Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

TUIGE IMANI YAO | DAUDI

“Vita Ni vya Yehova”

“Vita Ni vya Yehova”

DAUDI anakamata kwenye kitu fulani wakati maaskari wanataka kumuangusha kwa sababu ya kukimbia ovyoovyo. Macho yao yanaonyesha kwamba wanaogopa wakati wanakimbia kutoka kwenye nafasi ya kupigania. Ni nini iliwaogopesha sana hivyo? Inawezekana Daudi aliwasikia wanarudilia tena na tena neno moja kwa wasiwasi. Walikuwa wanarudilia jina la mwanaume mumoja. Na katika bonde, mwanaume huyo alisimama kwa majivuno, na pengine alionekana kuwa munene kuliko mwanaume yeyote mwenye Daudi alikuwa amekwisha kuona.

Mwanaume huyo ni Goliathi! Bila shaka Daudi alielewa sababu gani maaskari hao walimuogopa. Mwanaume huyo alionekana kuwa munene sana, na mwenye urefu wa kushangaza sana. Hata bila kuvaa vifaa vyake vya vita vyenye kushangaza, inawezekana uzito wake ulipita uzito wa wanaume wawili wanene wenye kutiwa pamoja. Lakini alikuwa na silaha za kilo sana, alikuwa na nguvu nyingi sana, na alikuwa mupiganaji mwenye uzoefu. Goliathi alikuwa anaomba kwa sauti kubwa mutu akuje kupigana naye. Wazia namna sauti yake kubwa inasikilika kwenye vilima wakati anazarau jeshi la Israeli na Sauli, mufalme wao. Aliomba mwanaume akuje kupigana naye, na kushinda vita hiyo kwa kupigana na yeye tu!—1 Samweli 17:4-10.

Waisraeli walitetemeka sana. Mufalme Sauli alitetemeka pia. Daudi alisikia kwamba hali hiyo ilikuwa imefanya zaidi ya mwezi moja! Majeshi mawili, ni kusema, Wafilisti na Waisraeli, yaliangaliana tu wakati Goliathi alirudilia mazarau yake kila siku. Daudi alijisikia mubaya. Kwa kweli, ni jambo la haya sana kuona namna mufalme wa Israeli, maaskari wake, na ndugu watatu wa Daudi wanatetemeka sana kwa sababu ya woga! Kwa maoni ya Daudi, mupagani huyo Goliathi hakuwa anaogopesha tu jeshi la Israeli, lakini pia alikuwa anafanya jambo la mubaya zaidi; alikuwa anamutukana Yehova, Mungu wa Israeli! Lakini, Daudi mwenye alikuwa kijana tu, angeweza kufanya nini? Na imani ya Daudi inaweza kutufundisha nini leo?—1 Samweli 17:11-14.

‘UMUTIE MAFUTA, KWA MAANA HUYU NDIYE!’

Acha tuzungumuzie mambo yenye yalifanyika miezi mingi mbele ya hapo. Mangaribi fulani, Daudi alikuwa anachunga kondoo wa baba yake kwenye vilima vyenye kuwa karibu na Bethlehemu. Alikuwa mwenye kuvutia, na bila shaka wakati huo alikuwa angali kijana mudogo. Alikuwa na sura ya mwekundu na macho yenye kupendeza. Wakati wa kimya, alikuwa anapiga muziki kwa kutumia kinubi. Alivutiwa sana na uzuri wa vitu vyenye Mungu aliumba, na ufundi wake wa kupiga muziki uliendelea kuongezeka kwa sababu alifurahia kufanya mazoezi kwa saa nyingi. Lakini mangaribi hiyo, Daudi aliitwa nyumbani. Baba yake alipenda kumuona bila kukawia.—1 Samweli 16:12.

Wakati alifika, Yese, baba yake, alikuwa anazungumuza na mwanaume mwenye kuzeeka sana. Mwanaume huyo ni Samweli, nabii mwaminifu. Yehova alimutuma aende kutia mafuta mutoto mumoja kati ya watoto wa Yese ili akuwe mufalme wa Israeli pa nafasi ya Sauli! Samweli alikuwa ameona ndugu saba wakubwa wa Daudi, lakini Yehova alimuonyesha waziwazi kwamba hakuchagua mumoja kati yao. Lakini wakati Daudi alifika, Yehova alimuambia Samweli: ‘Umutie mafuta, kwa maana huyu ndiye!’ Mbele ya wakubwa wote wa Daudi, Samweli anafungua pembe lenye kuwa na mafuta ya pekee na kumwanga sehemu fulani kwenye kichwa cha Daudi. Maisha ya Daudi yanakuwa tofauti kisha kutiwa mafuta. Biblia inasema hivi: “Roho ya Yehova ikaanza kutenda kazi juu ya Daudi kuanzia siku hiyo na kuendelea.”—1 Samweli 16:1, 5-11, 13.

Kwa unyenyekevu, Daudi alionyesha kwamba ni Yehova ndiye alimusaidia kuua wanyama wakali wa pori

Daudi alianza kuonyesha tamaa ya kutawala? Hapana, alitosheka kwa kuacha roho ya Yehova imuonyeshe wakati wenye kufaa wa kutimiza madaraka makubwa zaidi. Wakati huo, aliendelea na kazi yake ya hali ya chini ya kuchunga kondoo. Daudi alijitoa kwa bidii katika kazi hiyo. Kondoo wa baba yake walikuwa katika hatari mara mbili, mara moja walishambuliwa na simba na mara ingine walishambuliwa na dubu. Daudi hakujaribu tu kukimbiza wanyama hao wakali akiwa mbali. Lakini, alianza kupigana nao mara moja ili kulinda kondoo wa baba yake. Katika hali hizo mbili, aliua wanyama hao yeye mwenyewe tu!—1 Samweli 17:34-36; Isaya 31:4.

Kisha muda fulani, Daudi aliitwa tena. Mufalme Sauli alisikia habari za muzuri juu yake. Hata kama alikuwa angali mupiganaji mwenye nguvu, Sauli alikuwa hakubaliwe tena na Yehova kwa sababu ya kutotii maagizo ya Mungu. Yehova alikuwa ametosha roho yake juu ya Sauli, ndiyo sababu aliingiliwa na roho mbaya kila mara. Alikuwa mwenye kukasirika, mwenye kuwaziana mubaya, na mukali. Wakati roho hiyo mbaya ilikuwa juu ya Sauli, ni muziki tu ndio ungeweza kumutuliza. Wanaume fulani wa Sauli walisikia kuhusu ufundi wa Daudi wa kupiga muziki na wa kupigana. Kwa hiyo Sauli alimuita Daudi, na kisha akamufanya kuwa mumoja wa wapiga-muziki kwenye makao yake na mumoja wa wabeba-silaha wake.—1 Samweli 15:26-29; 16:14-23.

Zaidi sana vijana wanaweza kujifunza mambo mengi juu ya imani ya Daudi katika mambo haya. Tunaona kwamba Daudi alitumia wakati wake mwengine ili kufanya mambo yenye yalimusaidia kumukaribia Yehova. Tena, alijifunza ufundi wenye ulimusaidia apate kazi haraka. Lakini zaidi ya yote, alikubali roho ya Yehova imuongoze. Mambo hayo yanatufundisha kabisa somo kubwa!—Mhubiri 12:1.

USIACHE MOYO WA MUTU YEYOTE UZIMIE KWA SABABU YAKE

Wakati alikuwa anamutumikia Sauli, mara nyingi Daudi alirudia nyumbani ili kuchunga kondoo, na wakati fulani alifanya hivyo kwa muda murefu. Ni wakati kama huo ndio Yese alimutuma Daudi ili aende kuona wakubwa wake watatu wenye walikuwa katika jeshi la Sauli. Daudi alikuwa mutiifu; kwa hiyo alipelekea ndugu zake chakula katika Bonde la Ela. Wakati alifika, alihuzunika kuona majeshi hayo mawili katika hali yenye tulizungumuzia kwenye mwanzo wa habari hii. Wamoja walikuwa ngambo moja ya bonde na wengine ngambo ingine, na walikuwa wanaangaliana.—1 Samweli 17:1-3, 15-19.

Daudi hakuweza kuvumilia hali hiyo. Namna gani jeshi la Yehova, Mungu anayeishi, linaweza kuogopa mwanadamu bure, tena mupagani? Daudi aliona kwamba maneno ya kuzarau ya Goliathi yalikuwa ya kumutukana Yehova moja kwa moja. Kwa hiyo, bila woga, akaanza kuambia maaskari kwamba atamupiga Goliathi na kumushinda. Kisha muda kidogo tu, Eliabu, ndugu mukubwa ya Daudi, alisikia mambo yenye alikuwa anasema. Kwa hiyo alikaripia mudogo yake kwa ukali, na kusema kwamba iko hapo tu ili kuona namna watu wanakufa kwenye vita. Lakini Daudi alimujibu hivi: “Sasa nimefanya nini? Je, halikuwa neno tu?” Kisha akaendelea kusema kwa uhakika wote kwamba atamushinda Goliathi, mupaka wakati mutu fulani alimuelezea Sauli maneno yake. Mufalme akaomba Daudi aletwe mbele yake.—1 Samweli 17:23-31.

Daudi alimuambia mufalme maneno haya yenye kutia moyo juu ya Goliathi: ‘Usiache moyo wa mutu yeyote uzimie [kwa sababu yake].’ Sauli na wanaume wake waliogopa sana kwa sababu ya Goliathi. Pengine walifanya kosa la kujilinganisha wenyewe na mutu huyo munene sana, kwa kuwazia namna urefu wao ulifikia tu sehemu ya tumbo ao ya kifua chake. Waliwazia namna ilikuwa mwepesi kwa mwanaume huyo mwenye silaha kuwaua. Lakini Daudi hakufikiri hivyo. Kama vile tutaona, aliona tatizo hilo kwa njia tofauti kabisa. Kwa hiyo, alisema iko tayari kupigana na Goliathi.—1 Samweli 17:32.

Sauli alikataa na kumuambia: ‘Wewe hauwezi kuenda juu ya huyu Mufilisti kupigana naye, kwa maana wewe ni muvulana tu, naye ni mwanaume wa vita tangu uvulana wake.’ Daudi alikuwa kabisa mutoto? Hapana, lakini alikuwa angali mudogo ili kuenda katika jeshi, na pengine alionekana kama kijana tu. Lakini Daudi alijulikana tayari kuwa mupiganaji mukubwa na inawezekana alikuwa na miaka 19 hivi wakati huo.—1 Samweli 16:18; 17:33.

Daudi alimuhakikishia Sauli kwa kumuelezea mambo yenye alifanya wakati simba na dubu walishambulia kondoo. Alikuwa anajisifu? Hapana. Daudi alijua namna gani aliweza kupata ushindi. Alisema hivi: ‘Yehova, aliyenikomboa kutoka katika makucha ya simba na kutoka katika makucha ya dubu, yeye ndiye atakayenikomboa kutoka mukononi mwa huyu Mufilisti.’ Sauli alifikia kukubali. Kwa hiyo alimuambia hivi: ‘Enda, na Yehova akuwe pamoja nawe.’—1 Samweli 17:37.

Unapenda kuwa na imani kama Daudi? Kama jibu ni ndiyo, jua kwamba imani ya Daudi haikuwa ndoto ao jambo fulani lenye haliwezi kufanyika. Alikuwa na imani katika Mungu wake kwa sababu ya mambo yenye alijua na mambo yenye alikutana nayo. Alijua kwamba Yehova ni Mulinzi mwenye upendo na Mutimizaji wa ahadi zake. Kama tunapenda kuwa na imani kama hiyo, tunapaswa kujifunza juu ya Mungu wa kweli mwenye kuzungumuziwa katika Biblia. Wakati tunaishi kulingana na mambo yenye tunajifunza, sisi pia tutaona kwamba matokeo mazuri yenye tutapata yatatia nguvu imani yetu.—Waebrania 11:1.

‘YEHOVA ATAKUTIA KATIKA MUKONO WANGU’

Mwanzoni, Sauli alijaribu kumuvalisha Daudi vitu vyake vya kujilinda navyo katika vita. Vilitengenezwa na shaba kama vile vya Goliathi, na inawezekana kati ya vitu hivyo kulikuwa vazi la chuma lenye kufanyizwa na mabamba yenye kuingiana. Lakini wakati Daudi alipima kutembea na vitu hivyo, akatambua mara moja kwamba hataweza kupigana navyo kwa sababu vilikuwa vikubwa na vyenye kilo sana. Alikuwa hajafanya mazoezi ya kuwa askari, kwa hiyo hakuwa anazoea kuvaa vitu kama hivyo, zaidi sana vitu vya Sauli, mutu murefu kuliko wote katika taifa la Israeli! (1 Samweli 9:2) Alitosha vitu hivyo vyote na kuvaa nguo yenye alikuwa anazoea kuvaa, ni kusema, nguo yenye muchungaji alikuwa anavaa wakati wa kulinda kondoo wake.—1 Samweli 17:38-40.

Daudi alibeba fimbo yake ya kuchunga nayo wanyama, kombeo, na alitia mufuko wake kwenye mabega. Wakati huo, kombeo ilionekana kuwa kitu cha bure tu, lakini kwa kweli ilikuwa silaha ya ajabu. Kwa sababu ilikuwa na mufuko mudogo wenye kuwa wazi wenye ulifungwa juu ya kamba mbili za ngozi, kombeo ilikuwa silaha yenye kufaa kwa ajili ya muchungaji. Angeweza kutia jiwe kwenye mufuko huo, na kuizungusha-zungusha mbio sana juu ya kichwa, na kisha angeachilia kamba moja. Kwa hiyo, jiwe lingepiga kwenye alivizia bila kukosea. Kwa sababu silaha hiyo ilikuwa ya muzuri, wakati fulani katika jeshi kulikuwa vikundi vya wapiga-kombeo.

Kisha kuchukua vifaa vyake, Daudi alienda mbio ili kupigana na adui wake. Tunaweza kuwazia namna Daudi anafanya sala yenye kutoka moyoni wakati anainama katika bonde nafasi kwenye muto umekauka na kuchagua majiwe mazuri tano madogo-madogo. Kisha anaenda kwenye nafasi ya kupigania. Haende polepole, lakini anakimbia!

Wakati Goliathi aliona adui wake, aliwaza nini? Biblia inasema kwamba Goliathi ‘alianza kumuzarau kwa sababu alikuwa muvulana tu, mwekundu, na mwenye sura nzuri.’ Goliathi alisema hivi kwa sauti kubwa na yenye kishindo: ‘Mimi ni imbwa hivi kwamba unijie na fimbo?’ Ni wazi kwamba aliona tu fimbo yenye Daudi alikuwa nayo, lakini hakuona kombeo. Alimulaani Daudi kwa jina la miungu ya Wafilisti na kuapa kwamba atapatia mwili wake wenye kuzaraulika ndege na wanyama wa pori.—1 Samweli 17:41-44.

Siku hiyo, jibu la Daudi lilionyesha kwamba alikuwa kabisa na imani kubwa. Wazia tu namna kijana mudogo anamulalamikia Goliathi: ‘Unakuja kwangu ukiwa na upanga na mukuki na fumo, lakini mimi ninakuja kwako nikiwa na jina la Yehova wa majeshi, Mungu wa vikosi vya Israeli, ambaye umemutukana.’ Daudi alijua kwamba silaha na nguvu za mwanadamu haviko vya maana sana. Goliathi alimuzarau Yehova Mungu, na Yehova alipaswa kufanya jambo fulani. Daudi alionyesha kwamba “vita ni vya Yehova.”—1 Samweli 17:45-47.

Daudi aliona unene wa Goliathi na silaha zake. Lakini Daudi hakuacha mambo hayo yamuogopeshe. Hakufanya makosa yenye Sauli na watu wa jeshi lake walifanya. Daudi hakujilinganisha na Goliathi. Lakini, aliona namna Goliathi alionekana wakati alilinganishwa na Yehova. Kwa sababu alikuwa na urefu wa metre 2,9 hivi, Goliathi alikuwa murefu kupita wanaume wengine wote. Lakini Goliathi hakuwa kitu kwa kumulinganisha na Mutawala Mukubwa wa ulimwengu wote. Kwa kweli, kama mwanadamu mwengine yeyote, Goliathi alikuwa kama kidudu tu, na kwa hiyo ilikuwa mwepesi sana kwa Yehova kumuharibu!

Daudi alienda mbio kwenye adui wake, na kukamata jiwe moja katika mufuko wake. Alitia jiwe hilo katika kombeo lake na kuizungusha-zungusha juu ya kichwa chake mupaka wakati kombeo hiyo ilianza kufanya makelele. Goliathi alimukaribia Daudi, pengine alikuwa nyuma ya mwenye kubeba ngao yake. Inawezekana urefu wa Goliathi ulimuletea magumu kwa sababu ni vigumu kwa mubeba-ngao wa urefu wa kawaida kuinua ngao juu kabisa ili kulinda kichwa cha mutu huyo murefu. Na ni kwenye kichwa cha Goliathi ndiko Daudi alivizia.—1 Samweli 17:41.

Daudi aliona kwamba hata mutu murefu na munene sana haiko kitu wakati analinganishwa na Yehova Mungu

Daudi aliachilia jiwe lake. Wazia kimya yenye ilikuwa wakati jiwe hilo lilifyatuka kuelekea Goliathi. Bila shaka Yehova alihakikisha kwamba Daudi anatumia jiwe moja tu ili kumuua Goliathi. Jiwe lilipiga kwenye alivizia, na kuingia ndani ya paji la uso wa Goliathi. Mutu huyo murefu na munene sana alianguka chini kwenye uso wake! Inawezekana mwanaume mwenye kubeba ngao alikimbia kwa sababu ya woga. Daudi alimukaribia Goliathi, alikamata upanga wake, na kumukata kichwa kwa kutumia upanga huo.—1 Samweli 17:48-51.

Mwishowe, Sauli na maaskari wake wakapata nguvu. Kwa sauti kubwa ya vita, walifuatilia Wafilisti. Vita ikakuwa kama vile Daudi alikuwa amemuambia Goliathi: “Yehova . . ., atawatia ninyi mukononi mwetu.”—1 Samweli 17:47, 52, 53.

Leo, watumishi wa Mungu hawafanye vita ya kimwili. Wakati wa kufanya hivyo umekwisha kupita. (Mathayo 26:52) Lakini, tunapaswa kabisa kuiga imani ya Daudi. Kama yeye, tunapaswa kumuona Yehova kuwa mutu wa kweli, Mungu mwenye tunapaswa tu kutumikia na kuogopa. Wakati fulani, tunaweza kujiona kuwa hatuna uwezo mbele ya magumu yetu, lakini magumu yetu ni bure mbele ya nguvu ya Yehova yenye haina mwisho. Kama tunamuchagua Yehova kuwa Mungu wetu na kutia imani yetu ndani yake kama Daudi, hakuna magumu ao matatizo yenye yanapaswa kutuogopesha. Hakuna jambo lenye Yehova anaweza kushindwa kumaliza!