Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Uwezo wa Ajabu wa Kusikia wa Panzi Anayeishi Katika Miti

Uwezo wa Ajabu wa Kusikia wa Panzi Anayeishi Katika Miti

PANZI wa Amerika ya Kusini anayeishi katika miti (Copiphora gorgonensis) ana masikio ambayo hayafikie urefu wa milimeta moja, lakini masikio hayo yanafanya kazi kama masikio ya mwanadamu. Mududu huyo anaweza kutofautisha sauti ya vitu mbalimbali vilivyo mbali sana. Kwa mufano, anaweza kujua tofauti kati mulio wa panzi mwengine na sauti kubwa ya popo ambaye anawinda.

SIKIO LA PANZI ANAYEISHI KATIKA MITI

Fikiria hili: Masikio ya panzi huyo yako kwenye miguu yake miwili ya mbele. Kama vile masikio ya mwanadamu, masikio ya panzi huyo yanavuta sauti, yanapatanisha sauti hiyo na kitu fulani, na kuchunguza ni mara ngapi sauti hiyo inalia. Lakini wanasayansi wamegundua kwamba kuna tundu nyembamba lenye kujaa umajimaji ndani ya sikio la panzi huyo ambalo linafanana na mupira murefu wenye kujaa hewa. Tundu hilo ndani ya sikio lake, ambalo wanasayansi wameita tundu la kusikia, linafanya kazi kama sehemu ya ndani kabisa ya sikio la wanyama wenye kunyonyesha lakini ni ndogo zaidi. Tundu hilo la kusikia ndilo linamufanya panzi huyo awe na uwezo wa ajabu wa kusikia.

Daniel Robert, mwalimu wa Sayansi ya Viumbe Vilivyo na Uzima Kwenye Masomo ya Juu ya Bristol huko Uingereza, anasema kwamba uvumbuzi huo utasaidia mainjinia ao mafundi “kutengeneza vyombo vya kusikia vinavyofanana na sikio la asili ambavyo ni vidogo zaidi na vyenye uwezo muzuri zaidi wa kusikia kuliko vile ambavyo vimekwisha kutengenezwa.” Wachunguzi wanaamini kwamba katika miaka inayokuja jambo hilo litasaidia kutengeneza vyombo vya kiteknolojia vyenye sauti inayoenda kwa mwendo wa haraka sana, kutia ndani vyombo vya hospitali vinavyochukua picha za sehemu za mwili.

Unawaza namna gani? Uwezo wa ajabu wa kusikia wa panzi anayeishi katika miti ulijifanya wenyewe? Ao je, uliumbwa?