Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Kuwa Kiziwi Hakunizuie Kufundisha Wengine

Kuwa Kiziwi Hakunizuie Kufundisha Wengine

Nilibatizwa katika mwaka wa 1941, wakati nilikuwa na miaka 12. Lakini nilielewa kweli ya Biblia muzuri kabisa katika mwaka wa 1946. Sababu gani? Acha niwaelezee habari juu ya maisha yangu.

MWAKA wa 1910 hivi, wazazi wangu walitoka Tbilisi, Georgia, na kuhamia Kanada. Waliishi katika nyumba ndogo yenye ilikuwa katika shamba karibu na Pelly, Saskatchewan, mangaribi mwa Kanada. Nilizaliwa katika mwaka wa 1928, na nilikuwa mutoto wa mwisho kati ya watoto sita. Baba yangu alikufa miezi sita mbele nizaliwe, na mama yangu alikufa wakati nilikuwa mutoto mudogo. Kisha muda mufupi, Lucy, dada yangu mukubwa, alikufa wakati alikuwa na miaka 17. Kwa hiyo, Nick, mujomba wangu alinichunga mimi na wakubwa wangu.

Siku moja wakati nilikuwa ninajifunza kutembea, watu wa familia yangu waliniona niko ninakokota mukia ya farasi. Waliogopa kuwa farasi ingeniumiza, kwa hiyo, walinilalamikia kwa sauti kubwa ili niache. Lakini walikuwa nyuma yangu, na sikusikia namna walikuwa wananilalamikia. Jambo la kufurahisha ni kwamba, farasi haikuniumiza. Lakini, hiyo ndiyo siku watu wa familia yangu walijua kama nilikuwa kiziwi.

Rafiki mumoja wa familia yetu alisema kama itakuwa muzuri zaidi niende kusoma pamoja na watoto wengine viziwi. Kwa hiyo, Nick, mujomba wangu, alinituma kwenye masomo ya viziwi katika Saskatoon, Saskatchewan. Masomo hayo yalikuwa mbali sana na watu wa familia yetu, na kwa sababu nilikuwa tu na miaka tano, niliogopa sana. Ningeweza tu kutembelea watu familia yangu siku za mapumuziko na wakati tulikuwa tunafunga masomo. Mwishowe, nilijifunza luga ya ishara na nilifurahia kucheza na watoto wengine.

NINAJIFUNZA KWELI ZA BIBLIA

Katika mwaka wa 1939, dada yangu mukubwa Marion aliolewa na Bill Danylchuck, na wakaanza kutuchunga mimi na dada yangu Frances. Katika familia yangu, wao ndio walikuwa wa kwanza kujifunza pamoja na Mashahidi wa Yehova. Wakati wa mafungo ya masomo, walijikaza kufanya yao yote ili kunifundisha mambo yenye walikuwa wanajifunza katika Biblia. Haikuwa mwepesi kwetu kuzungumuza kwa sababu hawakujua luga ya ishara. Lakini wangeweza kuona namna nilikuwa ninafurahia kabisa mambo yenye nilikuwa ninajifunza juu ya Yehova. Nilielewa kuwa mambo yenye walikuwa wanafanya yalipaswa kupatana na mambo yenye Biblia inasema, kwa hiyo, nilienda pamoja nao katika kazi ya kuhubiri. Kisha muda mufupi nilipenda kubatizwa, na tarehe 5 Mwezi wa 9, 1941, Bill alinibatiza katika chombo kimoja cha chuma chenye kilikuwa na maji ya kutoka katika kisima. Maji hayo yalikuwa baridi sana!

Niko pamoja na kikundi cha viziwi kwenye mukusanyiko katika Cleveland, Ohio, katika mwaka wa 1946

Katika mwaka wa 1946, wakati nilirudia nyumbani wakati wa mafungo, tulihuzuria mukusanyiko katika Cleveland, Ohio, Amerika. Siku ya kwanza, dada zangu walikuwa wananiandikia mambo yenye yalikuwa yanafundishwa ili nifuate programu hiyo. Lakini siku ya pili, nilifurahi kujua kama kwenye mukusanyiko huo kulikuwa kikundi cha viziwi na mutu wa kutafsiri katika luga ya ishara. Mwishowe, nilifurahia programu hiyo, na ilikuwa jambo lenye kufurahisha sana kufikia kuelewa muzuri mambo yenye Biblia inafundisha!

KUFUNDISHA KWELI

Wakati huo, Vita ya Pili ya Ulimwengu ilikuwa imetoka tu kuisha, na watu walipenda kuonyesha kuwa wako washikamanifu kwa inchi zao. Lakini wakati nilirudia kutoka kwenye mukusanyiko na kuenda kwenye masomo, niliazimia kubakia mushikamanifu kwa Yehova. Kwa hiyo, Niliacha kusalimu bendera, kuimba wimbo wa taifa, na kufanya sikukuu mbalimbali. Niliacha pia kuenda kwenye kanisa pamoja na wanafunzi wenzangu. Walimu hawakufurahi na walijaribu kunitesa na kuniambia mambo ya uongo ili kunichochea nibadilishe mawazo yangu. Wanafunzi wenzangu walikuwa wanaona mambo yenye yalikuwa yanafanyika, na kwa sababu ya mambo hayo, nilipata nafasi nyingi za kuwahubiria. Wanafunzi wenzangu fulani, kutia ndani Larry Androsoff, Norman Dittrick, na Emil Schneider, walifikia kukubali kweli, na wangali wanamutumikia Yehova.

Wakati nilitembelea miji mingine, sikuzote nilifanya bidii ya pekee ili kuhubiria viziwi. Kwa mufano, katika Montreal, nilienda mahali viziwi wa eneo hilo walikuwa wanakutana. Nilihubiria Eddie Tager, kijana mumoja mwanaume mwenye alikuwa katika kikundi cha watu wenye jeuri. Mupaka alikufa mwaka jana, alikuwa katika kutaniko la luga ya ishara katika Laval, Quebec. Nilikutana pia na kijana mumoja mwenye kuitwa Juan Ardanez. Kama vile Waberoya wa zamani, alitafuta habari ili kuhakikisha kuwa mambo yenye alikuwa anajifunza yalitegemea Biblia. (Matendo 17:10, 11) Yeye pia alikubali kweli, na alikuwa muzee wa kutaniko katika Ottawa, Ontario, mupaka wakati alikufa.

Mahubiri ya barabarani mwanzoni mwa miaka ya 1950

Katika mwaka wa 1950, nilihamia Vancouver. Hata kama ninapenda kuhubiria viziwi, sitasahau hata kidogo mambo yenye nilijionea wakati nilihubiria mwanamuke mumoja mwenye kusikia mwenye aliitwa Chris Spicer; nilimuhubiria katika barabara. Alikubali kujiandikisha ili kupata magazeti kwa ukawaida na alipenda nizungumuze na bwana yake, Gary. Niliwatembelea nyumbani kwao, na tulikuwa na mazungumuzo ya murefu kwa kuandikiana. Kisha hapo hatukuonana tena. Lakini kisha kupita miaka fulani, nilishangaa wakati niliwaona wanakuja kunisalimia kwenye mukusanyiko katika Toronto, Ontario. Gary angebatizwa siku hiyohiyo. Jambo hilo lilinikumbusha kuwa ni jambo la maana sana kuendelea kuhubiri, kwa sababu hatuwezi kujua hata kidogo ikiwa mutu fulani mwenye tunahubiria atafikia kukubali kweli.

Kisha, nilirudia Saskatoon. Huko nilikutana na mwanamuke mwenye aliniomba nijifunze Biblia pamoja na watoto wake wawili wanawake wenye walikuwa mapasa, Jean na Joan Rothenberger, wenye walikuwa viziwi. Walikuwa wanasomea kwenye masomo ya viziwi kwenye mimi pia nilikuwa nimesomea. Kisha muda mufupi, watoto hao wanawake wawili walianza kuzungumuza na wanafunzi wenzao juu ya mambo yenye walikuwa wanajifunza. Mwishowe, wanafunzi tano wa somo lao wakakuwa Mashahidi wa Yehova. Mumoja kati yao alikuwa Eunice Colin. Nilikutana na Eunice kwa mara ya kwanza wakati nilikuwa katika mwaka wangu wa mwisho kwenye masomo ya viziwi. Wakati huo, alinipatia bonbon na kuniuliza ikiwa tunaweza kuwa marafiki. Kisha, akakuwa mutu wa maana sana katika maisha yangu. Akakuwa bibi yangu!

Mimi pamoja na Eunice katika mwaka wa 1960 na mwaka wa 1989

Wakati mama ya Eunice alivumbua kuwa Eunice alikuwa anajifunza Biblia, aliomba mukubwa wa masomo amusadikishe aache kujifunza. Hata kama alijaribu kumukataza na kutupa vichapo vyake vya kutumia ili kujifunza, Eunice aliazimia kubakia muaminifu kwa Yehova. Wakati alipenda kubatizwa, wazazi wake walimuambia hivi: “Kama unakuwa Shahidi wa Yehova, utatoka katika nyumba yetu!” Kwa hiyo, wakati alikuwa na miaka 17, Eunice alitoka kwao na akahamia katika familia moja ya Mashahidi. Aliendelea kujifunza na kisha akabatizwa. Wakati tulioana katika mwaka wa 1960, wazazi wake hawakufika kwenye ndoa yetu. Hata hivyo, kadiri miaka ilikuwa inapita, walituheshimia zaidi kwa sababu ya imani yetu na namna tulikomalisha watoto wetu.

YEHOVA AMENIHANGAIKIA

Mutoto wangu Nicholas pamoja na Deborah, bibi yake, wanatumikia kwenye Beteli ya Londres

Kwa sababu tulikuwa wazazi viziwi, ilikuwa vigumu kwetu kukomalisha vijana saba wanaume wenye kusikia. Lakini, tulihakikisha kuwa wanajua luga ya ishara ili tuweze kuzungumuza nao muzuri na kuwafundisha kweli. Ndugu na dada katika kutaniko walitusaidia sana. Kwa mufano, muzazi mumoja alituandikia kwenye karatasi kuwa mutoto wetu mumoja alikuwa anasema maneno ya mubaya katika Jumba la Ufalme. Tulimusaidia bila kukawia. Watoto wangu ine, James, Jerry, Nicholas, na Steven, ni wazee wa kutaniko na wanamutumikia Yehova kwa uaminifu pamoja na bibi zao na familia zao. Pia, Nicholas na bibi yake, Deborah, wanasaidia kutafsiri katika luga ya ishara kwenye Beteli ya Uingereza, na Steven na bibi yake, Shannan, wanatumika katika kikundi cha kutafsiri katika luga ya ishara kwenye Beteli ya Amerika.

Watoto wangu James, Jerry, na Steven na bibi zao wanategemeza katika njia mbalimbali kazi ya kuhubiri katika luga ya ishara

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, mwezi moja mbele ya kueneza miaka 40 katika ndoa yetu, Eunice alikufa kwa sababu ya ugonjwa wa kansere. Wakati wote wenye alipambana na ugonjwa huo, tumaini lake katika ufufuo liliendelea kumutia nguvu. Ninangojea kwa hamu sana wakati nitamuona tena.

Faye na James, Jerry na Evelyn, Shannan na Steven

Katika Mwezi wa 2, 2012, nilianguka na nikavunjika kiuno. Nilitambua kuwa nilikuwa na lazima ya musaada, kwa hiyo, nilienda kuishi pamoja na mutoto wangu mumoja pamoja na bibi yake. Sasa tuko katika Kutaniko la Luga ya Ishara la Calgary, na ninaendelea kuwa muzee katika kutaniko hilo. Kwa kweli, hii ndiyo mara yangu ya kwanza kuwa katika kutaniko la luga ya ishara! Kwa hiyo, namna gani niliendelea kufanya urafiki wangu pamoja na Yehova ukuwe wenye nguvu katika miaka hiyo yote yenye nilifanya katika kutaniko la luga ya Kiingereza? Yehova alinisaidia. Alitimiza ahadi yake ya kuhangaikia watoto wenye hawana baba. (Zaburi 10:14) Niko mwenye shukrani sana kwa wote wenye walikuwa tayari kuniandikia mambo yenye yalikuwa yanafundishwa, wenye walijifunza luga ya ishara, na kujikaza sana ili kutafsiri katika luga ya ishara kwa ajili yangu.

Ninasoma masomo ya mapainia katika luga ya ishara wakati nilikuwa na miaka 79

Wakati fulani sikuelewa mambo yenye yalikuwa yanasemwa na wakati fulani niliwaza kuwa hakuna mutu mwenye anaelewa namna ya kusaidia viziwi. Katika hali kama hizo, wakati nilijisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo na kupenda kuacha kabisa kumutumikia Yehova, nilifikiria maneno haya yenye Petro alimuambia Yesu: ‘Bwana, tutaenda kwa nani? Wewe uko na maneno ya uzima wa milele.’ (Yohana 6:66-68) Kama vile ndugu na dada wengi viziwi wenye wamekuwa katika kweli kwa miaka mingi, nimejifunza namna ya kuonyesha uvumilivu. Nimejifunza kumutegemea Yehova na tengenezo lake, na hilo limeniletea faida nyingi. Sasa kuko vichapo vingi katika luga yangu, na niko mwenye furaha kwa sababu ninaweza kuhuzuria mikutano na mikusanyiko katika Luga ya Ishara ya Amerika. Kwa kweli, nimekuwa na maisha yenye furaha na yenye kuleta baraka kwa kumutumikia Yehova, Mungu wetu mukubwa.