Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NAMNA YA KUACHANA NA CHUKI

4 | Ukubali Musaada wa Mungu Juu ya Kuachana na Chuki

4 | Ukubali Musaada wa Mungu Juu ya Kuachana na Chuki

Fundisho ya Biblia:

“Tunda la roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, fazili, wema, imani, upole, kujizuia.”​WAGALATIA 5:22, 23.

Ile Iko na Maana Gani?

Mungu tu njo anaweza kutusaidia tupiganishe chuki. Roho yake takatifu inaweza kutusaidia tukomalishe sifa zenye pengine hatungeweza kukomalisha siye peke. Kuliko kujaribu kumaliza chuki siye wenyewe, ni muzuri tutumainie nguvu ya Mungu. Tukifanya vile, tutajionea kama Paulo alisema kweli wakati aliandika hivi: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.” (Wafilipi 4:13) Na bila shaka, tutaweza kusema: “Musaada wangu unatoka kwa Yehova.”​—Zaburi 121:2.

Mambo Yenye Unaweza Kufanya:

“Yehova amenibadilisha kabisa. Nilikuwa mutu wa jeuri, lakini sasa niko mutu mwenye kuishi kwa amani na wengine.”​—WALDO

Usali kwa Yehova kwa moyo wote. Umuombe akupatie roho yake takatifu. (Luka 11:13) Umuombe akusaidie ukomalishe sifa za muzuri mu maisha yako. Ujifunze mambo yenye Biblia inasema juu ya sifa zenye zinaweza kukusaidia upiganishe chuki. Sifa sawa vile upendo, amani, uvumilivu, na kujizuia. Fikiria namna unaweza kukomalisha zile sifa mu maisha yako. Na upitishe wakati pamoya na watu wenye wako najikaza kukomalisha zile sifa. Wale watu wanaweza ‘kukuchochea katika upendo na matendo ya muzuri.’​—Waebrania 10:24.