Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | NAMNA YA KUFURAHIA KAZI YAKO

Kazi Ngumu​—Ingali ya Lazima Leo?

Kazi Ngumu​—Ingali ya Lazima Leo?

Alex anavuta pumuzi anaponyanyua kisanduku kingine na kukitia katika motokari ya kompanyi ya kuhamisha vitu ambamo anatumika. Anajiuliza yeye mwenyewe hivi: ‘Sababu gani ninashindwa kuacha kazi hii yenye hailete faida yoyote? Wakati gani nitapata matokeo ya muzuri katika kazi hii? Maisha yangu yangekuwa ya muzuri sana ikiwa sikukuwa ninafanya kazi!’

Kama vile Alex anayetajwa hapa juu, watu wengi leo hawafurahie kazi ngumu. Aaron anayefanya kazi ya kutengeneza motokari zilizoharibika anasema hivi: “Watu wengi wanafikiri kuwa hawastahili kufanya kazi ‘ya hali ya chini.’ Wanawaza hivi: ‘Ninafanya kazi hii mupaka siku nitapata kazi ya muzuri.’”

Sababu gani watu wengi wanajisikia kuwa hawastahili kufanya kazi ngumu? Pengine wanachochewa na vyombo vya kutangaza habari vinavyoonyesha mara nyingi maisha “ya muzuri sana” kuwa ni maisha ya raha na mepesi. Matthew, anayefanya kazi ya kutengeneza vitu vilivyoharibika anasema hivi: “Watu wanafikiri kuwa wakati unatumika sana ili kupata mambo uliyo nayo lazima, utapata matokeo kidogo ya muzuri katika maisha.” Shane anayefanya kazi ya kulinda majengo, alitambua pia mawazo hayo. Anasema hivi: “Watu hawapendi tena kutumika kadiri wanavyolipwa.”

Kwa upande mwengine, watu wengi walio na matokeo ya muzuri wanafurahia leo kazi ngumu. Daniel aliye na miaka 25, anayefanya kazi ya ujenzi anasema hivi: “Ninafikiri kuwa kazi ngumu ni yenye faida sana, zaidi sana wakati mutu anaifanya akiwa na miradi yenye kufaa.” Andre, aliye na miaka 23, anakubali pia hivyo. Anasema hivi: “Ninaamini kuwa kazi inaleta furaha na raha. Kutumika kidogo na kuwa na mambo kidogo ya kufanya hakulete furaha yenye kudumu, kunaleta tu muchoko wenye kudumu!”

Namna gani watu kama vile Daniel na Andre walifikia kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ngumu? Kwa kifupi, wametumia kanuni za Biblia katika maisha yao. Biblia haikataze kazi ngumu, inatia watu moyo watumike kwa bidii na kwa uvumilivu. Lakini Biblia haituambie tu tufanye kazi. Inatuonyesha pia namna ya kufurahia kazi yetu.

Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kukusaidia utosheke na kazi yako? Tunakuomba uchunguze kanuni fulani zenye kuzungumuziwa katika habari inayofuata.