Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Furahia Baraka ya Kutoa

Furahia Baraka ya Kutoa

“MOTOKARI inaweza kuondoka, lakini kijana Muchina abakie!” Alexandra alisikia maneno hayo wakati alikuwa anakaa ndani ya motokari, akingojea kuvuka mupaka kati ya inchi mbili za Amerika ya Kusini. Alishuka ili kuona jambo lenye lilikuwa linatendeka na kuona kijana mumoja Muchina akijikaza kuzungumuza Kihispania kibaya wakati alikuwa anajaribu kufasiria magumu yake ofisa mwenye kuchunga mupaka. Kwa sababu Alexandra alikuwa anaingia katika kutaniko la Mashahidi wa Yehova la luga ya Kichina, alijitolea ili kusaidia kutafsiri.

Mwanaume huyo alisema kwamba alikuwa mukaaji mwenye kukubaliwa na sheria lakini walikuwa wamemuiba feza na vitambulisho vyake. Mwanzoni, ofisa huyo hakukubali jambo hilo na akafikiri kwamba Alexandra alikuwa anafanya biashara ya watu. Mwishowe alikubali mafasirio ya mwanaume huyo, lakini alipaswa kulipa amande kwa sababu hakukuwa na vitambulisho vyenye kufaa. Kwa sababu hakukuwa na feza, Alexandra alijitolea ili kumukopesha dola 20. Mwanaume huyo alimushukuru sana na akasema kama atamurudishia zaidi ya dola 20. Alexandra alimuambia kwamba hakukuwa anatafuta faida; alifurahi kusaidia kwa sababu aliona kuwa hilo ndilo jambo la muzuri kufanya. Alipatia mwanaume huyo vichapo fulani vyenye kutegemea Biblia na akamutia moyo ajifunze Biblia pamoja na Mashahidi.

Inafurahisha moyo kusikia namna watu wanajitoa ili kusaidia watu wenye hawajue, na bila shaka watu wa dini zote na watu wenye hawana dini wanafanya matendo kama hayo. Ungekuwa tayari kujitoa kwa upendo katika njia hiyo? Ulizo hilo ni la maana kwa sababu Yesu alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Wanasayansi wamehakikisha pia jambo hilo kwa sababu wamevumbua kwamba kutoa kunakuletea faida. Tuone kama kunakuletea faida katika njia gani.

‘MUTOAJI MUCHANGAMUFU’

Mambo mbalimbali yameonyesha kwamba mara nyingi kuna uhusiano mukubwa kati ya kutoa na kuwa na furaha. Mutume Paulo aliandika kwamba ‘Mungu anamupenda mutoaji muchangamufu.’ Alikuwa anazungumuzia Wakristo wenye walitoa michango ili kusaidia waamini wenzao ambao walikuwa katika magumu. (2 Wakorintho 8:4; 9:7) Paulo hakusema kwamba walitoa kwa sababu walikuwa na furaha. Lakini walikuwa na furaha kwa sababu walitoa.

Kulingana na uchunguzi mumoja, kutoa “kunachochea sehemu fulani za ubongo zenye kuhusiana na raha, uhusiano na watu, na kutumainika, na kwa hiyo kunafanya mutu ‘ajisikie muzuri.’” Uchunguzi mwengine ulionyesha kwamba “kupatia mutu mwengine feza kuliletea mutu mwenye kutoa furaha zaidi, kuliko vile angejisikia ikiwa angezitumia yeye mwenyewe.”

Umekwisha kujisikia kwamba hauwezi kufanya mengi kwa sababu ya hali yako? Ukweli ni kwamba kila mutu anaweza kupata furaha ya kuwa ‘mutoaji muchangamufu.’ Wakati mutu anatoa na nia nzuri, haiko lazima atoe feza nyingi. Shahidi mumoja wa Yehova alituma ujumbe huu pamoja na muchango wake kwa wachapishaji wa gazeti hili: “Miaka hii yote nimeweza kutoa kiasi kidogo-kidogo tu cha feza kwenye Jumba la Ufalme.” Lakini, aliongezea hivi: “Yehova Mungu amenipatia mengi zaidi kuliko michango yenye nimetoa. . . . Asante kwa kufanya iwezekane kwangu kutoa zawadi hii; hilo linanitia moyo.”

Kwa kweli, kutoa haiko tu kupana feza. Kuko njia nyingi zingine za kutoa.

KUTOA NI MUZURI KWA AJILI YA AFYA YAKO

Kutoa kunakuletea faida wewe na watu wengine

Biblia inasema hivi: ‘Mwanamume mwenye fazili zenye upendo anaitendea kwa kuipa sawabu nafsi yake mwenyewe, lakini mutu mukatili anajiletea taabu.’ (Methali 11:17) Watu wenye fazili ao wema ni watoaji, wako tayari kutoa wakati wao, nguvu yao, wanahangaikia wengine, na kufanyia watu mambo mengine. Kufanya hivyo katika maisha kunawaletea faida katika njia nyingi, na faida kubwa zaidi ni kwamba kutoa ni muzuri kwa afya yao.

Uchunguzi mbalimbali umeonyesha kwamba wale wenye wanajitolea ili kusaidia wengine mara nyingi wanakuwa na maumivu madogo ya mwili na mahangaiko madogo kuliko wale wenye hawafanye hivyo. Kwa kawaida, wako na afya ya muzuri. Kutoa kunasaidia hata wale wenye kuwa na magonjwa yasiyopona, kama vile ugonjwa wa neva na SIDA, wakuwe na afya muzuri zaidi. Imeripotiwa kwamba kusaidia wengine kunawezesha watu wenye wanataka kutoka katika utumwa wa pombe, wasikuwe na mahangaiko mengi ya akili na kunaweza kuongeza uwezekano wa kuepuka kurudilia tabia yao.

Ili kufasiria sababu gani jambo hilo linatokea, inasemekana kwamba “kusikilia watu huruma, kuonyesha wema na kuwa tayari kutoa kunapunguza mawazo yasiyofaa.” Kutoa kunaweza pia kupunguza mahangaiko na kufanya damu isitembee haraka sana katika mwili. Na watu wenye bibi ao bwana yao alikufa waliacha kuonyesha alama za kushuka moyo wakati walijitolea ili kusaidia wengine.

Bila shaka, kutoa ni muzuri kwa ajili ya afya yako.

KUTOA KUNACHOCHEA WENGINE KUTOA

Yesu alitia moyo wanafunzi wake hivi: ‘Mukuwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi. Watawamwangia katika mufuko wa nguo zenu kipimo kizuri, kilichoshindiliwa, kilichotikiswa pamoja na kufurika. Kwa maana kwa kipimo munachopimia, watawapimia ninyi pia.’ (Luka 6:38) Wakati unatoa, mara nyingi watu wanachochewa kukuonyesha shukrani na wao pia wanakuwa tayari kutoa. Kwa hiyo, kutoa kunatia nguvu uhusiano na urafiki.

Kutoa kunatia nguvu uhusiano na urafiki

Watu wenye kufanya uchunguzi juu ya uhusiano kati ya watu wameona kwamba “watu wenye wanahangaikia wengine kila mara wanawachochea wengine kufanya hivyo pia.” Na hata, “kusoma tu juu ya matendo ya wema kunafanya watu wakuwe wenye kutoa zaidi.” Kulingana na uchunguzi mumoja “kila mutu katika kikundi anaweza kuchochea makumi ao hata mamia ya watu, wamoja kati yao ambao hajue na hajakutana nao.” Ni kusema, tendo moja la kutoa linaweza kuchochea watu wengine wakuwe tayari kutoa. Ungependa kuishi na watu kama hao? Kwa kweli, kungekuwa faida kubwa kama watu wengi zaidi wangezoea kutoa.

Mufano mumoja wenye kuonyesha faida ya kutoa, ulipitika katika Florida, inchi ya Amerika. Mashahidi fulani wa Yehova walijitolea ili kusaidia kisha kutokea kwa upepo mukubwa wenye uliharibu vitu vingi. Wakati walikuwa kwenye nyumba fulani wakingojea vifaa vya kutumia ili kuitengeneza, walitambua kama lupango ya jirani mumoja ilikuwa imeharibika, na wakajitolea kuitengeneza. Katika barua yenye jirani huyo aliandikia makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova, alisema hivi: “Nitaendelea kuwa mwenye shukrani. Niliona watu hawa kuwa kati ya watu wazuri zaidi wenye nimekutana nao.” Roho ya shukrani ilimuchochea atume muchango kwa ajili ya kazi yenye aliita kazi kubwa ya Mashahidi.

UIGE MUFANO WA MUTOAJI MUKUBWA ZAIDI

Jambo la maana lenye wanasayansi wamevumbua ni kwamba “inaonekana kuwa wanadamu wanazaliwa na tamaa ya kusaidia wengine.” Uchunguzi huo unaonyesha kwamba watoto “wanatenda kwa njia yenye kuhangaikia wengine hata mbele wajue kusema.” Sababu gani? Biblia inatoa jibu wakati inasema kwamba wanadamu waliumbwa ‘kwa mufano wa Mungu,’ ni kusema, wako na sifa kama za Mungu.​—Mwanzo 1:27.

Kutoa ni kati ya sifa nzuri za Muumbaji wetu Yehova Mungu. Ametupatia uzima na kila kitu chenye tuko nacho lazima ili kuwa na furaha. (Matendo 14:17; 17:26-28) Tunaweza kujua Baba yetu wa mbinguni na makusudi yake yenye upendo kwa ajili yetu kwa kujifunza Neno lake Biblia. Biblia inaonyesha pia kwamba Mungu amekamata mipango ili tukuwe na furaha wakati wenye kuja. * (1 Yohana 4:9, 10) Kwa sababu sifa ya kutoa inatoka kwa Yehova Mungu na kwa sababu umeumbwa kwa mufano wake, haishangaze kwamba kutoa, kwa kuiga Mungu, kunakuletea faida na kunafanya Mungu akukubali.​—Waebrania 13:16.

Unakumbuka Alexandra, mwenye tulitaja kwenye mwanzo wa habari hii? Mambo yalifikia kuwa namna gani? Hata kama mutu fulani mwenye alikuwa naye katika motokari alimuambia kama alikuwa amepoteza feza zake, mwanaume mwenye alisaidia aliita marafiki wake wenye walikuwa katika muji ambamo motokari ilisimama, na mara moja deni hilo la dola 20 lililipwa. Tena, mwanaume huyo alikubali jambo lenye Alexandra alimuambia na akaanza kujifunza Biblia. Kisha miezi tatu, Alexandra alifurahi kukutana tena na mwanaume huyo kwenye mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova wa luga ya Kichina katika inchi ya Peru. Ili kuonyesha shukrani yake kwa ajili ya mambo yote yenye Alexandra alimufanyia, mwanaume huyo alimualika yeye na watu wenye walisafiri pamoja naye kwenye mukusanyiko ili wakuje kula kwenye restora yake.

Kutoa na kusaidia wengine kunaleta furaha kubwa. Na zaidi sana ikiwa, kwa kufanya hivyo, unasaidia pia watu wafikie kumujua zaidi Mutoaji wa zawadi zote nzuri, Yehova Mungu! (Yakobo 1:17) Unafurahia baraka ya kutoa katika njia kama hiyo?

^ fu. 21 Ili kupata habari zaidi, ona kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova na kinapatikana pia kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com. Fungua kichwa VICHAPO > VITABU & BROSHUA.