Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Wafanya-biashara wenye walikuwa wanauzisha wanyama katika hekalu la Yerusalemu wangeweza kuitwa kabisa ‘wanyanganyi’?

HABARI yenye kuwa katika Injili ya Mathayo inaonyesha kama “Yesu aliingia katika hekalu na kuwafukuza wale wote waliokuwa wakiuza [wakiuzisha] na kununua katika hekalu, na kuzipindua meza za wale waliokuwa wakibadili pesa na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa. Naye akawaambia: ‘Imeandikwa, “Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,” lakini ninyi munaifanya kuwa pango la wanyanganyi.’”​—Mt. 21:12, 13.

Maandishi ya historia ya Wayahudi yanaonyesha kama wafanya-biashara wenye walikuwa wanauzisha katika hekalu, walikuwa wanatendea watu kwa udanganyifu kwa kuwawekea bei kali. Kwa mufano, maandishi ya Mishnah (Keritot 1:7) yanazungumuzia hali fulani yenye ilitokea katika miaka kati ya 1 na 100 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati bei ya njiwa-tetere wawili wa kutoa zabihu ilipanda na kuwa dinari moja ya zahabu. Hiyo ilikuwa sawa na mushahara wenye mufanyakazi mwenye hana ufundi angelipwa kisha kutumika kwa siku 25. Watu masikini walikubaliwa kutoa njiwa-tetere ao njiwa kuwa zabihu; lakini, hata bei ya ndege hao ilikuwa imepanda sana. (Law. 1:14; 5:7; 12:6-8) Rabbi Simeon ben Gamaliel, alihuzunishwa na hali hiyo na alipunguza hesabu ya zabihu zenye watu walipaswa kutoa na hilo lilifanya bei ya njiwa-tetere wawili ilishuka, sasa mutu angeweza kutumika kwa saa ili kuuza njiwa hao.

Kulingana na mafasirio hayo, Yesu alikuwa na sababu ya kuita wafanya-biashara wenye walikuwa katika hekalu, ‘wanyanganyi’ kwa sababu ya udanganyifu na pupa yao.