Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Siku ya Pentekoste mwaka wa 33, Wayahudi walikuja kabisa Yerusalemu “kutoka kila taifa kati ya yale yaliyo chini ya mbingu”?

Barabara Moja ya Yerusalemu Yenye Kujaa Watu Katika Mwaka wa 33.

Zaidi ya habari ya Biblia yenye kuelezwa katika Matendo 2:5-11, Philo, muandikaji Muyahudi aliyeishi wakati huo, aliandika habari yenye kusema juu ya kikundi cha watu wenye walikuja Yerusalemu kwenye Pentekoste mwaka wa 33 kisha kuzaliwa kwa Yesu.

Juu ya watu wenye walienda Yerusalemu, Philo aliandika hivi: “Watu wengi sana kutoka katika miji mingi, wamoja kupitia inchi, wengine kupitia bahari, kutoka mashariki na mangaribi na kusini na kaskazini walikuja kwenye kila sikukuu.” Pia alitaja maneno ya barua yenye Agripa wa Kwanza, mujukuu wa Herode Mukubwa, alitumia Caligula Mutawala wa Roma. Katika barua hiyo, Agripa alisema hivi juu ya Yerusalemu: “Muji Mutakatifu. . . ni muji mukubwa wa inchi ya Yudea lakini pia wa inchi zingine nyingi, kwa sababu ya vikundi vya watu wenye umetuma mara kwa mara katika inchi jirani mbalimbali.”

Agripa alitaja maeneo kwenye vikundi vya Wayahudi vilikuwa vinaishi, na hata maeneo ya mbali katika Mesopotamia, Afrika ya Kaskazini, Asia Ndogo, Ugiriki, na visiwa vya Mediterania. Joachim Jeremias, mutu mwenye elimu, anasema hivi: “Hata kama liste hiyo haizungumuzie waziwazi safari za kuenda Yerusalemu, wazo hilo halitajwe moja kwa moja, kwa sababu ilikuwa lazima kwa kila Muyahudi mwenye kuwa mutu muzima atembelee huko.”—Kumbukumbu la Torati 16:16.

Maelfu ya watu wenye walikuwa wanakuja Yerusalemu kwenye sikukuu za Wayahudi walikuwa wanapangishwa namna gani?

Sikukuu tatu zilikuwa zinafanywa kila mwaka katika Yerusalemu: sikukuu ya Pasaka, ya Pentekoste na ya Vibanda. Wakati wa mitume, maelfu ya watu walisafiri kutoka Israeli yote na kila mahali penye Wayahudi waliishi ili kuja Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu hizo. (Luka 2:41, 42; Matendo 2:1, 5-11) Watu hao wote walipaswa kupata nafasi ya kubakia.

Watu fulani walipitisha usiku pamoja na marafiki; wengine kwenye nyumba za wageni ao kwenye hoteli. Wengine wengi walilala katika mahema ndani ya muji ao kuzunguka kuta za muji. Wakati Yesu alikuja Yerusalemu kwa mara ya mwisho, alipanga katika muji wa Bethania wenye ilikuwa karibu.—Mathayo 21:17.

Majengo mengi yenye kuwa na beseni nyingi za kunawia yamevumbuliwa karibu na hekalu. Watu wanawaza kuwa majengo hayo yalikuwa nyumba za kupangisha wageni kwenye wangebakia na kujisafisha mbele ya kuingia katika hekalu. Maandishi fulani yenye yalivumbuliwa kwenye jengo moja kati ya majengo hayo yanaonyesha kama Théodote, kuhani na kiongozi wa sinagogi la eneo hilo, “alijenga sinagogi ili Sheria isomwe ndani na . . . zaidi ya hilo, nyumba ya wageni, na vyumba, na mahali pa kunawia ili kupangisha wageni wenye walikuwa na lazima.”