Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walijitoa kwa Kujipendea—Katika Urusi

Walijitoa kwa Kujipendea—Katika Urusi

WALIJITOA KWA KUJIPENDEA Katika Urusi

KATIKA mwaka wa 1991, Mashahidi wa Yehova wa inchi ya Urusi walifurahi sana kuona kazi yao yenye ilikuwa imekatazwa kwa muda wa miaka mingi inakubaliwa kisheria. Wakati huo, watu wengi hawakuwazia kwamba leo hesabu ya Mashahidi wa Yehova ingeongezeka na kuwa 170000! Kati ya wahubiri hao wa Ufalme wenye bidii, kuna Mashahidi wa inchi zingine wenye walihamia katika inchi ya Urusi ili kusaidia katika kazi hiyo ya mavuno ya kiroho. (Mt. 9:37, 38) Acha tuzungumuzie wamoja kati yao.

NDUGU WENYE KUJIPENDEA WANASAIDIA KUTIA NGUVU MAKUTANIKO

Mwaka ambamo kazi ya Mashahidi wa Yehova ilikubaliwa katika inchi ya Urusi, Matthew wa inchi ya Grande Braitagne alikuwa na miaka 28. Kwenye mukusanyiko fulani wenye ulifanyika mwaka huo, hotuba moja ilikazia kwamba makutaniko ya Mashariki mwa Ulaya inahitaji musaada. Kwa mufano, musemaji alitaja kutaniko fulani la muji wa Saint-Pétersbourg, katika inchi ya Urusi, lenye halikuwa na muzee hata mumoja, lakini lilikuwa tu na mutumishi wa huduma mumoja. Hata hivyo, wahubiri walikuwa wanaongoza mamia ya mafunzo ya Biblia! Matthew anasema hivi: “Kisha hotuba hiyo, niliendelea kufikiria inchi ya Urusi; kwa hiyo, nilisali na kumuambia Yehova juu ya tamaa yangu ya kuhamia katika inchi hiyo.” Aliweka kiasi fulani cha feza, aliuzisha vitu vingi vyenye alikuwa navyo, kisha akahamia katika inchi ya Urusi mwaka wa 1992. Mambo ilimuendea namna gani?

Matthew

Matthew anasema hivi: “Ilikuwa vigumu kujifunza luga. Sikuweza kuanzisha mazungumuzo mazuri ya kiroho.” Tatizo lingine ilikuwa kupata nyumba. Anasema hivi: “Sikumbuke tena nilihama mara ngapi kwa kipindi cha muda mufupi.” Hata kama alipata matatizo hayo mwanzoni, Matthew anasema hivi: “Kuhamia katika inchi ya Urusi ndio uamuzi muzuri sana wenye nimechukua katika maisha yangu. Kutumikia katika inchi ya Urusi kumenifundisha kumutegemea sana Yehova na kujionea namna ananiongoza katika njia nyingi.” Kisha, Matthew aliwekwa kuwa muzee na painia wa pekee, na leo anatumikia katika biro moja ya tawi karibu na muji wa Saint-Pétersbourg.

Katika mwaka wa 1999, Hiroo alipewa cheti cha kumaliza Masomo ya Mazoezi ya Kihuduma katika inchi ya Japani, wakati alikuwa na miaka 25. Mwalimu moja kati ya walimu wake alimutia moyo aende kutumikia katika inchi ingine. Hiroo alikuwa amesikia kwamba kulikuwa lazima kubwa katika inchi ya Urusi na akaanza kujifunza luga ya Kirusi. Alichukua pia hatua ingine ya kumusaidia sana. Anasema hivi: “Nilienda kuishi katika inchi ya Urusi kwa muda wa miezi sita. Kwa sababu inchi hiyo iko na baridi nyingi, nilienda huko Mwezi wa 11 ili kuona ikiwa ninaweza kuzoea baridi hiyo.” Kisha kuishi katika baridi hiyo, alirudia katika inchi ya Japani, na huko alianza kuishi maisha mepesi ili aweke feza za kumusaidia kuhamia katika inchi ya Urusi.

Hiroo na Svetlana

Leo, Hiroo amefanya miaka 12 katika inchi ya Urusi na ametumikia katika makutaniko mengi. Wakati fulani, alikuwa muzee peke yake na alishugulikia wahubiri zaidi ya 100. Katika kutaniko moja, kila juma alikuwa anaongoza sehemu nyingi wakati wa Mukutano wa Utumishi, alikuwa anaongoza Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi, funzo la Munara wa Mulinzi, na Mafunzo tano ya Kitabu ya Kutaniko. Alitembelea pia ndugu na dada wengi ili kuwasaidia kiroho. Wakati Hiroo anakumbuka miaka hiyo, anasema hivi: “Kusaidia ndugu na dada wakuwe nguvu kiroho kuliniletea furaha kubwa.” Kutumikia mahali penye kuwa lazima kubwa, kumemuletea faida gani? Anasema hivi: “Mbele nihamie Urusi, nilikuwa muzee na painia, lakini kisha kufika katika inchi hiyo, nilijisikia kuwa nimekuwa na urafiki mupya pamoja na Yehova. Nimejifunza kumutegemea kabisa Yehova katika sehemu zote za maisha yangu.” Katika mwaka wa 2005, Hiroo alioa Svetlana, na wote wawili wanaendelea kufanya kazi ya upainia.

Michael na Olga pamoja na Marina na Matthew

Matthew mwenye kuwa na miaka 34 na ndugu yake Michael, mwenye kuwa na miaka 28, ni wa inchi ya Kanada. Wote wawili walitembelea Urusi na walishangaa sana kuona watu wengi wenye kupendezwa wanahuzuria mikutano lakini hakukuwa ndugu wengi ili kuongoza mikutano hiyo. Matthew anasema hivi: “Kutaniko lenye nilitembelea lilikuwa na muzee mumoja mwenye kuzeeka na kijana mumoja mutumishi wa huduma, lakini watu 200 walikuwa wanahuzuria mikutano. Wakati niliona uhitaji huo, nilichochewa kuhamia huko ili nisaidie ndugu hao.” Alihamia Urusi katika mwaka wa 2002.

Kisha miaka ine, Michael alihamia Urusi na bila kukawia alitambua kwamba kulikuwa kungali lazima ya ndugu. Kwa sababu alikuwa mutumishi wa huduma, aliombwa kushugulikia mambo ya feza za kutaniko, vichapo, na eneo. Aliombwa pia kufanya kazi yenye ingefanywa na mwandishi wa kutaniko, alikuwa anatoa hotuba za watu wote, na alisaidia katika kazi ya kutayarisha mikusanyiko na kujenga Majumba ya Ufalme. Bila shaka, ndugu wangali wanahitajiwa katika makutaniko ya inchi ya Urusi. Hata kama kushugulikia migawo mingi ni kazi ngumu, Michael, ambaye sasa ni muzee wa kutaniko, anasema hivi: “Kusaidia ndugu na dada kunaniletea furaha kubwa. Hii ndiyo njia nzuri zaidi ya kutumia maisha yangu!”

Wakati huo, Matthew alioa dada Marina, na Michael alioa dada Olga. Ndugu hao na bibi zao, pamoja na wengine wengi wenye kujitolea, wanaendelea kusaidia makutaniko iongezeke.

DADA WENYE BIDII WANASAIDIA KATIKA KAZI YA MAVUNO

Tatyana

Katika mwaka wa 1994, wakati dada Tatyana alikuwa na miaka 16, mapainia sita wa pekee kutoka République Tchèque, Polandi, na kutoka Slovakia walianza kutumikia katika kutaniko lake katika inchi ya Ukrainia. Anawakumbuka kwa furaha na kusema hivi: “Mapainia hao wenye bidii walikuwa wenye kukaribiwa kwa urahisi na wema, na walikuwa wanaelewa vizuri Biblia.” Alijionea namna Yehova alibariki roho yao ya kujitolea, na alisema hivi: ‘Ninapenda kuwa kama wao.’

Mufano wa mapainia hao ulimutia moyo sana; kwa hiyo, wakati wa mapumuziko ya masomo, Tatyana alisafiri pamoja na wengine ili kuenda kuhubiri katika maeneo ya mbali ya inchi ya Ukrainia na Biélorussie yenye ilikuwa haijahubiriwa. Alifurahia sana kuhubiri katika maeneo hayo; kwa hiyo, alifanya mipango ya kuhamia katika inchi ya Urusi ili kupanua utumishi wake. Kwanza, alitembelea inchi hiyo kwa muda mufupi ili kukutana na dada mwengine mwenye alikuwa amehamia huko, na pia ili kutafuta kazi ya kimwili yenye ingemutegemeza katika kazi ya upainia. Kisha, alihamia katika inchi ya Urusi mwaka wa 2000. Je, ilikuwa mwepesi kwake kufanya mabadiliko hayo?

Dada Tatyana anaeleza hivi: “Kwa sababu sikukuwa na uwezo wa kulipia nyumba nzima, nilipaswa kuishi katika chumba cha kulipia. Haikuwa mwepesi kuishi hivyo. Wakati fulani nilitaka kurudi nyumbani. Lakini, sikuzote Yehova alinisaidia nielewe kwamba nitapata faida kwa kuendelea kufanya utumishi wangu katika inchi hiyo.” Leo, dada Tatyana ni misionere katika inchi ya Urusi. Anamalizia kwa kusema hivi: “Miaka yote yenye nimepitisha katika inchi ingine ilinisaidia kujionea mambo mazuri sana na kupata marafiki wengi. Zaidi ya yote, miaka hiyo imenisaidia kufanya imani yangu ikuwe yenye nguvu zaidi.”

Masako

Dada Masako wa inchi ya Japani, mwenye iko na miaka zaidi ya 50, anatamani sana kuwa misionere, lakini matatizo ya afya haimuruhusu afanye kazi hiyo. Hata hivyo, wakati alisikia muzuri kwa kiasi fulani, aliamua kuhamia katika inchi ya Urusi ili kusaidia katika kazi ya mavuno. Hata kama ilikuwa vigumu kupata makao mazuri na kazi nzuri, alijikaza kujitegemeza kwa kufundisha luga ya Kijapani na kufanya kazi mbalimbali za nyumbani. Ni nini ilimusaidia aendelee na kazi yake ya kuhubiri?

Wakati anakumbuka miaka 14 yenye ametumikia katika inchi ya Urusi, dada Masako anasema hivi: “Furaha yenye ninapata katika kazi ya kuhubiri ni nyingi sana kuliko magumu yenye ninapata. Kuhubiri katika maeneo yenye kuwa na lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme kunanisaidia nikuwe na maisha ya bila kuhangaika na yenye furaha.” Anaongeza hivi: “Kwangu mimi, imekuwa kama muujiza kujionea namna Yehova amenisaidia kwa muda wa miaka hiyo yote kwa kunitolea chakula, manguo, na makao.” Zaidi ya kutumikia mahali penye kuwa lazima kubwa katika inchi ya Urusi, dada Masako ameshiriki pia katika kazi ya mavuno katika inchi ya Kirghizistan. Tena, ametegemeza vikundi vyenye kutumia luga ya Kiingereza, Kichina, na Uighur. Leo, ni painia katika muji wa Saint-Pétersbourg.

FAMILIA ZINATEGEMEZA NA ZINABARIKIWA

Inga na Mikhail

Kwa sababu ya matatizo ya kupata feza, mara nyingi familia nyingi zinahamia katika inchi zingine ili maisha yao ikuwe muzuri zaidi. Lakini kama vile Abrahamu na Sara, familia fulani zinahamia katika inchi zingine kwa sababu ya miradi ya kiroho. (Mwa. 12:1-9) Fikiria mufano wa ndugu Mikhail na dada Inga bibi yake, wenye walitoka katika inchi ya Ukrainia na kuhamia katika inchi ya Urusi katika mwaka wa 2003. Bila kukawia walipata watu wenye walikuwa wanatafuta kweli ya Biblia.

Mikhail anasema hivi: “Siku moja, tulihubiri katika eneo fulani lenye lilikuwa halijahubiriwa na Mashahidi wa Yehova hata siku moja. Mwanaume mumoja mwenye kuzeeka alifungua mulango na kutuuliza hivi: ‘Muko wahubiri?’ Wakati tulisema ndiyo, alisema hivi: ‘Nilijua kwamba mungefika siku moja. Maneno ya Yesu haiwezi kukosa kutimia.’ Kisha mwanaume huyo akataja maneno ya Mathayo 24:14.” Mikhail anaongezea hivi: “Katika eneo hilo, tulikutana pia na kikundi cha wanawake 10 wa dini ya Baptiste, ambao walikuwa na njaa ya kupata kweli. Walikuwa na kitabu Kuishi Milele, na kila mwisho wa juma walitumia kitabu hicho ili kujifunza Biblia. Kwa muda wa saa nyingi tulijibia maulizo yao na kuimba nyimbo za Ufalme, na tulikula chakula pamoja nao. Siku hiyo ni kati ya mambo mazuri sana yenye ninaendelea kukumbuka.” Mikhail na Inga wako hakika kwamba kutumikia mahali penye kuwa lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme kumewasaidia wamukaribie Yehova, wapende zaidi watu, na wamebarikiwa kwa kupata maisha yenye kufurahisha sana. Leo, wanatumikia katika muzunguko.

Oksana, Aleksey, and Yury

Katika mwaka wa 2007, ndugu Yury na dada Oksana bibi yake, wa inchi ya Ukrainia, wenye leo wako na miaka 35 hivi, pamoja na mutoto wao Aleksey, mwenye leo iko na miaka 13, walitembelea biro ya tawi ya Urusi. Huko, kwenye karte ya inchi ya Urusi waliona eneo kubwa lenye lilikuwa halijapewa kutaniko fulani. Oksana anasema hivi: “Kisha kuona karte hiyo, tulielewa vizuri sasa kwamba kuna lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme. Hilo lilituchochea kuanza kufikiria namna ya kuhamia katika inchi ya Urusi.” Ni jambo gani lingine liliwasaidia? Yury anasema hivi: “Kusoma katika vichapo vyetu habari kama vile, ‘Je, Unaweza Kutumikia Katika Eneo la Kigeni?’ kulitusaidia sana. * Tulitembelea eneo fulani katika inchi ya Urusi lenye biro ya tawi ilitupendekeza na tulitafuta nyumba na kazi.” Katika mwaka wa 2008, walihamia katika inchi ya Urusi.

Mwanzoni, ilikuwa vigumu kupata kazi, na mara nyingi walipaswa kuhama-hama. Yury anasema hivi: “Tulisali kila mara ili tusivunjike moyo; kisha tuliendelea kufanya kazi ya kuhubiri na kutumaini kwamba Yehova atatutegemeza. Wakati tunatia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza, tunajionea namna Yehova anatuhangaikia. Kazi hiyo ilitia nguvu familia yetu.” (Mt. 6:22, 33) Kutumikia mahali penye kuwa lazima kubwa kumeletea kijana Aleksey faida gani? Oksana anasema hivi: “Kumemusaidia sana. Alijitoa kwa Yehova katika sala na kubatizwa wakati alikuwa na miaka 9. Kutambua kwamba kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme kulimuchochea afanye kazi ya upainia musaidizi wakati wa mapumuziko ya masomo. Anapenda sana kuhubiri na anafanya kazi hiyo kwa bidii; hilo linatuletea furaha kubwa.” Leo, Yury na Oksana ni mapainia wa pekee.

“HUZUNI YANGU KUBWA”

Maneno ya wafanyakazi hao katika mavuno ya kiroho inaonyesha wazi kwamba, inaomba kumutegemea kabisa Yehova ili kupanua utumishi wako kwa kuhamia katika inchi ingine. Bila shaka, ndugu na dada wenye kutumikia mahali penye kuwa lazima kubwa wanapata magumu mbalimbali katika eneo lao mupya. Hata hivyo, kuhubiria watu wenye kupendezwa na habari njema ya Ufalme kunawaletea furaha kubwa. Unaweza kuwa tayari kusaidia katika kazi ya kukusanya mavuno mahali penye kungali lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme? Ukiamua kufanya hivyo, unaweza kujisikia kama Yury, mwenye alisema hivi kuhusu uamuzi wake wa kuhamia mahali penye kuwa lazima kubwa: “Huzuni yangu kubwa ni kwamba sikufanya hivyo mbele ya wakati.”

^ fu. 20 Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 1999, ukurasa wa 23-27.