwa furaha. Tena, watu wanaweza kupambana na matatizo ao hali fulani zinazoweza kuwafanya wapendezwe na ujumbe wa Biblia. Kwa hiyo, tunajikaza kuzungumuza na watu mara kwa mara.