KAMPANYE YA UKUMBUSHO
Yesu Atamaliza Vita
Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alionyesha kama anapenda watu sana. Alifikia hata kutoa uzima wake kwa ajili yao. (Matayo 20:28; Yohana 15:13) Hivi karibuni, ataonyesha tena kama anapenda watu kwa kutumia mamlaka yake akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu ili “kumaliza vita katika dunia yote.”—Zaburi 46:9.
Ona namna Biblia inafasiria mambo yenye Yesu atafanya:
“Ataokoa maskini mwenye kulilia musaada, pia mutu wa hali ya chini na mutu yeyote mwenye hana musaidizi. Atamusikilia huruma mutu wa hali ya chini na maskini, na ataokoa uzima wa maskini. Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”—Zaburi 72:12-14.
Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yesu alishatufanyia na mambo yenye atatufanyia? Mu Luka 22:19, Yesu aliambia wanafunzi wake wakumbuke kifo yake. Njo maana kila mwaka, ku tarehe yenye Yesu alikufa, Mashahidi wa Yehova wanakutanaka juu ya kukumbuka kifo yake. Tunakukaribisha na weye ukuye kufanya Ukumbusho wa kifo ya Yesu pamoya na siye Siku ya Yenga, tarehe 24, Mwezi wa 3, 2024.