Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mungu Iko na Huruma?

Mungu Iko na Huruma?

MAMBO YENYE UUMBAJI UNATUFUNDISHA

Huruma “ni uwezo wa kujitia pa nafasi ya mutu mwengine ao kujisikia namna anajisikia kwa kuwazia vile mambo yangekuwa ikiwa wewe ungekuwa katika hali ya mutu huyo.” Dr. Rick Hanson munganga wa magonjwa ya akili anasema kuwa uwezo wa kusikilia mutu huruma uko katika damu yetu.

FIKIRIA JAMBO HILI: Sababu gani wanadamu wameumbwa na huruma, sifa yenye viumbe wengine hawana? Biblia inaonyesha kama Mungu aliumba wanadamu kwa mufano wake. (Mwanzo 1:26) Tumeumbwa kwa mufano wa Mungu katika maana ya kwamba, tunaweza kuiga utu wake na kwa hiyo kuonyesha kiasi fulani cha sifa zake za muzuri. Kwa hiyo, wakati huruma inachochea watu wenye upendo kusaidia wengine, wanaiga Muumbaji mwenye huruma, Yehova Mungu.​—Mezali 14:31.

MAMBO YENYE BIBLIA INATUFUNDISHA JUU YA HURUMA YA MUNGU

Mungu anatusikilia huruma na hapendi kuona tunateseka. Kuhusu watu wa Israeli ya zamani wenye walivumilia utumwa mukali katika Misri na miaka 40 ya kuteseka katika jangwa, Biblia inasema hivi: “Katika taabu zao zote, yeye alitaabika.” (Isaya 63:9) Ona kwamba Mungu hakuona tu taabu yao. Angeweza kusikia maumivu yao. Alisema hivi: “Ninajua muzuri maumivu yenye wako nayo.” (Kutoka 3:7) Mungu anasema tena hivi: “Mutu yeyote mwenye anawagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.” (Zekaria 2:8) Wakati wengine wanatuumiza, yeye pia anaumia.

Biblia inatuhakikishia kuwa hata kama tunaweza kujilaumu na kujiona kuwa hatustahili Mungu atuonyeshe huruma, “Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu na anajua mambo yote.” (1 Yohana 3:19, 20) Mungu anatujua muzuri zaidi kuliko sisi wenyewe. Anajua muzuri hali zetu, mawazo, na namna tunajisikia. Anatusikilia huruma.

Tunaweza kumutegemea Mungu ili kupata kitulizo, hekima, na musaada, tukijua kama anatolea musaada wale wenye kuwa katika taabu

Maandiko yanatuhakikishia

  • “Utaita, na Yehova atajibu; utalilia musaada, na atasema, ‘Mimi huyu!’”​—ISAYA 58:9.

  • “‘Kwa maana ninajua muzuri mawazo yenye ninafikiria kuwaelekea ninyi,’ ni vile Yehova anasema, ‘mawazo ya amani, na hapana ya musiba, ili kuwapatia ninyi wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini. Na mutaniita na kuja na kusali kwangu, na nitawasikiliza.’”​—YEREMIA 29:11, 12.

  • “Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi. Je, hayaandikwe katika kitabu chako?”​—ZABURI 56:8.

MUNGU ANATUONA, ANATUELEWA, NA ANATUSIKILIA HURUMA

Kujua kama Mungu anatusikilia huruma, kunaweza kutusaidia kupambana na magumu? Tufikirie mufano wa Maria:

“Niliona kama maisha yalikuwa nguvu na yenye kukosa haki wakati nilipata maumivu ya kufiwa na mutoto wangu mwanaume wa miaka 18 kisha kupambana na kansere kwa miaka mbili. Nilimukasirikia Yehova kwa sababu hakumuponyesha na kuzuia kifo!

“Miaka sita kisha, rafiki mwenye upendo na mwenye huruma katika kutaniko alinisikiliza wakati nilimuelezea kuwa Yehova hakuwa ananipenda. Kisha kunisikiliza kwa saa nyingi bila kunikatiza, alitaja andiko lenye lilinigusa moyo sana. Ilikuwa 1 Yohana 3:19, 20, yenye kusema hivi: ‘Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu na anajua mambo yote.’ Dada huyo alinifasiria kama Yehova anaelewa taabu yetu.

“Hata hivyo, ilikuwa nguvu kuachana na kisirani yangu! Kisha nilisoma Zaburi 94:19, yenye kusema hivi: ‘Wakati mahangaiko yalinilemea, ulinifariji na kunituliza.’ Nilijisikia kama vile maandiko hayo yalikuwa tu yameandikwa kwa ajili yangu! Nilifikia kuelewa kama kuzungumuza na Yehova kuhusu taabu yangu kunatuliza, nikijua kwamba ananisikia na kunielewa.”

Ni jambo lenye kutia moyo sana kujua kama Mungu anatuelewa na kutusikilia huruma! Lakini sasa, sababu gani kuko mateso mengi? Ni kwa sababu Mungu anatupatia malipizi juu ya makosa yetu? Je, Mungu atafanya jambo fulani ili kuondoa mateso yote? Habari zenye kufuata zitajibia maulizo hayo.