Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Kubwa

Chembe Zako—Zinaweka Habari Nyingi Sana!

Chembe Zako—Zinaweka Habari Nyingi Sana!

KATIKA mwaka wa 1953, James Watson na Francis Crick, wanabiolojia wa molekuli, walichapisha jambo fulani lenye walivumbua. Jambo hilo lilikuwa la maana sana kuhusu namna watu walikuwa wanaelewa uzima kulingana na sayansi. Walikuwa wamevumbua kuwa ADN inafanyizwa na sehemu mbili zenye kujikunja-kunja. * ADN hiyo yenye kuwa kama nyuzi, inapatikana mara nyingi katika kiini cha chembe, iko na habari zenye kufichwa ao “kuandikwa.” Hilo linafanya chembe zenye uzima zikuwe na uwezo wa kuweka habari nyingi sana. Uvumbuzi huo wenye kushangaza ulileta mabadiliko katika biolojia (sayansi yenye kujifunza juu ya viumbe vyenye uzima)! Habari zenye “kuandikwa” katika chembe ziko na kusudi gani? Na jambo lenye kushangaza zaidi ni hili: Namna gani zilifika humo?

SABABU GANI CHEMBE ZIKO NA LAZIMA YA HABARI?

Umekwisha kujiuliza namna gani mbegu kidogo inakuwa muti ao namna gani mbegu ya uzazi ya mwanaume na mbegu ya uzazi ya mwanamuke zinapounganishwa zinakuwa mutu? Umekwisha kujiuliza namna gani uliriti tabia zako? Habari zenye kuwa katika ADN zinaweza kukusaidia kupata majibu.

Karibu chembe zote ziko na ADN, molekuli za ajabu sana zenye kufanana ngazi ndefu zenye kujikunja-kunja. Katika chembe za uriti, ao ADN zote za mwili, inakadiriwa kuwa ngazi hizo ziko na “vipandio (éscaliers)” vya kemikali miliare 3. Wanasayansi wanaita vipandio hivyo kuwa ni mapasa kwa sababu kila kipandio kinafanyizwa na sehemu mbili za kemikali, na wakati zinawekwa pamoja zinakuwa ine. Kwa kutumia herufi ya kwanza ya kila kemikali, zinaandikwa kwa kifupi A, C, G na T; hizo ni herufi nyepesi za alfabeti. * Katika mwaka wa 1957, Crick alisema kama namna vipandio hivyo vinapangwa ndiyo inafanyiza habari zenye kufichwa. Kuanzia mwaka wa 1961 na kuendelea, wanasayansi walianza kuelewa habari hizo.

Habari, ziwe za picha, sauti, ao maneno, zinaweza kuchungwa na kutumikishwa katika njia mbalimbali. Kwa mufano, ordinatere zinafanya hivyo kwa njia ya kielektroniki. Chembe zenye uzima zinachunga na kutumikisha habari kwa njia ya kemikali, ADN ndiyo sehemu kubwa katika kazi hiyo. ADN inapitishwa wakati chembe zinagawanyika na wakati viumbe vinazaana; inaonekana kuwa uwezo huo ndio unapitisha tabia.

Namna gani chembe zinatumia habari? Fikiria ADN kama vile maagizo juu ya namna ya kupika chakula mbalimbali, kila maagizo juu ya kupika chakula fulani inafuatwa hatua kwa hatua, na kila hatua inaelezwa muzuri kupitia maandishi yenye kuwa wazi. Lakini kuliko chakula hicho kikuwe keki ao biskuti, pengine kinakuwa chou ao ngombe. Katika chembe zenye uzima, hatua hizo zinajiendesha zenyewe kama mashini, na hilo linafanya ziwe za ajabu sana na ngumu zaidi kueleweka.

Habari zenye kuwa katika chembe ya bakteria zinaweza kujaza kitabu chenye kurasa 1000

Habari zenye kuwa katika chembe za uriti zinachungwa mupaka wakati kunakuwa lazima, pengine ili kuweka chembe mupya nafasi ya chembe zenye kuzeeka ao kufa, ao ili kupitisha tabia kwa watoto. ADN iko na habari za kiasi gani? Fikiria bakteria, kiumbe kimoja kati ya viumbe vidogo sana. Mwanasayansi Mujerumani Bernd-Olaf Küppers alisema hivi: “Kwa njia yenye wanadamu wanaweza kuelewa, tunaweza kusema kama habari zenye kuwa katika molekuli ya chembe ya bakteria zinaweza kujaza kitabu chenye kurasa 1000.” Ndiyo sababu profesa wa kemia, David Deamer, aliandika hivi: “Hata aina nyepesi sana ya uzima ni yenye kushangaza sana.” Chembe za uriti za mwanadamu zinaweza kulinganishwa na nini? Küppers anasema hivi: “[Chembe hizo] zinaweza kujaza chumba cha kuwekea vitabu chenye kujaa maelfu ya vitabu.”

“YANAANDIKWA KWA NAMNA TUNAWEZA KUELEWA”

Küppers anasema kama maandishi yenye kuwa katika ADN yanaweza kulinganishwa na luga. Anaonyesha kwamba, “kama luga ya wanadamu, luga ya molekuli ya chembe za uriti iko pia na mupangilio wake wa maneno.” Kwa kifupi, ADN iko na sarufi ao kanuni zenye kuongoza kwa uangalifu namna maagizo yanafanywa na kutimizwa.

“Maneno” na “misemwa” katika ADN vinafanyiza “maagizo” mbalimbali yenye inaongoza kutengenezwa kwa proteini na vitu vingine vyenye kufanyiza chembe mbalimbali za mwili. Kwa mufano, “maagizo” yanaweza kusaidia katika kufanyiza chembe za mifupa, chembe za mishipa, chembe za neva, ao chembe za ngozi. Mwanamageuzi Matt Ridley, alisema hivi: “Nyuzi ya ADN ni habari, ujumbe wenye kuandikwa katika maagizo ya kemikali, kila kemikali inaandikwa kwa herufi moja. Pengine ni vigumu kuamini jambo hilo, lakini maagizo hayo yanaandikwa kwa namna tunaweza kuelewa.”

Daudi, muandikaji mumoja wa Biblia, alimuambia Mungu hivi katika sala: “Macho yako yalikiona kiini-tete changu, na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa.” (Zaburi 139:16) Kwa kweli, katika andiko hilo, Daudi alitumia maneno ya mufano. Hata hivyo, Daudi alisema kweli kabisa, kama waandikaji wengine wa Biblia. Hakuna hata mumoja wao mwenye aliongozwa na habari za kutunga ao hadisi za watu wa zamani.—2 Samweli 23:1, 2; 2 Timotheo 3:16.

Namna gani mutoto anariti tabia kutoka kwa wazazi wake?

NAMNA GANI MAANDISHI YALIFIKA HUMO?

Mara nyingi, wakati wanasayansi wanajaribu kufasiria jambo fulani lenye halieleweke, hilo linatokeza jambo lingine. Ni vile ilikuwa juu ya kuvumbuliwa kwa ADN. Wakati ilijulikana kama ADN iko na habari zenye kufichwa, watu fulani wenye kufikiri sana walijiuliza, ‘Namna gani maandishi yalifika humo?’ Ni kweli, hakuna hata mutu mumoja mwenye aliona namna molekuli ya kwanza ya ADN ilifanywa. Kwa hiyo, sisi wenyewe tunapaswa kufanya maamuzi. Lakini, maamuzi hayo hayapaswe kuwa ya kuwazia tu. Fikiria mifano yenye kufuata.

  • Katika mwaka wa 1999, vipande vya vyombo fulani vya zamani sana vyenye kutengenezwa kwa udongo vilivumbuliwa katika inchi ya Pakistani. Vilikuwa na alama zisizo za kawaida na mupaka leo maana ya alama hizo haijajulikana. Hata hivyo, vinaonwa kuwa vilitengenezwa na mwanadamu.

  • Miaka fulani kisha Watson na Crick kuvumbua muundo wa ADN, wanafizikia wawili walisema kuwa watafanya uchunguzi juu ya sauti za radio zenye kupita katika anga.Walianzisha uchunguzi ili kujua ikiwa kuko watu wenye akili wenye kuishi inje ya dunia. Sayansi inaendelea kufanya uchunguzi huo.

Hilo linatufundisha nini? Wakati watu wanaona habari fulani, wanatambua kuwa ilitokana na viumbe wenye akili, iwe habari hiyo ni alama kwenye vyombo vya udongo ao sauti za radio zenye kupita katika anga. Hawana lazima ya kuona namna habari hiyo inafanywa ili kuchukua uamuzi. Lakini, wakati wanadamu walivumbua maagizo ya ajabu sana, ni kusema, maagizo ya uzima, watu wengi walisahau kuwa inaomba mutu fulani mwenye akili ili kutokeza maagizo hayo. Walisema kuwa ADN ilijitokeza yenyewe. Jambo hilo linapatana na akili? Ni la kweli? Linapatana na sayansi? Wanasayansi wengi wenye kuheshimika wanasema hapana. Kati yao kuko Musomi Gene Hwang na Profesa Yan-Der Hsuuw. Fikiria mambo wanasema.

Musomi Gene Hwang anajifunza mambo ya hesabu juu ya chembe za uriti. Wakati fulani aliamini mageuzi, lakini mambo yenye amejifunza yamebadilisha mawazo yake. Aliambia gazeti Amuka! hivi: “Kujifunza chembe za uriti kunasaidia kuelewa uzima na ujuzi huo unanifanya nishangazwe sana na hekima ya Muumbaji.”

Profesa Yan-Der Hsuuw anasimamia uchunguzi wa kiini-tete (embryon) kwenye masomo moja ya juu katika inchi ya Taiwan. Na yeye alikuwa anaamini mageuzi, lakini uchunguzi wake ulimusaidia kubadilisha mawazo yake. Juu ya namna chembe zinajigawanya na kujipanga, alisema hivi: “Chembe zenye kufaa zinapaswa kutokezwa kwa utaratibu wenye kufaa na kwenye nafasi zenye kufaa. Kwanza chembe zenye kufanana zinajikusanya pamoja na kisha zinajikusanya tena ili kufanyiza viungo mbalimbali na miguu na mikono. Ni fundi gani anaweza kuandika maagizo kwa ajili ya hatua kama hizo? Lakini maagizo juu ya namna kiini-tete kinakomaa yanaandikwa muzuri sana katika ADN. Wakati ninachunguza uzuri huo, hilo linafanya niamini kuwa uzima uliumbwa na Mungu.”

Gene Hwang (kushoto) na Yan-Der Hsuuw

NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Ndiyo! Ikiwa ni Mungu ndiye aliumba uzima, ni jambo la haki asifiwe, wala si mageuzi. (Ufunuo 4:11) Tena, kama tuliumbwa na Muumbaji mwenye hekima zaidi, tuko na sababu ya muzuri ya kuwa duniani. Hilo halingewezekana kama uzima ulitokana na hatua zenye hazikupangwa. *

Kwa kweli, watu wenye kufikiri wanatamani sana kupata majibu yenye kufurahisha. Viktor Frankl, profesa mwenye alikuwa anafundisha juu ya mufumo wa neva na juu ya magonjwa ya akili, alisema kama “kutafuta kusudi la maisha ndilo jambo lenye mwanadamu anahangaikia sana.” Katika maneno mengine, tuko na uhitaji wa kiroho wenye tunapaswa kutimiza. Uhitaji huo unaeleweka ikiwa tu tuliumbwa na Mungu. Lakini, kama tuliumbwa na Mungu, alitupatia namna ya kutimiza uhitaji huo wa kiroho?

Yesu Kristo alijibia ulizo hilo kwa kusema hivi: ‘Mwanadamu ataishi, si kwa mukate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova [ao Mungu].’ (Mathayo 4:4) Maneno ya Yehova, yenye kuandikwa katika Biblia, yametimiza uhitaji wa kiroho wa watu wengi sana. Hilo limefanya maisha yao yakuwe na maana na wamepata tumaini kwa ajili ya wakati unaokuja. (1 Wathesalonike 2:13) Biblia inaweza kukusaidia wewe pia. Kwa kweli, ni muzuri uchunguze kitabu hicho cha pekee.

^ fu. 3 Watson and Crick walisaidiwa na kazi za wanasayansi wa mbele yao juu ya ADN yenye kumaanisha asidi deoksiribonyukilia.—Soma kisanduku “ Tarehe za Maana Juu ya ADN.”

^ fu. 6 Herufi hizo ni adenine, cytosine, guanine, na thymine.

^ fu. 22 Ulizo juu ya uumbaji na mageuzi linazungumuziwa sana katika broshua Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai na Uhai—Ulitokana na Muumba? Unaweza kupata broshua hizo kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com.