Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Waisraeli walikuwa na chakula ingine mu jangwa zaidi ya mana na kware?

Mana njo chakula yenye Waisraeli walikula sana mu miaka 40 yenye walipitisha mu jangwa. (Kut. 16:35) Yehova aliwapatia pia mara mbili ndege wenye kuitwa kware. (Kut. 16:12, 13; Hes. 11:31) Lakini Waisraeli walikuwa na aina ingine kidogo ya chakula.

Kwa mufano, wakati fulani Yehova alikuwa naongoza watu wake “mahali pa kupumuzikia” kwenye walipata chakula na maji. (Hes. 10:33) Moja kati ya zile mahali ilikuwa oazisi ya Elimu, “mahali kwenye kulikuwa chemchemi kumi na mbili (12) na miti ya mitende makumi saba (70).” (Kut. 15:27) Kitabu Plants of the Bible inasema kama miti ya mitende “iliota fasi mingi, . . . na ilitumiwa sana mu jangwa. Ilitoa chakula, mafuta, na kivuli kwa mamilioni ya watu.”

Inawezekana Waisraeli walisimama kwenye oazisi yenye inajulikana leo kuwa Feiran, yenye kuwa sehemu ya Bonde la Muto wa Feiran. a Kitabu Discovering the World of the Bible inasema kama ile bonde la muto “iko na urefu wa kilometre 130. Kati ya mabonde ya mito yenye kuwa katika Sinai, iko kati ya mabonde ya mito yenye kuwa ya murefu zaidi, ya kupendeza zaidi, na yenye kujulikana sana. Kutoka kwenye muto unakutana na bahari mupaka ku oazisi ya Feiran, kuko kilometre 45 hivi. Ile oazisi iko na kilometre 4.8 yenye kujaa miti mingi ya mitende yenye kupendeza. Na iko ku karibu metre 610 juu ya usawa wa bahari. Ni yenye kupendeza sana mupaka imefananishwa na bustani ya Edeni. Kwa maelfu ya miaka, watu wengi wamevutiwa na ile fasi kwa sababu ya ile miti ya mitende.”

Miti ya mitende katika oazisi ya Feiran

Wakati Waisraeli walitoka Misri, walibeba unga wenye ulikuwa umefinyangwa, vyombo vya kufinyangia unga, na inawezekana walibeba pia mbegu fulani na mafuta. Bila shaka vile vitu havikukawia. Waisraeli walibeba pia “makundi na mifugo, mifugo mingi sana.” (Kut. 12:34-39) Lakini kwa sababu ya hali ngumu ya mu jangwa, hesabu ya wanyama wao ilipunguka. Pengine Waisraeli walikula wamoja kati yao. Na pengine wengine walitolewa kuwa zabihu, hata kwa miungu ya uongo. b (Mdo. 7:39-43) Lakini, Waisraeli waliendelea kufuga wanyama fulani. Maneno yenye Yehova aliambia Waisraeli wakati walikosa kabisa imani inaonyesha vile. Aliwaambia hivi: “Wana wenu watakuwa wachungaji katika jangwa kwa miaka makumi ine (40).” (Hes. 14:33) Kwa hiyo, inawezekana mifugo yao iliwapatia maziwa na wakati fulani nyama, lakini bila shaka haikukuwa ya kutosha kwa ajili ya watu karibu milioni tatu kwa miaka 40. c

Wanyama walipata wapi chakula na maji? d Inawezekana ile wakati mu jangwa mulikuwa mvua na mimea mingi zaidi kupita leo. Kitabu Étude perspicace des Écritures, Buku ya 1, inasema kama kumepita miaka 3500, “maji katika eneo ya Arabia ilikuwa ya mingi kupita yenye iko leo. Juu kuko mabonde ya mingi ya mito yenye kukauka, ile inaonyesha kama zamani mu ile eneo mulikuwa mvua ya mingi yenye ilifanyiza mito.” Hata vile, kwa ujumla jangwa ilikuwa fasi ya kuogopesha na yenye haikukuwa na chakula na maji. (Kum. 8:14-16) Kama Yehova hangewatolea maji kwa muujiza, Waisraeli na wanyama wao wangekufa.—Kut. 15:22-25; 17:1-6; Hes. 20:2, 11.

Musa aliambia Waisraeli kama Yehova aliwapatia mana ‘ili awafundishe kwamba mwanadamu haishi kwa mukate tu lakini mwanadamu anaishi kwa kila neno lenye linatoka katika kinywa cha Yehova.’—Kum. 8:3.

a Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 5, 1992, uku. 24-25.

b Biblia inazungumuzia mara mbili zenye Waisraeli walimutolea Yehova zabihu za wanyama mu jangwa. Mara ya kwanza ilikuwa wakati wa kuweka makuhani, na mara ya pili ilikuwa wakati wa Pasaka. Ile matukio yote ilifanyika mu mwaka wa 1512 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, mwaka wa pili kisha Waisraeli kutoka Misri.—Law. 8:14–9:24; Hes. 9:1-5.

c Ku mwisho-mwisho wa miaka 40 yenye Waisraeli walipitisha mu jangwa, walikamata mamia ya maelfu ya wanyama wenye walinyanganya ku vita. (Hes. 31:32-34) Hata vile waliendelea kula mana mupaka wakati waliingia mu Inchi ya Ahadi.—Yos. 5:10-12.

d Hakuna jambo yenye kuonyesha kama wanyama walikuwa nakula mana, juu Yehova aliambia Waisraeli kama kila mutu alipaswa kuokota mana yenye atamaliza, hakutaja wanyama.—Kut. 16:15, 16.