Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HEKIMA YA ZAMANI YENYE FAIDA LEO

Ukuwe Tayari Kusamehe

Ukuwe Tayari Kusamehe

KANUNI YA BIBLIA: ‘Muendelee . . . kusameheana kwa hiari [kwa kupenda] ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwengine. Kama vile Yehova alivyowasamehe ninyi kwa hiari, nanyi mufanye vivyo hivyo pia.’—Wakolosai 3:13.

Kusamehe kunamaanisha nini? Katika Biblia, zambi inafananishwa na deni na kusamehe kunafananishwa na kuondoa deni. (Luka 11:4) Kitabu fulani kinasema kama katika Biblia, neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “kusamehe” linamaanisha “kuachilia deni, kwa kuacha kulilipisha.” Kwa hiyo, wakati tunaamua kusamehe mutu mwenye ametukosea, tunaachilia mambo bila kutazamia tena kitu fulani kutoka kwake. Wakati tunasamehe mutu, hilo halimaanishe kama tulifurahia mambo mabaya yenye alitufanyia ao hayakutuumiza. Lakini, tunaamua tu kuacha kumuwekea kinyongo (kumukasirikia katika moyo) hata kama tuko na “sababu ya kulalamika” yenye kufaa.

Kusamehe kuko na faida leo? Kwa sababu hatukamilike, sisi wote tunafanya zambi. (Waroma 3:23) Kwa hiyo, tunaonyesha hekima wakati tuko tayari kusamehe wengine, kwa sababu leo ao kesho sisi pia tutakuwa na lazima watusamehe. Tena, wakati tunaamua kusamehe, tunajiletea faida sisi wenyewe. Namna gani?

Wakati tunaweka hasira na kinyongo katika moyo wetu, na tunakosa kusamehe, tunajiumiza wenyewe. Kuweka mambo kama hayo katika moyo kunaweza kutufanya tukose furaha, kunaweza kufupisha maisha yetu, na kutufanya tukuwe na huzuni. Tena, kunaweza kutuletea magonjwa hatari. Ripoti moja ya gazeti fulani la Amerika yenye iliandikwa na Musomi Yoichi Chida na Profesa wa Saikolojia Andrew Steptoe, ilisema hivi: “Uchunguzi wa hivi karibuni unaonyesha kama kuko upatano kati ya hasira na chuki na magonjwa ya moyo.” (Journal of the American College of Cardiology)

Lakini, tuone faida za kusamehe. Wakati tuko tayari kusamehe wengine, tunalinda umoja na amani, na hilo linasaidia kulinda urafiki. Na jambo la maana zaidi, tunaonyesha kama tunamuiga Mungu mwenye kuwa tayari kusamehe watenda zambi wenye kutubu, na mwenye anatuomba sisi pia tusamehe wengine.—Marko 11:25; Waefeso 4:32; 5:1.