Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Kuwa na uraia wa Roma kulimuletea mutume Paulo faida gani?

Paulo alisema hivi: “Ninakata rufani kwa Kaisari!”

Uraia wa Roma ulimufanya mutu akuwe na haki na mapendeleo fulani mahali popote alienda katika Utawala wa Roma. Raia wa Roma alijitiisha kwa sheria ya Roma, hapana sheria za miji ya majimbo. Wakati alishitakiwa, angekubali kusamba kulingana na sheria za eneo alipatikana ndani, lakini alikuwa pia na haki ya kusikiwa kwenye tribinali ya Roma. Ikiwa anahukumiwa kifo, alikuwa na haki ya kusamba mbele ya mutawala wa Roma.

Kwa sababu ya haki hizo, Cicero, mwanasiasa Muroma aliyeishi katika miaka 100 ya kwanza mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, alisema hivi juu ya sheria hizo: “Kumufunga raia wa Roma ni kuvunja sheria; kumupiga fimbo ni uovu; kumuua ni kama vile unaua muzazi ao mutu wa familia yako.”

Mutume Paulo alihubiri sana katika Utawala wote wa Roma. Maandiko yanaonyesha kuwa alitumia haki zake za uraia wa Roma mara tatu: (1) Aliwaambia waamuzi Wafilipi kuwa wamevunja haki zake kwa kumupiga. (2) Alionyesha kama alikuwa raia wa Roma ili asipigwe katika Yerusalemu. (3) Alikata rufani (aliomba aende kusamba) kwa Kaisari, mutawala wa Roma, ili amusikilize moja kwa moja.—Matendo 16:37-39; 22:25-28; 25:10-12.

Namna gani wachungaji walikuwa wanalipwa wakati wa zamani?

Maandishi haya yanaonyesha mapatano ya Kuuza Kondoo na mbuzi, Karibu Mwaka wa 2050 mbele ya Kuzaliwa kwa Yesu

Yakobo alichunga mifugo ya mujomba wake Labani kwa miaka 20. Alitumika miaka 14 ya kwanza ili aoe watoto wanawake wawili wa Labani, na miaka 6 iliyobaki, alipewa mushahara wa mifugo. (Mwanzo 30:25-33) Gazeti moja linasema kama “waandikaji na wasomaji wa zamani wa maandishi ya Biblia walijua sana makubaliano ya kuchunga wanyama, kama yale yaliyofanywa kati ya Labani na Yakobo.” (Biblical Archaeology Review)

Mapatano fulani kama hayo yalivumbuliwa chini ya udongo katika muji wa Nuzi, Larsa, na nafasi zingine katika inchi ya Irak ya leo. Kwa kawaida, mapatano yalifanywa katika kipindi cha mwaka cha kukata kondoo manyoya na yalimalizika kipindi cha mwaka uliofuata. Wachungaji walikubali daraka la kuchunga hesabu fulani ya wanyama wenye walihesabiwa kulingana na miaka na jinsia (ikiwa ni dume ao jike). Kisha mwaka moja, mwenye wanyama alipewa kiasi fulani chenye walikubaliana cha manyoya, vyakula vyenye kutokana na maziwa, watoto waliozaliwa na mifugo yake, na vitu vingine. Kila kitu cha zaidi kilikuwa cha muchungaji.

Kondoo waliongezeka ikiwa muchungaji alipewa kondoo jike wengi. Kondoo jike 100 walitazamiwa kuzaa wana-kondoo 80. Muchungaji alipaswa kulipa ikiwa wanyama walipunguka ao kupotea. Hilo lilimufanya achunge muzuri wanyama wenye alipewa.